Bunge lapitisha Muswada unaotaka wake wa Marais na Maspika wastaafu kulipwa kiinua mgongo

Bunge lapitisha Muswada unaotaka wake wa Marais na Maspika wastaafu kulipwa kiinua mgongo

Hii nchi aliyenacho huongezewa asienacho hupokwa zaidi.
Bunge limepokea msaada na kuupitisha ili wenza wa viongozi wastaafu walipwe mafao ya kustaafu. Sio vibaya kwa kuwa hoja ina mashiko kwa wahusika na ilitolewa na mmoja wa wanufaika aliomo bungeni.
Wananchi wa kawaida waliofanya kazi na kustaafu hadi leo wanapigania haki zao za madai ya kustaafu lakini hawajalipwa na bunge inalijua hili. Serikali inalijua lakini wazee hawa wanyonge hawana mtu wa kuwasimania na kuhakikisha wanalipwa. Hivi kweli hii ndio Tanzania waliyoiacha mwl. Nyerere na Karume. Mbona wenye sauti hawa wajali wanyonge.
Bunge na Serikali simamieni haki wazee wastaafu na wasio na wakuwasimania walipwe haki zao za madai ya kustaafu.

Sent from my Infinix X657C using JamiiForums mobile app
 
Kwenye kipindi hiki kigumu,ni kweli kuna ulazima wa kuongeza gharama za kuendesha serikali!?
Ma CCM, yanamuonea huruma mke wa waziri mkuu! Ambaye kwanza anabiashara zake, harali na haramu, watoto wapo sekta nyeti,
Akaunti imenona! Kwanini hii huruma wasipewe vijana wanaomaliza vyuo na kukosa ajira, vijana wapewe hata 400K, kwa mwezi! Ili kukidhi, mahitaji Yao, mpaka watakapo pata ajira,
Wanasema hao tayari washachukua chao mapema kwenye mikopo ya elimu yajuu hivyo ukiwapa tena nchi itaingia hasara
 
Bunge limepitisha muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali namba 4 wa mwaka 2023 ambapo moja ya marekebisho katika sheria ya Mafao ya Kustaafu katika Utumishi wa kisiasa inapendekezwa Wenza (Mke/Mume) wa Marais Wastaafu, Wenza wa Makamu wa Rais Wastaafu na Wenza wa Mawaziri Wakuu Wastaafu walipwe kiinua mgongo kwa kipindi cha uongozi wa Wenza
wao.

Akiwasilisha marekebisho hayo leo Oktober 31,2023 wakati wa kikao cha Bunge Mjini Dodoma, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Dk. Eliezer Feleshi amesema kuwa vifungu vipya vya 9A, 12A na 14A vinapendekezwa kuongezwa katika Sheria ya Mafao ya Kustaafu katika Utumishi wa Kisiasa, Sura ya 225.

Sambamba na marekebisho hayo, vifungu vya 11, 13 na 15 vinapendekezwa kurekebishwa ili kuweka utaratibu wa malipo ya fadhila kwa Wenza wa Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu endapo watafariki wakiwa madarakani au baada ya kumaliza muda wao na kufariki kabla ya kulipwa mafao au stahiki zao.

Kwa mujibu wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Kifungu cha 18 kinapendekezwa kurekebishwa ili kuweka utaratibu wa wenza wa Spika Mstaafu aliyefariki kupokea mafao ya pensheni ya kila mwezi.

Muswada huo uliopitishwa utawasilishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aweze kuutazama muswada huo na akiuridhia atasaini ili iwe sheria.

#MillardAyoBUNGENI
Upumbavu wa Bunge na Watawala unaenda kuwabebesha mzigo mzito walipakodi ambao hawana maji na umeme wa uhakika wala huduma bora za afya.


Hii ndiyo CCM ambayo imeamua kufanya itakavyo kwa sababu inaamini inaongoza mazuzu.

Haya ndo yanayoenda kuiangusha muda si mrefu kwenye sanduku la kura
 
Watu wanalipa tozo mbalimbali, wanalipa kodi mbalimbali, hali ni ngumu, maisha yamewapiga Watanzania.

Badala ya Serikali kuleta muswada wa kubana matumizi yasiyo ya lazima ili kuwapa unafuu Watanzania, yenyewe inaleta muswada wa kuzigawa fedha za Watanzania kwa kikundi kidogo cha watu ambacho hata hivyo kimekuwa kikifaidi mema ya Nchi kwa muda mrefu kabisa.

Mungu mwenye enzi, nguvu na uweza wa ajabu aingilie kati suala hili. Tunaodhani wangekuwa msaada kwa Wananchi, hao ndo wanakuwa GENGE la majizi na mafisadi.

Wabunge nao wakiamua tu, wanajiongezea posho na marupurupu ya kila aina.

Allah Akbar.
 
Bunge limepitisha muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali namba 4 wa mwaka 2023 ambapo moja ya marekebisho katika sheria ya Mafao ya Kustaafu katika Utumishi wa kisiasa inapendekezwa Wenza (Mke/Mume) wa Marais Wastaafu, Wenza wa Makamu wa Rais Wastaafu na Wenza wa Mawaziri Wakuu Wastaafu walipwe kiinua mgongo kwa kipindi cha uongozi wa Wenza
wao.

Akiwasilisha marekebisho hayo leo Oktober 31,2023 wakati wa kikao cha Bunge Mjini Dodoma, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Dk. Eliezer Feleshi amesema kuwa vifungu vipya vya 9A, 12A na 14A vinapendekezwa kuongezwa katika Sheria ya Mafao ya Kustaafu katika Utumishi wa Kisiasa, Sura ya 225.

Sambamba na marekebisho hayo, vifungu vya 11, 13 na 15 vinapendekezwa kurekebishwa ili kuweka utaratibu wa malipo ya fadhila kwa Wenza wa Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu endapo watafariki wakiwa madarakani au baada ya kumaliza muda wao na kufariki kabla ya kulipwa mafao au stahiki zao.

Kwa mujibu wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Kifungu cha 18 kinapendekezwa kurekebishwa ili kuweka utaratibu wa wenza wa Spika Mstaafu aliyefariki kupokea mafao ya pensheni ya kila mwezi.

Muswada huo uliopitishwa utawasilishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aweze kuutazama muswada huo na akiuridhia atasaini ili iwe sheria.

#MillardAyoBUNGENI
Wanapeana tu ulaji ****nina zao.
 
Watu wanalipa tozo mbalimbali, wanalipa kodi mbalimbali, hali ni ngumu, maisha yamewapiga Watanzania.
Badala ya Serikali kuleta muswada wa kubana matumizi yasiyo ya lazima ili kuwapa unafuu Watanzania, yenyewe inaleta muswada wa kuzigawa fedha za Watanzania kwa KIKUNDI kidogo cha watu ambacho hata hivyo kimekuwa kikifaidi mema ya Nchi kwa muda mrefu kabisa.

Mungu mwenye enzi, nguvu na uweza wa ajabu aingilie kati suala hili.
Tunaodhani wangekuwa msaada kwa Wananchi, hao ndo wanakuwa GENGE la majizi na mafisadi.

Wabunge nao wakiamua tu, wanajiongezea posho na marupurupu ya kila aina.
Allah Akbar.
Luka 19:26
“Akawajibu, ‘Nawaambia kwamba kila aliye na kitu, ataongezewa. Lakini yule asiye na kitu, hata alicho nacho atanyangʼanywa.
 
Watu wanalipa tozo mbalimbali, wanalipa kodi mbalimbali, hali ni ngumu, maisha yamewapiga Watanzania.

Badala ya Serikali kuleta muswada wa kubana matumizi yasiyo ya lazima ili kuwapa unafuu Watanzania, yenyewe inaleta muswada wa kuzigawa fedha za Watanzania kwa kikundi kidogo cha watu ambacho hata hivyo kimekuwa kikifaidi mema ya Nchi kwa muda mrefu kabisa.

Mungu mwenye enzi, nguvu na uweza wa ajabu aingilie kati suala hili. Tunaodhani wangekuwa msaada kwa Wananchi, hao ndo wanakuwa GENGE la majizi na mafisadi.

Wabunge nao wakiamua tu, wanajiongezea posho na marupurupu ya kila aina.

Allah Akbar.
Hii ingelitufanya wtanxania tuasi nchi, lkn tumelala ndiyo maana wanafanya watakavyo
 
Mtu akiwa kiongozi Tanzania huamini yeye ana akili kuliko yeyote yule na ndio mwenye haki kuliko raia yeyote yule na mali asili yeyote ile ambayo iko chini yake hiyo ni mali yake.
 
Taifa la Tanzania halihitaji hawa wanasiasa kukomboa watu bali linahitaji sasa nguvu ya umma itakayowapiga ambush maharamia waliojitwalia Taifa hili na kulifanya mali yao binafsi.

Ukombozi utakaofanyika ndio utaleta tija na heshima tuitakayo wote kama watanzania,
 
Watu wanalipa tozo mbalimbali, wanalipa kodi mbalimbali, hali ni ngumu, maisha yamewapiga Watanzania.

Badala ya Serikali kuleta muswada wa kubana matumizi yasiyo ya lazima ili kuwapa unafuu Watanzania, yenyewe inaleta muswada wa kuzigawa fedha za Watanzania kwa kikundi kidogo cha watu ambacho hata hivyo kimekuwa kikifaidi mema ya Nchi kwa muda mrefu kabisa.

Mungu mwenye enzi, nguvu na uweza wa ajabu aingilie kati suala hili. Tunaodhani wangekuwa msaada kwa Wananchi, hao ndo wanakuwa GENGE la majizi na mafisadi.

Wabunge nao wakiamua tu, wanajiongezea posho na marupurupu ya kila aina.

Allah Akbar.
Andika vizuri kwamba sio sawa kutoa mafao Kwa wenzao wa Viongozi
 
FB_IMG_1698813136753.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom