Bunge Live larudi. Kuoneshwa kuanzia Aprili 5, 2022 katika mkutano wa saba wa Bunge la Bajeti

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Vikao vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania vitaanza kurushwa live. Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dodoma, Katibu wa Bunge. Ndg. Nenelwa Mwihambi.

Nenelwa amesema baada ya maboresho ya Studio ya Bunge na Kamati ya Uongozi ya Bunge kuridhia vikao vya Bunge vitaanza kurushwa live kuanzia kesho tarehe 05 Aprili 2022 wakati Mkutano wa Saba wa Bunge mahsusi kwa ajili ya kupitisha Bajeti ya Serikali utakapoanza Bungeni Jijini Dodoma.

Januari mwaka 2016, waziri wa habari wa wakati huo, Nape Nnauye alitoa tangazo bungeni la kusitisha matangazo ya Bunge ya moja kwa moja akitoa sababu ya kupanda kwa gharama kwenye shirika la utangazi la Taifa(TBC) zilizofikia bilioni 4.2 kwa mwaka.

Nape alisema TBC ilikuwa ikigharamia matangazo ya Bunge kwa kutumia vyanzo vyake vya mapato kama matangazo madogo ya kibiashara. TBC katika kupunguza gharama na kubana matumizi ikaona busara kurusha baadhi ya matangazo live na mengine kurekodiwa kisha kurushwa kwenye kipindi maalum usiku ambayo ingewapa pia fursa watanzania walio wengi kwani mchana huwa wana kazi za kiofisi au ujenzi wa Taifa.

PIA, Soma=>TBC1 yasitisha kuonesha baadhi ya Mikutano ya Bunge moja kwa moja (Bunge LIVE)

 
Katibu wa Bungea la Tanzania, Nenelwa Mwihambi, amesema Kamati ya Uongozi ya Bunge imeridhia vikao vya Bunge vitakavyoanza kesho Jumanne vitaanza kurushwa live. Maboresho ya Studio ya Bunge yamekwisha.
Hii nchi ina unafiki sana, na hili atasingiziwa JPM kwamba ndo alizuia, kumbe waliozuia wapo humohumo ndo wananafikia sasa!!
 
Nani ataangalia bunge la Chama kimoja ?
 
Kilio chetu ni Katiba Mpya na hamtaki kukisikia.
yaani nyie hamnaga hoja za maana zinazowahusu wananchi wa hali ya nchini mnachojali ni siasa ambazo wengi haziwasaidii sana bei ya vitu kupanda siyo agenda yenu maisha bora kwa mtanzania siyo agenda yenu mnacho haha nacho ni katiba mpya ambayo haileti unafuu wa maisha kwa mtanzania zaidi ya uchiu wenu wa madaraka tu
 
Nani ana haja ya kuangalia bunge la hovyo, la kusifia na kumpongeza rais
 
Bunge au vikao vya Ccm??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…