Leo tarehe 16 Juni 2020, Rais Magufuli analivunja bunge kwa ajili ya kufanya matayarisho ya uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu, ambapo uchaguzi wa rais na wabunge utafanyika kwa wakati mmoja.
Bunge la 11 lilifunguliwa na Rais Magufuli Novemba 20, 2015 baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Tutawaletea kile kinachojiri kutoka bungeni.
FUATILIA:
UPDATES:
Marais Wastaafu, Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu Dr Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Mstaafu Dr Gharib Bilal wakiwa Bungeni mjini Dodoma wakisubiri kusikia hotuba ya kulivunja Bunge Leo kutoka kwa kwa Rais Dk John Magufuli.
View attachment 1480357
09:24am - Makamu wa Rais na Rais wa Zanzibar wameshafika katika Ukumbi wa Bunge na pia wapo Viongozi wa zamani
09:36 Rais Magufuli awasili kwenye viwanja vya Bunge, akaribishwa kwa Wimbo wa Taifa na kukagua Gwaride Maalum
09:49 Rais Magufuli aingia Bungeni kusaini kitabu cha wageni
10: 00 Rais Magufuli aingia katika ukumbi wa Bunge
10: 10 Spika wa Bunge asema Miswada 60 imepitishwa kuwa sheria katika Bunge la 11
Katika Mkutano huu umeanza kwa kufunguliwa na Spika wa Bunge ambaye ameeleza mafanikio ya Bunge la 11 kwa ufupi.
Aidha, Spika Ndugai ameeleza kuwa toka Novemba mwaka 2015 Rais Magufuli alipolifungua Bunge hilo na kulipa mamlaka ya kuanza kazi kama ilivyo haki Kikatiba Bunge hilo l;imefanikiwa kufanya kazi mbalimbali.
Katika hili Spika Ndugai ameelaza baadhi ya kazi zilizotekelezwa na Bunge hili ambzo ni pamoja na kupitisha jumla ya miswada 60 ambayo yote imepeta kibali kwa Mh. Rais na kuwa Sheria za Nchi, Maadhimio yaliyopitishwa na bunge yalikuwa 38, Maswali yaliyoulizwa na kujibiwa na Serikali jumla yake ni 3376 na Maswali ysliyoulizwa kwa Waziri Mkuu yalikuwa 172.
10: 13 Spika amkaribisha Rais kuhutubia Bunge
10:14 Rais aanza kulihutubia Bunge
Rais alitaka Bunge kusimama kuwakubuka wabunge na waliptangulia mbele za haki.
Ashukuru uwepo wa marais na viongozi wastaafu wakiwemo Lowassa na Sumaye na kusema
“Kwa wakati nikizindua Bunge hili nilieleza mipango mingi na ninashukuru tumeweza kuitekeleza”
“Katika kipindi cha miaka 5 iliyopita tumetimiza wajibu wetu kwa kiasi kikubwa”
“Watangulizi wangu waliweka misingi imara iliyowezesha kufikia mafanikio tuliyopata kwa miaka 5 iliyopita…ushauri wao umenisaidi kwa kiasi kikubwa”
“Tanzania imeendelea kuwa kisiwa cha Amani na mipaka yetu imeendelea kuwa salama. Kama tunakumbuka, tulikuwa na wimbi la uhalifu wa kutumia silaha huko Kibiti lakini tulifanikiwa kudhibiti”
"Ripoti ya Global Peace Index ya mwaka 2020, imeonyesha Tanzania ni ya kwanza kwa Afrika Mashariki na ya 7 kwa nchi zilizo chini ya Jangwa la Sahara kwa kuwa na amani na utulivu"
"Serikali ilizidisha mapambano dhidi ya rushwa, uhujumu uchumi na ufisadi. Wakati nazindua Bunge hili Novemba 20 2015, niliahidi kuanzisha Mahakama ya Mafisadi. Hadi sasa jumla ya mashauri 407 yamefunguliwa, 385 yamesikilizwa"
Tumetaifisha Mashamba 23, Viwanja 298, Kampuni 3, Maghala 69 vilevile mali zilizowekewa zuio zikisubiria taratibu mbalimbali za utaifishaji
Nitumia fursa hii kuipengeza mamlaka ya kupamabana na dawa za kulevya kwa kufanikisha kudhibiti. Katika kipindi cha Miaka mitano Jumla ya tani 97.99 za bangi, tani 85.84 mirungi, Kilo 567.96 heroin, 23.383 za cocaine zimekamatwa, Pamoja na watuhumiwa 37,104
Mwezi December 2019 TRA ilikusanya trilioni 1.987 kiwango ambacho ni cha juu zaidi kuwahi kukusanywa katika historia ya nchi yetu
Mapato ya ndani ya halmashauri yamekuwa kutoka 402.66 bilioni 2015/6 hadi bilioni 661 mwaka wa fedha wa 2019
Tumepanua wigo wa upatikanaji wa huduma za Elimu, Afya na Maji. Tumetoa elimu bila malipo; tumeweza kuongeza madawati kutoka zaidi ya milioni 3 hadi zaidi ya milioni 8. Tumeongeza Mikopo ya Elimu ya Juu kutoka Bilioni 348.7 hadi Bilioni 45
Tumekarabati shule Kongwe za Sekondari 73 kati ya 89. Tumejenga mabweni 253 na maabara 227. Tumetoa vifaa vya maabara 2,956 na tumepunguza uhaba wa madawati ambapo yameongezeka kutoka 3,245,311 mwaka 2015 hadi 8,095,207. Ni sawa na ongezeko la 200%
Tulianza kutoa elimu bila malipo kwa elimu ya msingi na sekondari na hadi Februari 2020, tuikuwa tumetumia Trilioni 1.01 kugharamia - Tumeongeza shule za msingi kutoka 16,899 mwaka 2015 hadi 17,804 mwaka huu. Shule za Sekondari kutoka 4,708 hadi 5,330
Kwa upande wa sekta ya afya tumeongeza vituo vya kutolea huduma. Hospitali za wilaya 71 na hospitali za mikoa 10. Tumejenga hospitali za rufaa za kanda 3. Zaidi ya hapo tumeajiri watumishi wapya zaidi ya 1,000
Tumefanikiwa kusomesha madaktari Bingwa 301 ambao wameongeza huduma ktk magonjwa ya moyo, figo, sikio. Vifo vya watoto wachanga chini ya siku 28 vimepungua kutoka 25 hadi 7 kwa vizazi 1,000. Wagonjwa kutoka nje ya nchi wameanza kuja husasani wa moyo
Katika kipindi cha Awamu ya 5, tumefanikiwa kufufua shirika la simu (TTCL) ambalo lilikuwa limekufa
Tumekamilisha ujenzi wa barabara za kiwango cha lami za kiasi cha kilometa 3,500. Tumeanza kujenga flyovers na interchange kwa kuanzia Dar ili kupunguza msongamano
Nchi sasa ina takriban Kilomita 13,000 za barabara za lami. Kilomita 2,000 zinaendela kujengwa - Madaraja 13 yamekamilika. Katika awamu hii hakuna mkoa ambao haukupatiwa fedha za kujenga barabara kwa kiwango cha lami > Ahadi yetu ni kuhakikisha tunaiunganisha mikoa kwa barabara za lami na inaendelea kutekelezwa kwa kiwango kikubwa. Natumai Waziri ataendelea kusimamia.
Barabara kutoka Mpanda - Kigoma - Nyakanazi zinaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami na mashahidi ni wananchi kwani wanawaona wakandarasi katika maeneo hayo
Tunakamilisha ujenzi wa Reli ya kisasa SGR awamu ya kwanza kutoka Dar hadi Morogoro. Fedha zote za ujenzi wa SGR ni pesa za Serikali 100%
Tumeboresha usafiri wa maji kwenye maziwa yetu makuu. Tumekarabati meli 5 katika Ziwa Victoria; tunaendelea kujenga meli ya MV Mwanza (Hapa Kazi Tu). Tumekarabati meli ya Mafuta ktk Ziwa Tanganyika na MV Liemba inaendelea kukarahatiwa
Kwa upande wa Nyasa tumejenga meli ya kubeba abiria 200 na mizigo tani 200. Tuna mpango wa kujenga meli mpya ya kutoa huduma kati ya mkoa wa Mtwara na nchi ya Comoro ili mizigo yetu iende moja kwa moja bila kupita nchi nyingine.
Kwa upande wa Nyasa tumejenga meli ya kubeba abiria 200 na mizigo tani 200. Tuna mpango wa kujenga meli mpya ya kutoa huduma kati ya mkoa wa Mtwara na nchi ya Comoro ili mizigo yetu iende moja kwa moja bila kupita nchi nyingine.
Tumefufua ATCL kwa kununua ndege mpya 11 na ambapo 8 zimefika na nyingine zinatengenezwa - Faida nyingine ya ndege tumeiona katika kipindi hiki cha Corona ambapo Watanzania mbalimbali waliokwama ikiwemo India tumewarejesha.
Tumeboresha upatikanaji wa nishati ya umeme. Ujenzi wa Mradi wa Julius Nyerere Hydropower Station unaendelea ingawa ulipigiwa kelele sana. Pesa zote za ujenzi ni za Watanzania. Umetumia Tsh. 6.5 trilion na unaweza kuzalisha 2,115 MegaWatts
Idadi ya watumiaji wa umeme (energy access) imeongezeka kutoka 35% hadi 85%. Tumepunguza tatizo la kukatikakatika kwa umeme. Tangu tumeingia madarakani, nchi yetu haijawahi kuingia gizani
Tumeokoa Bilioni 719 kwa mwaka kwa kuzima mitambo ya IPTL na Simbion na kusaidia TANESCO kuanza kujiendesha yenyewe
Tumeboresha usikivu wa simu kutoka 79% mwaka 2015 hadi 94% 2019 > Idadi ya watumiaji wa simu za mkononi na watumiaji wa data imeongezeka, hii imechangiwa na kupungua kwa gharama za kupiga simu kwa dakika 1 kutoka Tsh. 267 mwaka 2015 hadi Tsh. 40 tu
Katika viwanda, tumejenga viwanda vipya 8,477 vikiwemo Viwanda vikubwa 201, vya Kati 460, Vidogo 3,406 na vidogo sana ni 4,410 - Hii imeongeza idadi ya viwanda nchini kutoka 52,633 kwa mwaka 2015 hadi viwanda 61,110 katika mwaka 2020
0% ya Pato la taifa inatoka kwenye Kilimo na tunategemea sekta hiyo kwa ajili ya chakula kwa 100%. Tumeongeza mtaji ktk Benki ya maendeleo ya kilimo. Tumeongeza upatikanaji wa pembejeo na zana za kilimo ikiwemo mbegu bora na matrekta.
Kwenye uvuvi, sangara kwenye ziwa Victoria wameongezeka kutoka tani 417,936 mwaka 2016 hadi tani 816,964 mwaka 2020 - Urefu wa sangara umeongezeka kutoka wastani wa Sentimita 16 hadi sentimita 25.2 na hivyo samaki wetu kuhitajika katika soko la Ulaya
Uzalishaji wa mazao ya chakula umeongezeka kutoka tani 15,528,820 kwa mwaka 2015 hadi 16,891,974 mwaka 2018/19. Mahitaji ya chakula kwa mwaka ni chini ya tani milioni 14. Uzalishaji mazao ya Biashara umeongezeka kutoka tani 796,502 hadi tani 1,144,163.1
Tumeongeza uzalishaji wa miche ya mazao ya kimkakati. Tumejenga na kukarabati skimu za umwagiliaji na vihenge vya kuhifadhi mazao. Tumefufua masoko ya mazao, tumetafuta masoko na tumeimarisha vyama vya ushirika.
Tumeongeza maeneo ya ufugaji kutoka hekta milioni 1.4 mwaka 2015 hadi milioni 5 mwaka 2020. Hii imesaidia sana kupunguza migogoro kati ya wakulima na wafugaji. Tumejenga mabwawa mapya 104 na tumeongeza idadi ya ng'ombe waliohamilishwa kutoka 1,005 hadi 514,700
Kwa lengo la kukuza uchumi tumeboresha mazingira ya biashara ikiwemo kutumia BluePrint. Tumefanya marekebisho ya sheria mbalimbali na kupunguza urasimu ktk kutoa vibali na kufuta tozo zenye kero 173 ambapo tozo 114 zinahusu sekta ya kilimo na uvuvi
Kutokana na hatua hizo biashara yetu nje imeongeza kutoka trilioni 11.5 2014/15 hadi kufikia trilioni 16.6 2018/19 > Jambo la kufurahisha zaidi ni Tanzania imekuwa na urari chanya wa mauzo ya bidhaa kwenye masoko ya Afrika Mashariki na SADC
Kwa upande wa masoko ya EAC kutoka 2015 hadi 2018 Tanzania imekuwa na urari chanya wa mauzo ya bidhaa kwa wastani wa dola milioni 288.04. Kuhusu uwekezaji, kituo chetu kimesajili miradi mipya 1,307 yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 14.607
Kwa mujibu wa taarifa za hali Uchumi kwa mwaka 2018, shughuli za sanaa na burudani ziliongoza kwa ukuaji kwa mwaka 2018, ilikua kwa 13.7% - Mwaka 2019 ilishika nafasi ya 3 kwa ukuaji wa 11.2%. Hongereni Wasanii wetu wa Bongo Fleva, Filamu, na Michezo
Kwenye Sekta ya Madini mageuzi makubwa yamefanyika ikiwemo kuanzishwa Wizara mahsusi ya madini, kudhibiti utoroshaji na usafirishaji wa madini ghafi nje ya nchi, kuanzisha masoko ya madini kwenye kila mkoa na kuongeza ushiriki wa wafanyabishara wadogo
Mwezi Julai 2017 tulipitisha sheria ya kulinda Rasilimali za Taifa ikiwemo madini. Nashukuru Spika na Wabunge kwa kupitisha sheria hii muhimu sana kwa taifa letu. Kwa hakika mmeingia kwenye vitabu vya historia ya nchi yetu na vizazi vitawakumbuka
Kupitishwa kwa sheria hiyo kumewezesha kwa mara ya kwanza Watanzania kumiliki rasilimali zao kwa nguvu za kisheria. Na sheria hiyo pia ndiyo imefanikisha kuanzishwa kwa kampuni ya Twiga Mineral Co. ambayo Serikali inamiliki hisa 16% na Barrick 84%
Kwa mujibu wa taarifa za hali Uchumi kwa mwaka 2018, shughuli za sanaa na burudani ziliongoza kwa ukuaji kwa mwaka 2018, ilikua kwa 13.7% - Mwaka 2019 ilishika nafasi ya 3 kwa ukuaji wa 11.2%. Hongereni Wasanii wetu wa Bongo Fleva, Filamu, na Michezo
Kwenye Sekta ya Madini mageuzi makubwa yamefanyika ikiwemo kuanzishwa Wizara mahsusi ya madini, kudhibiti utoroshaji na usafirishaji wa madini ghafi nje ya nchi, kuanzisha masoko ya madini kwenye kila mkoa na kuongeza ushiriki wa wafanyabishara wadogo
Mwezi Julai 2017 tulipitisha sheria ya kulinda Rasilimali za Taifa ikiwemo madini. Nashukuru Spika na Wabunge kwa kupitisha sheria hii muhimu sana kwa taifa letu. Kwa hakika mmeingia kwenye vitabu vya historia ya nchi yetu na vizazi vitawakumbuka
Kupitishwa kwa sheria hiyo kumewezesha kwa mara ya kwanza Watanzania kumiliki rasilimali zao kwa nguvu za kisheria. Na sheria hiyo pia ndiyo imefanikisha kuanzishwa kwa kampuni ya Twiga Mineral Co. ambayo Serikali inamiliki hisa 16% na Barrick 84%
Kadhalika imesaidia kutolewa kwa malipo ya fidia ya dola milioni 100 kati ya dola million 300 ambazo kampuni ya Barrick ilikubali kutulipa. Nakushukuru Mh. Spika kwa kuunda Kamati maalum ya Bunge ya kuchunguza utoroshaji wa madini ya Tanzanite
Kamati hiyo ilitoa ushauri wa kujenga ukuta wa Km 25 katika mgodi wa Mererani na sisi Serikali ambao ni wasikivu tuliujenga kwa haraka sana. Sekta ya Madini imeanza kukua kwa kasi ambapo 2019 iliongoza kwa ukuaji kwa 17.7% ikifuatiwa na ujenzi 14.1%
Mapato yatokanayo na madini nayo yameongezeka. Kwenye mwaka 2018/2019 zilikusanywa bilioni 346 kutoka bilioni 194 mwaka 2016/17. Kwenye mwaka huu 2019/20 tunatarajia kukusanya bilioni 470 ambapo mwezi Aprili licha ya tumekusanya bilioni 58.
Haijawahi kutokea kabisa, kiwango cha juu tulichowahi kukusanya kwa mwezi kilikuwa bilioni 43. Haya yametokana na kupitishwa kwa sheria mliyopitia ninyi Wabunge. Mafanikio mengine ni kutolewa kwa leseni 221 za uchenjuaji madini na 4 za uyeyushaji.
Kupitia jitihada zilizofanyika ikiwemo utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo ambayo nisingependa kuitaja hapa tumetengeneza ajira 6,032,299 - Kati ya hizo, ajira 1,975,723 zimezalisha na sekta rasmi na 4,056,576 zimezalishwa na sekta zisizo rasmi.
Rais atangaza kufunguliwa kwa shule kufuatia kufungwa baada ya mlipuko wa Corona.
Amesema hali ya Corona nchini inaendelea vizuri na imepungua sana. Amesema shughuli nyingine zote kama kufunga ndoa nazo ziendelee na maisha lazima yarudi kama ilivyokuwa awali.
Hapa duniani si rahisi kufanya japo lisikutane na vikwazo au changamoto na sisi ktk miaka mitano tumekutana na changamoto mbalimbali - Mojawapo ni kuibuka kwa janga hili la Corona. Napenda kulishukuru Bunge hili kwa kupitisha azimio la kunipongeza.
Kabla ya kuhitimisha hotuba yangu napenda nirudie kuwashukuru Watanzania wote wa makundi yote wakiwemo wakulima, wafugaji, wavuvi na wafanyabiashara kwa kuiunga Serikali katika kudumisha amani na kulipa kodi.
Namshukuru sana Makamu wa Rais, mwanamama shupavu na jasiri, Mama Samia S. Hassan kwa kunisaidia sana majukumu. Namshukuru Rais wa Zanzibar, Dkt Ali M. Shein kwa ushauri na ushirikiano alionipa. Namshukuru na kumpongeza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
Nawashukuru Mawaziri na Manaibu Waziri. Wamefanya kazi usiku na mchana kwa upendo mkubwa sana. Walinivumilia sana. Hawakuwa na uhakika na uwaziri wao lakini wamechapa kazi sana. Nawashukuru Makatibu, Naibu, Wakuu wa mikoa, wilaya na watumishi wote wa Serikali
Natambua Dkt. Shein anamaliza muhula wake kwa mujibu wa Katiba. Hivyo, nampongeza kwa utumishi uliotukuka akiwa Makamu wa Rais kwa miaka 8 na Rais kwa miaka 10. Mh. Rais Dkt. Shein kazi umeifanya. Umeweka historia na namna yake ktk utumishi wa umma.
Naishukuru CCM kwa kusimamia vizuri Serikali na kuhakikisha ilani ya uchaguzi ya 2015-20 inatekelezwa vizuri. Usimamizi mzuri uliofanywa na CCM umethibitisha maneno ya Baba wa Taifa, "Chama legelege huzaa Serikali legelege" and the vice versa is true
Navishukuru vyama vingine vya siasa ambavyo vilitoa ushirikiano kwa Serikali kwa miaka 5 > Wapo baadhi ya viongozi ambao licha ya tofauti zetu za kiitikadi walikuwa pamoja na Serikali wakati wote. Inatakiwa kuwa hivyo, sisi sote ni wamoja na tunajenga taifa moja
Niwashukuru Wabunge wa vyama vingine, japo walikuwepo baadhi wenyewe kila jambo walikuwa wakipinga lakini nao nawashukuru. Naamini wakati ujao watakuwa wamejifunza kwamba kupingapinga kila kitu sio vizuri.
Kwa namna ya pekee nampongeza sana mwanamama jasiri, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu kwa uvumilivu wake - Nataka kusema kwa dhati nilimtesa sana, nilikuwa nampigia simu mara nyingi muda mwingine saa 8 usiku - Naomba aniombee msamaha sana kwa Mume wake
Pongezi hizi zinastahili watanzania na Bunge hili maana pamoja na Corona kutawala Bunge hili liliendelea na vikao kama kawaida - Bunge liliendelea kuwatumikia Watanzania ingawa nafahamu wapo wachache waliokimbia na sijui kama wamerejea.
Kukimbia halikuwa jambo sahihi kwasababu matatizo au changamoto hazikimbiwi - Kukimbia changamoto ni ishara ya udhaifu, uoga na kutokujiamini - Siku zote njia sahihi ni kukabiliana na matatizo ndio maana tuliamua kuikabili Corona tukimtanguliza Mungu
Namshukuru Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Kamati zake zote kwa namna walivyosimamia hili. Ninayosema ni kwa dhati sana - Napenda pia kuvishukuru Vyombo vya Ulinzi na viongozi wenzangu ndani ya Serikali na Watanzania kwa namna tulivyosimama pamoja
Nimekuja hapa kutimiza lengo lililopo la kikatiba hasa la kuruhusu kuanza kwa mchakato wa Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 2020. Nyote mnafahamu Uchaguzi ni zoezi muhimu katika kukuza Demokrasia katika nchi yoyote
Mbali na kuwapa wananchi fursa ya kuwachagua viongozi wanaowataka, inatoa pia fursa kwa viongozi kujua endapo wanaaminiwa na wananchi. Katika hilo natambua baadhi yenu hapa mmeshaonesha nia ya kuwania tena na wapo waliotangaza kutowania tena
Nawatakiwa maisha mema wale waliotangaza kustaafu na ninawatakia kila la kheri wale wanaowania tena > Naamini wengi wenu hasa wale wenye kuvaa nguo za kijani watarejea lakini kwa ambao hawatabahatika kurejea tunawashukuru kwa mchango wao kwenye Bunge hili
Navisihi vyama vya siasa na wanasiasa kujiandaa vizuri katika uchaguzi huu. Navihimiza vyama kutoa fursa za kutosha kwa wanawake, vijana na walemavu. Nawasihi wagombea kuepuka matusi na vurugu. Nchi hii ni yetu sote, tujiepushe na shetani wa matusi
Tumtangulize Mungu kwenye kampeni. Matusi na kejeli hayajengi, sisi sote ni wamoja. Tukabishane kwa hoja na kushindanisha ilani zetu. Yeyote atakayetaka kuleta vurugu namtahadharisha, Serikali iko macho. Uchaguzi haumaanishi Serikali imeenda kulala
Baada ya kusema yote sasa natamka kuwa Bunge hili linavunjwa rasmi na tarehe itatangazwa rasmi kwenye gazeti la Serikali. Niwatakie mafanikio mema na nataka niwahakikishie zile tisheti zenu zilianza kuingia saa 8 za usiku kwa kila mmoja