Bungeni: Mbunge wa CHADEMA amtimua mpangaji wake ambaye ni Askari Polisi, adai haoni maana ya kushirikiana nae, Waziri Lugola amtisha

Bungeni: Mbunge wa CHADEMA amtimua mpangaji wake ambaye ni Askari Polisi, adai haoni maana ya kushirikiana nae, Waziri Lugola amtisha

Haitoshi kuwafukuza mapolisi hayo matendaji lazima yatimuliwe yakalale CCM.
Halafu huyo mkata viuno si awapangishe nyumbani kwake?
 
Hii midada ya viti maalumu chadema sio wa kulaumu sana maana sera kichwani hamna na jinsi ya upatikanaji wao huwa ni aibu kuelezea humu.
 
Mpaka hivi sasa bado natafuta Mantiki ya Kumfukuza Askari Nyumbani Kwako ambako umempangisha kwa sababu tu za Kisiasa na Hasira. Askari Kufukuzwa kuna Uhusiano gani za matatizo ya Kiuchaguzi au ya Kisiasa? Hivi ukija kuwa Mzee na ukasikia nawe Mwanao ambaye labda amekuwa Askari nae akifanyiwa hivi kama Mama utajisikiaje?

Leo hii unaposema kuwa umemfukuza Askari Kwako kwakuwa huoni umuhimu wake hivi na Wao Askari ambao kwa bahati nzuri Sisi Wananchi tunawahitaji sana kwa Ulinzi na Usalama wa Mali zetu Siku ikitokea nawe ukapatwa na matatizo wakikususia na yakakukuta makubwa utamlaumu nani?

Kama unajinasibu kuwa Wewe ni mpenda Demokrasia na unapambania Haki za Watu unapomfukuza Askari Kwako ulikompangisha uliangalia pia na upande wake wa Pili wa Familia yake ambayo ni kama vile umeinyanyasa? Kwa Kitendo hiki unategemea Kweli upate hata Mwanachama Mmoja ndani ya hiyo Familia ambaye pengine Kura yake hiyo moja na nyinginezo zingeweza Kuitoa CCM Madarakani kama unavyotaka?

Ni kweli Askari wanaweza wakawa na Changamoto zao ila Kumfukuza Nyumbani Kwako halafu unakuja Kujisifia na Kuutangazia Umma wa Watanzania ni Uthibitisho wa aina ya Roho mbaya yenye Ukatili mwingi uliyonayo. CCM haitotolewa Madarakani kwa Kuwachukia Mapolisi bali itatolewa kwa Sera, Mipango na Mikakati thabiti.

Na kilichoniuma na kunisikitisha zaidi ni kwamba haya Maamuzi yamefanywa na Mwanamama ambaye nilikuwa naamini kuwa ndiyo Jinsia ambayo Kiasili imetawaliwa na Huruma kuliko hata Wanaume. Na hakuna Kitu kibaya kama Kutengeneza Bifu na Mapolisi na leo anaweza akafurahi ila natabiri mapema kuna Hatari naiona inaelekea kwa aliyemfukuza Askari Nyumbani Kwake.

Tujifunze Kutenganisha Hasira na Utu.
Kampangishe wewe huyo Askari.
 
Najaribu kutafakari ni sheria ipi itamtia hatiani huyo mbunge
 
Mama nakuonea huruma sana. Je umejiandaa vyema kupambana na Hilo kundi? Wanaweza kukutengenezea fitina makusudi sijui utakuja Tena hadharani kuwalalamikia hawafanyi kazi.
 
Ovyo kweli kweli kiongozi ni kioo cha jamii hivi sasa mtu kama huyu anafundisha nini wananchi.

Hii ni ‘hate crime’ na hatua za kisheria lazima zichukue mkondo wake.
 
Hata mimi ningemuondoa ila nisingemtangaza bungeni

Ishu sio kumuondoa polisi, ishu ni kuutarifu umma juu ya mpasuko uliopo hapa nchini. Upendo, udugu na amani ya moyoni haipo tena. Hili ndilo jambo alilotaka kuelezea umma. Ujumbe umefika
 
Najaribu kutafakari ni sheria ipi itamtia hatiani huyo mbunge
TRA kama alikuwa kodi halipi na TRA ikishamtia hatiani haruhisiwi.kugombea Tena milele udiwani ,ubunge ,uraisi au uongozi wa serikali ya mtaa sababu kukwepq Kodi ni moja us kosa ambalo ukidakwa haruhusiwi kugombea

Pia Kuna huo.mkataba wa kupanga nyumba Kama kakiuka imekula kwake
Tatu kosa la kimaadili.la kibunge ,bunge lenyewe Lina uwezo wa kula naye sahani moja
 
Ovyo kweli kweli kiongozi ni kioo cha jamii hivi sasa mtu kama huyu anafundisha nini wananchi.

Hii ni ‘hate crime’ na hatua za kisheria lazima zichukue mkondo wake.
Hiyo ni hate speech .Nchi za wenzetu saa hii angekuwa na pingu
 
Mama nakuonea huruma sana. Je umejiandaa vyema kupambana na Hilo kundi? Wanaweza kukutengenezea fitina makusudi sijui utakuja Tena hadharani kuwalalamikia hawafanyi kazi.
Tena aelezwe wazi traffic polisi wanasubiria magari yake barabarani hakuna atakayekuwa tayari kumpa ushirikiano Kama yeye asivyotaka ushirikiano
 
Ndo kusema ile kinga ya wabunge wakiwa mjengoni nayo ndo haina maana tena?
Aliyemsema na kumtimua hayuko bungeni kamnyanyasa mtu nje ya bunge hakuna Cha Kinga hapo.Huwezi niibia ukakimbilia bungeni ukasema uliniibia halafu ujifanye una Kinga ya bunge.Kitendo kiovu ulichofanya nje ya bunge lazima uwajibike
 
Aliyemsema na kumtimua hayuko bungeni kamnyanyasa mtu nje ya bunge hakuna Cha Kinga hapo.Huwezi niibia ukakimbilia bungeni ukasema uliniibia halafu ujifanye una Kinga ya bunge.Kitendo kiovu ulichofanya nje ya bunge lazima uwajibike

Uovu ni upi?
Kumkataa mpangaji au kutangaza bungeni nimemkataa mpangaji?
 
Baada ya kauli ya Mbunge Sophia Mwakagenda (CHADEMA) aliyosema amemuondoa mpangaji ambaye ni Polisi kwenye nyumba yake kwa sababu haoni haja ya kushirikiana nae.

Waziri Kangi Lugola amemuagiza IGP Simon Sirro kumchukulia hatua Mbunge huyo na wengine wanaotoa kauli zenye viashiria vya uvunjifu wa amani.

hata mimi ningemtimuwa au hata kumwitia mwizi apewe kichapo maana ndio wanao wapa kiburi hao mashetani wa kijani.
 
Huyo hawajui polisi wa nchi hii ni heri angekaa tu kimya kwa kuwa tayari ameshamtimua na nafsi yake imesuuzika badala ya kuendekeza huo upayukaji.

Atalengeshwa kwa wahuni wampore halafu wasikilizie ataenda ku-report wapi!

Akijipeleka huko atakutana na yaliyomkuta Magdalena Sakaya miaka ile.
 
Back
Top Bottom