Buriani Mzee Ruksa: Ni Deng Xiaoping Wetu wa Mageuzi ya Kiuchumi, Demokrasia, Haki za Binadamu na Uhuru wa Habari. Asante kwa Ruksa Zako, Pumzika!

Nairobi palionekana kama Ulaya, mtu akitoka Nairobi anarudi na sabuni, dawa za kupigia mswaki na bidhaa nyingine za basic needs.

Mwinyi aliondoa habari hizo.
Aisee!

Kula ilikuwa changamto, sukari changamoto. Nguo za viraka. Haikutosha, hata sabuni na dawa ya kupigia mswaki?

Kama kitu kama sabuni na dawa ya kupigia mswaki vilionekana anasa nakosa cha kusema kiukweli! Mlipitia kipindi kigumu sana.
 
Kiranga

Mama yangu aliniambia baba yako alifuatwa na usalama wa taifa nyumbani na wakaondoka naye kisa anaonekana tu ana maendeleo fulani.

Na hicho kipindi mzee alitaka kununua gari, mama anasema na laiti angelikuwa ameshalinunua halafu usalama ndiyo wamemdaka hali ingekuwa mbaya kwa baba yenu.

Kwa sababu kuna ndugu yetu mmoja alifilisiwa na alikamatwa kabisa na aliwekwa ndani. Walichimbia hela nyengine chini ya ardhi ili wasionekane wana visenti angalau.
 
Mwalimu ana pande mbili za sarafu nzuri na mbaya.

Ubaya ni kwamba propaganda imepigwa zaidi katika upande mzuri ila mbaya umefichwa hivyo ni rahisi zaidi makosa ya Mwalimu kurejewa na walio mfuatia kwa sababu Watanzania wengi hawafahamu upande mbaya wa Mwalimu.

Ogopa sana mtu ambaye itikadi imemtawala kupindukia ni ngumu kuamini jambo fulani ana kosea au hayupo sahihi, siku zote yeye ata amini ana fanyiwa hujuma au hajaeleweka wakati sivyo.

Wakomunisti na wajamaa wengi wa mwanzo ukomunisti na ujamaa uliwalevya kupindukia na hili pia naliona kwa mataifa ya kibepari hawa watu huwa hawaoni wala hawasikii na wala huwa hawaamini kwamba nje ya mawazo na mfumo wao kuna mambo mengi bora unaweza kujifunza na kuyachukua.

Mwalimu ujamaa ulimlevya na kumpofusha mazima akawa haoni wala hasikii wala aamini kuwa kuna mazuri na mabaya ndani ya ujamaa na pia kuna mazuri na mabaya nje ya ujamaa.
 
Aisee!

Kula ilikuwa changamto, sukari changamoto. Nguo za viraka. Haikutosha, hata sabuni na dawa ya kupigia mswaki?

Kama kitu kama sabuni na dawa ya kupigia mswaki vilionekana anasa nakosa cha kusema kiukweli! Mlipitia kipindi kigumu sana.

Watu walikuwa wanatengeneza sabuni zao zinaitwa maganji, wanachanganya magadi, majivu, mafuta na vitu gani sijui, wanapata sabuni za kutengeneza wenyewe.

Wengine walikuwa wanafua kwa kutumia majani ya mpapai.

Chakula kilikuwa haba tulikula bulga, bulga ni kama uji fulani wa ngano kama nakumbuka vizuri. Kulikuwa hakuna mchele wala unga.

Ronald Reagan akatufanyia mpango tukapewa unga wa msaada kutoka Marekani, unga wenyewe wa njano, watu wakawa wanasema huu unga wa njano ni mahindi ya kula wanyama, ni unga wa mahindi ya kula farasi na ng'ombe, si ya kula watu.

Lakini kwa sababu tulikuwa na njaa, tukala tu ule ugali wa njano. Tuliuita ugali wa Yanga kwa sababu ya rangi ya njano.

Nimekumbuka miaka ile mpaka machozi yamenitoka.

Mwinyi aliondoa dhiki ile.
 
Kama tunataka kujenga taifa bora tuna hitaji kuwa katikati ya ujamaa na ubepari kamwe tusiwe wajamaa wala wabepari.

Kuna madhara makubwa sana sisi kulevya na itikadi za kibepari au kijamaa.

Tunahitaji kujua yapi ni bora katika ubepari na yapi ni mabaya pia tunapaswa kujua yapi ni bora katika ujamaa na yapi ni mabaya.

Case study yetu ya mwanzo inapaswa kuwa China na Singapore.
 
Bila shaka mwinyi alipata shida Sana kuongoza huku nyerere akiwa pembeni akifanya interference ya Mara kwa Mara.

Namkumbuka hata sera za benjamini mkapa nyerere alikuwa anazikosoa waziwazi
 
Ww jamaa uminitoa tongo za macho
 
Kwa kweli niwape pole sana ya dhati kabisa kutokea moyoni.

Kuna kitabu chochote naweza kuyapata haya Bw. Kiranga? Au hata pdf?

Kwa sababu kwa kizazi chetu yakizungumzwa haya yanaoenakana kama hadithi.

Kuna kipindi nilikuwa naongea na wenzangu walishangaa na wengine kubisha kwamba Tanzania kwa zaidi ya mara mbili imenusurika kupinduliwa kijeshi. Ajabu watu hawajui kama kuna kitu kama hiki! Na siliongelei kisiasa yani niliongela kihistoria.
 
Ewaaa! Naungana na wewe kwenye hili! Lakini napata tabu kwa nchi yetu kwa maana safu ya uongozi bado sijamuona aliye na maono ya namna hii!
 
My always wish ni kumuona Hussein Mwinyi akishika Uraisi wa Jamhuri. I see him kufanya makubwa sana ila sasa ndio sijui kama itakuw hivyo. Nadhani Magufuli alikuwa anamuandaa kuwa Mrithi wake baada yake.
 
Kuna kipindi alipwaya mpaka Nyerere aliamua kumsaidia.

Alishindwa kabisa kucontrol bunge , serikali ilikua inaanguka.

Anyways nitamkumbuka kwa kuuza Loliondo kwa waarabu.

Familia yake ina bahati sana ya Uongozi ila ni vilaza.
sio alishindwa ku control Bunge, aliridhia Demokrasia ichukue nafasi yake

Wabunge wengi kupitia G55 walipiga kura kuridhia kurejeshwa serikali ya Tanganyika ambayo hadi leo inaliliwa, Mwinyi akajadiliana na PM wake Malecela na Katibu Mkuu wa Chama Horace Kolimba wakaona bora waridhie kilio cha wengi

kuna Machawa wakamjulisha Mwl Nyerere ndio mbio mbio akaomba iitishwe Kikao cha Wabunge cha CCM walati huo Wabunge wote ni CCM akaomba awahutubie kwa kuwa kule Bungeni hatambuliki kisheria

ndio akawaibukia akatibua mpango akawaambia mkitaka Serikali 3 kwanza mjitoe CCM kwa kuwa sio sera ya Chama , wakati huo ukijitoa CCM kama vile umejitoa uhai na mchezo ukaishia hapo wa Serikali 3


Unaemwita Kilaza hakuwa na lugha za kukera wala kufedhehesha ila naamini kama kwny familia yako wangepewa fursa ya kuchagua Baba kati yako na Yeye kwa kura za siri angepita kwa kura za ushindi wa Tsunami
 
My always wish ni kumuona Hussein Mwinyi akishika Uraisi wa Jamhuri. I see him kufanya makubwa sana ila sasa ndio sijui kama itakuw hivyo. Nadhani Magufuli alikuwa anamuandaa kuwa Mrithi wake baada yake.
JPM alimtaka ndio awe Samia wake na aliwahi kulisema hadharan JPM mwenyewe, sema yule Mzee akiekuwa na jina la Mgombea kwny mfuko wa koti pia alikuwa na jina la Makamu wa Rais na akafanikiwa kumshawishi Mgombea urais kubadiki jina la Makamu wake kwa mujibu wa hayati Mwamba mwenyewe
 
Azimio la Zanzibar lilileta mageuzi,yakiwemo ya upatikanaji wa bidhaa muhimu,ambazo kipindi Cha bwana haambiliki zilikuwa kama anasa.

RIP Baba wa demokrasia,licha kwamba kule Kigoma kwenye Kura za ndio idadi ya Kura ilizidi idadi ya wapiga kura.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…