Bus kuwa VIP linatakiwa kuwaje maana kuna moja nimepanda hakuna tofauti kubwa na la kawaida

Bus kuwa VIP linatakiwa kuwaje maana kuna moja nimepanda hakuna tofauti kubwa na la kawaida

Bus halikuwepo wakati nakata tiketi , lilikuja baadae muda wa kusafiri ulipokaribia
Ungeanzisha timbwili yani umeshapanda unaanza kuwauliza choo kiko wapi..?
kama hakipo unawaambia unamwaga inya kuanzia mwisho wa bus mpk kwa dereva!.
unang'aka haswa kama hakuna na AC unawaambia unavunja dirisha!.
yani unahakikisha hukamatiki hivyo vi juice na biscuit unakataa unapiga zogo unataka ugali nyama!..🤣
 
[/QUOTE]
Na mie leo najiunga na wa CHAI hii

Sababu haujataja Jina la kampuni na ukisafiri kutoka wapi kwenda wapi.

Unajua JF ipoje? 😉
Wanajijua wenye hizo huduma . Wajirekebisha wataje huduma za kweli na sio kuongezea za uongo ambazo hazipo.
 
Kuna bus moja huko kanda ya ziwa sitalitaja ila sipandi tena kutokana na kutuona abiria ni wajinga.

Baada ya kukuta kampuni niliyoizoea kujaa nikaenda kampuni nyingine nikaambiwa imebaki VIP na nikatajiwa nauli ambapo inaongezeka elfu 15 kutoka ile ya kawaida. Nikawauliza kuna huduma gani za ziada wakaniambia kuna choo, Azam TV, msosi na Internet basi nikaona hii nzuri, nikalipa .

Kufika muda wa kusafiri kuingia ndani nikaona seat ziko tu kama za kawaida, baada ya muda tukaunganishwa Wi-Fi speed ya kobe, hakuna cha choo wala nini na tukawa tunasimama kwenye kuchimba dawa mavyoo ya nje . Wakazidi kutuona abiria ni wajinga kwa kutugawia biskuti za sh.mia na pipi mbili.

Kwa nini msiwe wakweli yaani biskuti za sh mia, pipi na WiFi ndio mnaita bus VIP na kuongeza nauli?

Kuongezeka kwa elfu 15 sio kubwa sana lakini kwa nini muongope kwa kutaja huduma za uongo?

Abiria sio wajinga.
Kwa nchi hii ya watawala Wagagagigikoko na wachumiatumbo. basi likishaandikwa "VIP BUS" ubavuni mwake, tayari linakuwa VIP mkuu. Nchi ya kipuuzi sana hii.
 
Na mie leo najiunga na wa CHAI hii

Sababu haujataja Jina la kampuni na ukisafiri kutoka wapi kwenda wapi.

Unajua JF ipoje? 😉
!!
 

Attachments

  • IMG-20241210-WA0006.jpg
    IMG-20241210-WA0006.jpg
    45.9 KB · Views: 1
Nilikata VIP ya Kigoma-Saratoga ili nishukie Tabora.
Wakati wa kusubiria gari nikaingia KB Lounge Mbezi nikagonga vyombo nikijua sitapata shida ya kuchimba dawa. Nilijuta na siipandi tena.

Juzi nimetoka Masasi na VIP-Mining Nice. Hakuna cha internet wala refreshments. Choo kipo ila abiria wamejaa hadi wamekaa mlango wa chooni. Nimewadharau sana wenye gari.
Jana nimepanda BM VIP ya Arusha ya saa tatu. Hawa nawaa maua yao. Kila kitu walichoandika kipo. Huduma nzuri sana.
Kesho nitapanda Nacharo ya Tanga. Nitaleta mrejesho.
Angalizo. Sipo hapa kuaribu biashara ya mtu ili hii iwe iama changamoto na ifanyiwe kazi
 
VIP

2 x 2

Huduma:
Bites
Vinywaji
AC
TV
Jamaa alitaka agonge ugali nyama mboga saba km kwa shilole.
Huwa najikazasana kutokula njiani.
Siku tunaenda Dom enzi za BM Chalinze pale pembeni tulifakamia ile mibata maji, huku tuliambiwa ni kuku kienyeji, mpaja km mguu wa mtoto, nikala chipsi yai kuku kienyeji hata sikumbuki km lilikua la mbuni lile.
Ila hataakuumwa tumbo, msosi ndo ulikua hadithi.
 
Bus halikuwepo wakati nakata tiketi , lilikuja baadae muda wa kusafiri ulipokaribia
Mkuu pole sana,mi nilikua mbio nirudi dar na mishe zangu niko mbeya kwanza tukuyu huko.
Nafika mbeya stand nikakamatishwa Abood ya kutoka tunduma sa tatu inaingia na siti nikapewa.
Ile kuingia ndani hamna siti.
Nilikalia kiroba cha mchele mpk bongo.
na tulipita pale moro saa nzima+ garage kwao.
Nilijuta.
Sijawai kupanda tena mabus.
 
Back
Top Bottom