Busara kidogo inahitajika katika hili

Busara kidogo inahitajika katika hili

Baba mwenyewe alisema ulikuwa ni ujana na anajutia, hivyo it was never My Ma's fault..!
Kumbe...basi asikusumbue. Nachukia wanaume wa hivi alijua kabisa ana mtoto mahali kilichomkimbiza ni kipi na kilichomrudisha ni kipi?? apambane na hali yake. Msamehe ndio lakini hakuna namna nafasi aliyoipoteza muda wote huo aje aipate kirahis rahis tu.Nina dada yangu nae ana kesi kama hii mwanae yupo chuo sasa et baba mtu ndio anakuja alafu sasa anamtafuta mtoto kwa kuibia ibia.

Wanaume wanaokimbia watoto jaman mkikimbia msirudi mnaumiza sana watoto wenu hata kama mama mtu ndio alikosea mtoto/watoto wanahusika vipi? Yaani mtu unakua na sababu gani hasa usilee mwanao?? Mambo yakiwa magumu huko ndio mnarud ooh mwanangu nisamehe hii kitu inaudhi mno.
 
Aiseh nilimpoteza mtoto wangy wa kiume kisa mama yake alituchanganya watatu nikakataa nikisema tupo watatu nitaaminije ni mimi!!leo dogo ana miaka tisa kapewa ubin Mwingine!!!hayo ndio maisha aiseh!!!heshimu baba yako tu!!ili upate haki yako!!!
 
Aiseh nilimpoteza mtoto wangy wa kiume kisa mama yake alituchanganya watatu nikakataa nikisema tupo watatu nitaaminije ni mimi!!leo dogo ana miaka tisa kapewa ubin Mwingine!!!hayo ndio maisha aiseh!!!heshimu baba yako tu!!ili upate haki yako!!!
Dah!...pole aisee japo wewe pia ni chanzo kwa kukataa kuwajibika.......na wewe umekubali kabisa dogo apotee kirahisi hivyo ?.....chukua hatua mapema.

Fight for your 'blood' man
 
Hii mada waisome sperm donor wote waliopo humu jf, inasikitisha sana mtu kujifanya anakupenda sasa ilhali alikukana na kukutelekeza tangu mimba🤤🤤, baba mlezi kamsitiri mama yako na wewe pasipo kusita, mthamini na ongea nae juu ya hilo mpe heshima na nafasi yake maana anastahili hilo na abarikiwe sana

Anajipendekeza baada ya kukosa mtoto wa kike tu
 
Ni ngumu kidogo kutoa ushauri wa jumla pasipo kujua haswa kisa kilichofanya baba yako wa kibaiolojia kutengana na mama yako na hatimaye 'kutelekeza' ujauzito/mtoto...

Baba anayekulea ambaye kiuhalisia ndiyo baba yako ana nafasi kubwa ya kushirikishwa hali halisi kuliko kuendelea kumficha...
 
Binti,
Kama ni haki yako ya kumjua baba mama yako ameshakupatia.Kama ni upendo wa kibaba,Umeupata kwa baba yako mlezi.Baba yako mzazi hana haki yoyote ya kujaribu au kukulazimisha umpe nafasi katika maisha yako kama wewe hauko tayari.Maadam ameshakupa contact zake na umeshampa nafasi ya kukuona nafikiri inatosha.

Wewe kwa sasa ni mtu mzima.Unayo haki ya kuamua kiwango cha muingiliano unachohitaji kutoka kwake na kumwambia stop iwapo unahisi anakukera au kukubughudhi.Heshima aliyopewa na mama yako pamoja na baba yako wa kufikia ya kuweka jina lake kwako inatosha kwa sasa.Mengine yanategemea hisia zako na uamuzi wako.

Zingatia kwamba kila uamuzi utaofanya una weza ama kukupa furaha au kukupa huzuni na ushauri wangu kwako ni huu.Usikubali akufanye mateka wa kihisia bali tanguliza furaha yako kwanza.Mpe heshima yake na nafasi yake kwa kadiri ya nafsi yako.

Nakutakie kila la heri na unao moyo mzuri sana kuweza kusamehe.
 
Huwa nawaambiaga Sana wanaume wenzangu kuhusu matukio kama haya, unaishi na mtu mpaka unampa ujauzito then either unamfukuza au unamtafutia sababu uachane nae...later unakuja kudai haki yako uliyokuwa huna mpango nayo na kuona si kitu.

Carleen Una haki kusema chochote juu ya huyo Biological father mpaka ulipo sasa, don't hurt that Baba Mlezi hata iweje muombe Mungu akujaalie katika hilo, najua you make wise decision on this.
 
Hii mada waisome sperm donor wote waliopo humu jf, inasikitisha sana mtu kujifanya anakupenda sasa ilhali alikukana na kukutelekeza tangu mimba[emoji1786][emoji1786], baba mlezi kamsitiri mama yako na wewe pasipo kusita, mthamini na ongea nae juu ya hilo mpe heshima na nafasi yake maana anastahili hilo na abarikiwe sana

Anajipendekeza baada ya kukosa mtoto wa kike tu
Kabisaa baada ya kukosa mtoto wa kike ndo kakumbuka kuna sehemu alipanda mbegu ila sio kwa mapenzi maana angekua na binti kwa mkewe nako asingekumbukwa kabisaa!!huyo amerudi tu purposely ila hana mapenzi

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
Hiyo ndio dhima kuu ya ubongo, kufikiria. Ndio maana nimesema fikra zangu hizi zinaweza kua si sahihi kutokana humu tu watu wa historia,tamaduni na mila tofauti kutokea maeneo tofauti ndio maana wengine humu ni rahisi kumwambia mzazi wake kua "Nakupenda Baba" jambo ambalo Kwangu au kwetu ni kitu cha ajabu sana ajili ya mila na tamaduni za kwetu.

But kwa zile mila Common za muafrika sidhani kama ni vyema kumuita baba yako kua "This man,Huyu Mwanaume, yule Mwanaume". Mbele ya watu wazima utaonekana una utovu wa nidhamu na heshima.

Je wewe binafsi unaweza au unaona kwako sawa ukiwa mbele ya marafiki au ndugu zako unamu-Address mama yako kwamba "Yule mwanamke, huyu mwanamke, That woman, n so so so...? Unaona kwako hilo ni sawa kulifanya.??

Lakini pia bado naweza kua sipo sahihi kwa hili nililoeleza hapa, so mtakaonielewa vibaya mnisamehe.. Being Right is relative...I might be right because I fed your Ego and I might be wrong coz ain't fed your Ego

Btw ningependa mjadala wa kuhusu Kumuita mzazi huyu au yle uishie hapa maana sio lengo kuu la mtoa mada. Tujikite sasa katika mada!
Just like you said, "nidhamu" could be relative too. Kile ambacho kwako hakifai, kwa mwingine kinaweza kuwa ni cha kawaida kabisa. Na pia, mila zako sio lazima zifanane na mila za mleta mada.

Jifunze kuchukulia poa mambo mengine. Too much imagination inakupunguzia uwezo wa kupuuza mambo ambayo yanastahili kupuuzwa. Nakubaliana na wewe, hili liishie hapa.

I rest my case!
 
Hey guys..!
Huwa napenda kuja hapa na uchiinga' wa hapa na pale, ila naombeni Leo niwe serious kidogo, hii ni issue ya kweli kabisa ya maisha yangu..!!

Sijui kwanini nataka kushare kama ni ushauri nitaupokea, ila kama kuna la kujifunza mtu aweza lichukua pia likamsaidia..

Mimi ni kati ya watu wachache waliobahatika kulelewa na 'baba mlezi' kwa ule upendo ambao lije jua, ije mvua I am 100% sure siwezi upata popote pale, I hate to call it Him baba mlezi, ila huo ndiyo ukhalisia..!!

Na bahati nzuri nilipewa bahati ya kujua ukweli nikiwa mdogo, Baba hakupenda hili jambo lakini kama ningekuja kujua sasa nadhani ningedata kabisa kujua Huyu Mwanaume anayenipenda kuliko chochote kuwa He is not My Real Father...!

Nakumbuka nikiwa mdogo kabisa, nilikuwa natazama photo album ya Mama ya zamani, Nika point picha mojawapo ya mkaka ambaye alikuwa ananifanania sana sana, nikamuambia 'Mama, bila shaka huyu ndiye Fulani' (hapa nilimtaja baba mzazi kwa jina lake)..

Mama alicheka akauliza umejuaje.?? Nikamuambia nimeona tu tunavyofanana, akaniambia ni kweli ni yeye..! Hilo likaishia hapo na ni sura ya ujanani kabisa, hivyo nikabaki na wazo tu kuwa Me and that man we real look alike, maisha yakaendelea hivyo..!!

Baba mlezi ndiye Baba ambaye nimekua nikijua huyu ndiye dunia yangu, He is so proud ov Me na hivi tuko na lighting color wote, hivyo nikitembea naye natambulishwa almost everywhere like she is my first daughter, na watu wakiona hiyo rangi angavu wanajua kabisa ndiyo ni kweli na husema kabisa mmefanana hasa..!

Katika wanaume I can admit wameni spoil ni this Man, na ukubwa wangu huu imagine that man bado ananiita 'my happiness' 'totoo', 'my everything'..! ana watoto wengine wa kike kwa kiume lakini the whole family inajua kipenzi cha Baba ni nani..!

Katika watu naogopa kuumiza maishani mwangu ni huyu mwanaume, Imagine, alinambia 'binti yangu, usije kuniaibisha', hayo maneno huwa natembea nayo chochote nachofanya nawaza nisije m-dissapoint yule mwanaume, japo ni muda mrefu ila huwa yanaishi moyoni mwangu daima..!!

Baada ya yote hayo, nikiwa binti mkubwa kabisa mwaka Jana mwishoni, napokea simu ya mtu anajitambulisha kuwa Mimi ni mwanae, kwanza I was shocked sababu najua baba yangu nilishapiga naye story mchana, mpaka aliponitajia jina ndiyo nikaelewa..!!

Nikajikuta nalia machozi, sijui ni kwanini nililia vile, anyways, nilizungumza naye kwa nidhamu na utulivu mkubwa nikawa namsikiliza, akaniambia anaomba sana samahani kwa kuniacha miaka yote hiyo, na alikuwa akinitafuta sana bila mafanikio ila hivi sasa ndiyo kafanikiwa kunipata..!

Anaomba sana samahani, kwa kuniacha, kutokuwa pale kwa ajili yangu na pia kwa kumuumiza Mama, na kinachomuuma hakufanikiwa kupata mtoto wa kike huko alikokwenda Mimi ndiyo bintiye wa pekee, kapata watoto wa kiume woote..!!

Huruma ni kweli alikuwa anatia me nikamuambia Mimi sina tatizi lolote na wewe, ila kwa jinsi ulivyomuumiza yule Mama sijui ni kitu gani utafanya mpaka tu akuelewe na kukusamehe maneno uliyomtamkia na jinsi ulivyomuacha Mimi nikiwa tumboni na nikuambie tu ukweli hajawahi kusahau..!

Akawa anataka tuonane japo anione tu, nikamuambia ongea kwanza na Mama, ndiyo naweza nikakuona japo kwa sehemu tulizokuwepo tulikuwa jirani kiasi ila sikuweza tu kwenda kumuona bila ruhusa, na pia sikutaka kabisa kumshirikisha hili Baba nilihisi tu kama atajiskia vibaya, sijui ni kwanini nilifikiri hivyo, kama nilivyosema mwanzo sikutaka nimfanye ajiskie vibaya kwa ajili yangu kwa namna yoyote ile,

Mpaka Leo sikuwahi muambia Baba yangu chochote na yeye hakuwahi niuliza chochote japo Mama alishamuambia kuwa baba mzazi kanitafuta, Nadhani anasubiri kama nitamuambia chochote ila Mimi siwezi muambia kitu kiukweli..!!

Japo kiukweli niliwahi enda kumuona baba mzazi, I was just curious kumuona na ni kitu nilikuwa natamani sana, I can admit he is very charming person kama Mimi anapenda kufurahi mno pia.! Ila nimekaa naye na kuongea naye it's like talking to a stranger, ana maisha yake tu anajiweza lakini Ile furaha hupata nikiwa na Baba yangu mlezi it was never there.! tulifanikiwa kuongea mengi na kupiga story na akawa anajutia sana lakini on my side nilimuambia ni sawa tu nilishamsamehe..!

Tatizo linaanzia wapi, sahii analalamika anataka ule ukaribu na bond ya Baba na Mwanae, anahisi namtenga, anahisi sijamsamehe, lakini sina tatizo naye ni kuwa almost every day the only Man that came into my mind ni Baba Mlezi, the only Man niwe na siku nzuri ama mbaya lazima nimuambie na ni lazima anitafute ama nimtafute, na ukubwa huu lakini ni kawaida kuona 'Imethibitishwa' zake kwa simu yangu, huwa ananitreat bado kama vile Mimi ni kabinti kadogo, mpaka niliwahi muambia nikija olewa nitahakikisha naolewa na mwanaume anayenipenda at least nusu ya upendo wako, akacheka akaniambia tu Muombe Mungu sana na ulivyo tu huyo mwanaume kazi atakuwa nayo, nikamuambia wewe ndiyo umeniharibu lakini, akatabasamu akajibu, ipo siku nitakuja kuelewa..!

Kabla nisahau, Mama hataki ushirika naye kabisa anasema Baba anayemtambua yeye ni Baba Mlezi tu, japo yeye pia alimuambia ashamsamehe hivyo asijali aendelee na maisha yake kwa amani, Naomba nikazie hapa My Ma hajawahi nizuia Mimi kuwasiliana wala kumuona Baba sababu ni yeye ndiye alipambana nitumie jina la Baba mzazi alisema hataki nipoteze haki ya kumjua baba mzazi pia, na alikuwa anaimani sana kuwa ipo siku baba yako mzazi atarudi tu na utamuona, na kweli yakatimia..!!

tukirudi huku kwa baba mzazi, analalamika mpaka namuonea huruma lakini sipati ile feeling ya ubaba juu yake what am I supposed to do.? Na huwa ananitumia pesa za hapa na pale ananiambia vocha namuambia tu ahsante, hata ile kuita 'Baba' naona ugumu, me huwa naishi zangu kama vile he doesn't exist, nikikumbuka ni mara moja namjulia hali mpaka nikumbuke tena siyo Leo, most of the time yeye ndiye hunitafuta na malalamiko juu anahisi nafanya kusudi kumkomoa lakini hapana, moyo wangu unaishi huku kwingine toka utotoni..! anataka nikawajue ndugu zake lakini I don't feel like I do belong there, kawapa ndugu zake namba wananitafuta lakini siwafurahii all the same pia, na kumsamehe nishamsamehe lakini the bond ain't there, na malalamiko yake yananiumiza lakini nimeshindwa yafanyia kazi..!!

Nashindwa hata nimfanye nini maskiini..!!
Mwambie baba mlezi ukweli and make sure unawakutanisha

Na unamweka baba mzazi wkenye nafasi yake na kumweleza sifa zote ulizotuambia hapa za baba mlezi

Hiyo itampa mlezi heshima na amani na mzazi atajua nafasi yake

Hakuna kitu kibaya Kwa mwamaume kama akijua unamficha vitu

Na hasa kama amesacrifice maisha yake Kwa ajili yako

Btw…. Mbona hii story inajurudia sana humu jf?

Mbona kama hii issue ilishakua solved na member mmoja veteran humu?
 
Nitazungumza na Baba this Pasaka, nitaona kile atasema..!
Unajua huyo baba mlezi anaweza akaacha uamue lakini ikamuumiza sana.
Natamani huyu baba mzazi abaki tu kama mgeni mualikwa ktk maisha yako yote!
Ili uwe na amani pia,kwanza ht hao ndugu zako na mkewe kwa baba mzazi sidhani kama wanaupendo nawe maana hapo ukute wanawaza umefata Materials things!achana nao
Situation yako ilimtokea mdogo wangu kwa mamdogo 34yrs back ,mbaba alikataaga mimba!
Yule mzee anajiweza sanaa kimaisha ni mkulima mkubwa anauza mpk nje huko ila hanaga mtoto mpk Leo.
Mamdogo alifariki mda mrefu sana dogo anatumia jina La huyo mzee na la mwisho ni ukoo wa kina mama...
Sasa miaka ya hivi karibuni akaanza kumtafuta mwanawe aliyemkataaga kipindi hiko ,akaanza kumtafuta mamdogo mwingine mpenda hela akampanga vzr wakamfata binti kumueleza kua baba ake Mara sijui vipi na vipi kabla hajamaliza akasema "stop mamamdogo,sina baba ktk hii dunia,na staki kwa namna yoyote mumtaje huyo mtu nimekubali sina baba na ntaishi bila baba,kwa maisha niliyopitia ya kuishi bila baba mzazi Leo sihitaji mwingine baada ya kupata shida zote aseme Mimi ni mwanawe na akamuambia odo ukitaka tukosane ongelea huyo mzee,simjui na sihitaji kumjua mpk naingia kaburini na sina deni kwa Mungu"
Vikamshuka mpenda hela yule na yule mzee hata alipokuja na pesa zake Dogo amekaza wajomba wakasema maamuzi tunamuachia yeye aamue sisi hatuna usemi maana mama ake amefariki 1994 toka kipindi hajajitokeza na bad enough walikua wote mkoa hukoo baada ya mamdogo kufariki walienda kuzika kina mama wakarudi wakamuacha mtoto wakiamini baba ake atamfata kumbe alivyofata huku nyuma na baadhi ya watu akasema sio mwanangu simtaki,na enzi zile hakuna simu aliishi maisha ya kichokoraa km miezi miwili mama angu mzazi Mimi siku moja akasema ngoja niende nikaangalie dogo anaishije ,mkoa anauliza pale home anaambiwa hawajui alipo ikabidi aanze kumsaka kesho yake anamkuta maeneo ya stendi anaomba omba mama akamchukua wakaja nae Dar akasomeshwa na wajomba na sasa ana ajira yake na ameolewa na mume mzuri tu.
Sio story Carleen ni uhalisia upo ktk familia yetu kabisaa!

Kuna mwanaume waselfish Sana'a mwishowe wanaambulia majuto makubwa na wewe pia usiwe selfish acha baba mlezi afaidi matunda yake
Be wise in ur decision kuhusu hilo jambo

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
Unajua huyo baba mlezi anaweza akaacha uamue lakini ikamuumiza sana.
Natamani huyu baba mzazi abaki tu kama mgeni mualikwa ktk maisha yako yote!
Ili uwe na amani pia,kwanza ht hao ndugu zako na mkewe kwa baba mzazi sidhani kama wanaupendo nawe maana hapo ukute wanawaza umefata Materials things!achana nao
Situation yako ilimtokea mdogo wangu kwa mamdogo 34yrs back ,mbaba alikataaga mimba!
Yule mzee anajiweza sanaa kimaisha ni mkulima mkubwa anauza mpk nje huko ila hanaga mtoto mpk Leo.
Mamdogo alifariki mda mrefu sana dogo anatumia jina La huyo mzee na la mwisho ni ukoo wa kina mama...
Sasa miaka ya hivi karibuni akaanza kumtafuta mwanawe aliyemkataaga kipindi hiko ,akaanza kumtafuta mamdogo mwingine mpenda hela akampanga vzr wakamfata binti kumueleza kua baba ake Mara sijui vipi na vipi kabla hajamaliza akasema "stop mamamdogo,sina baba ktk hii dunia,na staki kwa namna yoyote mumtaje huyo mtu nimekubali sina baba na ntaishi bila baba,kwa maisha niliyopitia ya kuishi bila baba mzazi Leo sihitaji mwingine baada ya kupata shida zote aseme Mimi ni mwanawe na akamuambia odo ukitaka tukosane ongelea huyo mzee,simjui na sihitaji kumjua mpk naingia kaburini na sina deni kwa Mungu"
Vikamshuka mpenda hela yule na yule mzee hata alipokuja na pesa zake Dogo amekaza wajomba wakasema maamuzi tunamuachia yeye aamue sisi hatuna usemi maana mama ake amefariki 1994 toka kipindi hajajitokeza na bad enough walikua wote mkoa hukoo baada ya mamdogo kufariki walienda kuzika kina mama wakarudi wakamuacha mtoto wakiamini baba ake atamfata kumbe alivyofata huku nyuma na baadhi ya watu akasema sio mwanangu simtaki,na enzi zile hakuna simu aliishi maisha ya kichokoraa km miezi miwili mama angu mzazi Mimi siku moja akasema ngoja niende nikaangalie dogo anaishije ,mkoa anauliza pale home anaambiwa hawajui alipo ikabidi aanze kumsaka kesho yake anamkuta maeneo ya stendi anaomba omba mama akamchukua wakaja nae Dar akasomeshwa na wajomba na sasa ana ajira yake na ameolewa na mume mzuri tu.
Sio story Carleen ni uhalisia upo ktk familia yetu kabisaa!

Kuna mwanaume waslefish Sana'a mwishowe wanaambulia majuto makubwa.
Be wise in ur decision kuhusu hilo jambo

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
Thank you!

Well said

Yaani huyo mzee anawez hata kujuta na kupata msongo

But he won’t say because he doesn’t want to hurt the girl
 
Pole sana , ukirudi kwenye psychology ni dhahiri kuwa mtoto wa kike upendwa sana na baba na pia binti umpenda baba sana , sasa hapa ndiyo tatizo lilipoanzia ulishaathirika na upendo wa baba mlezi since ukiwa mdogo na hivyo ni vigumu huo upendo kuugeuza.

Sasa si shida ila jua kumtenga baba yako mlezi itakuchukua mda sana na inahitaji njia za kisaikolojia sasa usifike huko kaa na baba mzazi , mueleze scenario nzima ila mjulishe haumtengi ila mko wote , baada ya hapo jitaidi kuongeza mawasiliano naye kupunguza lawama .

Kwa hivyo nahisi itakuwa Sawa na maisha yataendele .after all he is your real father

Pole sana ni ugonjwa wa saikolojia ila tiba yake ni hiyo.
 
Hii dunia inazunguka kwa kasi sana, nampa pole baba mzazi.

Off the topic:

Nina kaka yangu yeye alikua na mwanamke akaambiwa ana mimba ya huyo mwanamke jamaa kapambana akalea mimba hadi kujifungua. Picha ikaanza mtoto wa kiume kazaliwa mweupe pee na jamaa ni mweusi tii na binti ni mweusi tii.

Sasa rumours zikaanza mtoto si wajamaa, jamaa akaanza upelelezi mwanamke akakaza kuwa mtoto ni wake. Baada ya mwaka mtoto anazidi kubadilika, weupe unakolea hana sura ya mama wala ya baba. Ndipo jamaa akakomaa kua wakapime DNA mwanamke akaruka maili mia.

Jamaa akasema kama umegoma kupima DNA ya mtoto mie sitatoa na wala sitajihangaisha na gharama za mtoto. Kumbuka Hayo walifikiana wakiwa dawati la jinsia.

NB. Huyo bro ana familia yake na huyo mwanamke alikua ni mchepuko wanafanya wote kazi. Jamaa likawa funzo kwake hapigipigi hovyo tena saivi.
 
Back
Top Bottom