Bwawa la Nyerere ni uamuzi mgumu na wa kijasiri uliofanywa na Magufuli!

Bwawa la Nyerere ni uamuzi mgumu na wa kijasiri uliofanywa na Magufuli!

Baada ya Kabendera kupiga kwenye Mshono naona PUSH GANG wanakuja na Legacy ya NZIRANKENDE.
 
Elimu ni jambo lililo wazi, sio ugonjwa useme ni siri kati ya mgonjwa na daktari wake.

sasa kama jambo liko wazi huyu bwana ako alikuwa anahoji ili apate chakula au???

unakurupuka huko umeshiba makande unaanza na vyeti vya rais!!!
 
Dar es Salaam kulikuwa na shida gani hadi watu wahamie Dodoma??
Hakuna project iliyohitaji maamuzi magumu na uthubutu wa ajabu kama project ya serikali kuhamia Dodoma. Inashangaza nchi kubwa kama hii viongozi wa aina ya Magufuli wanatokea nadra sana.
 
Huyu hapa jpm alikuwa kuna kitu ananuza
IMG_20221015_003741.jpg
 
sasa kama jambo liko wazi huyu bwana ako alikuwa anahoji ili apate chakula au???

unakurupuka huko umeshiba makande unaanza na vyeti vya rais!!!

Rais ni nani, au kwako ni Mungu nini?
 
Ok JPM alikuwa anathubutu, lakini alikuwa hajali ipasavyo ushauri wa kitaalamu au kuwa na subira utafiti kamili utangulie ujenzi wa mradi.
WWF wana msemo " the true cost of a dam never shows up on a balance sheet". Aswan Dam huko Misri kmf uliongeza eneo la umwagiliaji maji kwa wakulima, lakini mimea iliyopandwa ilikuwa hafifu kwa kukosa virutubisho vilivyonaswa bwawani. Matumizi ya mbolea yakaongeza sana gharama. Huko kwenye delta ya mto Nile uzalishaji wa kamba (prawns) ulitoweka- $7 bilioni kwa mwaka zikapotea.
Nini tunajifunza toka mgao wa umeme uliopo sasa hivi wakati tuna mabwawa ya Kidatu, Kihansi, Pangani,Mtera nk?
Mjomba Magu alikuwa na nia nzuri lakini wakati ulikuwa umeishapita wa kujenga Bwawa hilo.
Mwalimu Nyerere aliambiwa na maswaiba wake wa Nordic Countries kujenga hilo bwawa miaka ya 70,lakini Vita vya Kagera vikavuruga mapesa ya kulijenga.
Mjomba Magu kaja kujenga bwawa hilo tena kubwa kuliko makisio ya utawala wa Mwl Nyerere, miaka 40 baadae mazingira yamekuwa tofauti,tabia nchi,maji ya mto Rufiji sio kama enzi hizo kwa sababu vyanzo vya maji vimeharibiwa na shughuli za binadamu.
Pili,Sasa tuna gesi asilia nyingi tu,alitakiwa atumie gesi asilia kama nishati namba mmoja,in a long run matumizi ya kuni yangepungua,na uoto wa asili kwenye mabonde yetu ugerudi.
Lakini walikata miti milioni 6 kupisha ujenzi wa bwawa hilo unategemea hiyo miti ilichukuwa miaka mingapi?
Kuna uwezekano wa huo mradi ukawa white elephant sababu ya kitu muhimu kimoja kikuu UPATIKANAJI WA MAJI YA KUTOSHA KUENDESHA TURBINE ZOTE KWA WAKATI WOTE.
 
Hakuna project iliyohitaji maamuzi magumu na uthubutu wa ajabu kama project ya serikali kuhamia Dodoma. Inashangaza nchi kubwa kama hii viongozi wa aina ya Magufuli wanatokea nadra sana.

Hatatokea tena mbona
 
Unaweza ukafanya uamzi mgumu na ukawa wa kipuuzi vilevile..

Kwanza angekuwepo Mwendazake hilo Bwawa lingemalisika 2040 maana hakuwa na pesa..

Baada ya mwaka na nusu ujenzi uko zaidi ya 70% kutoka 30% ya miaka 2 ya kujengwa na Mwendazake,zaidi ya mara 2.

Izo n chuki binafsi zako hakuna mrad ulochelwa enz za magu
 
Sina uwezo wa kujua uhakika wa hiyo "R.I.P". Mwenye mamlaka makubwa juu ya hilo anajuwa mwenyewe.

Ila nikubaliane na wewe, kuna maamuzi ambayo aliyafanya Magufuli, katika hali ya kawaida angestahili heshima zote zinazowezekana ndani ya nchi hii.
Binafsi nitaongezea na uamzi wa kwenda Dodoma, na mengine kadhaa wa kadhaa.

Lakini nisichojuwa kingine ni jinsi akili yake ilivyokuwa ikifanya kazi; kiasi kwamba hayo mazuri yakichanganywa na yale ya hovyo kabisa, mazuri yote yanaonekana yana uchafu mkubwa sana.

Una ushahidi wa hayo mabaya?
 
Mjomba Magu alikuwa na nia nzuri lakini wakati ulikuwa umeishapita wa kujenga Bwawa hilo.
Mwalimu Nyerere aliambiwa na maswaiba wake wa Nordic Countries kujenga hilo bwawa miaka ya 70,lakini Vita vya Kagera vikavuruga mapesa ya kulijenga.
Mjomba Magu kaja kujenga bwawa hilo tena kubwa kuliko makisio ya utawala wa Mwl Nyerere, miaka 40 baadae mazingira yamekuwa tofauti,tabia nchi,maji ya mto Rufiji sio kama enzi hizo kwa sababu vyanzo vya maji vimeharibiwa na shughuli za binadamu.
Pili,Sasa tuna gesi asilia nyingi tu,alitakiwa atumie gesi asilia kama nishati namba mmoja,in a long run matumizi ya kuni yangepungua,na uoto wa asili kwenye mabonde yetu ugerudi.
Lakini walikata miti milioni 6 kupisha ujenzi wa bwawa hilo unategemea hiyo miti ilichukuwa miaka mingapi?
Kuna uwezekano wa huo mradi ukawa white elephant sababu ya kitu muhimu kimoja kikuu UPATIKANAJI WA MAJI YA KUTOSHA KUENDESHA TURBINE ZOTE KWA WAKATI WOTE.
Mkuu heb acha kukaririshwa.
Heb google hapo uangalie haya mabwawa mawili uone yamejengwa mwaka gani
1. Three Gorges Dam - 22,500MW - China
2. TalHige Dam - 6,000MW - Etheopia

Hivi vijisababu vya tabia inchi vipo Tanzania tu au ndo Elimu ya kukariri?huko kwa wenzetu wanaojenga hawana hizi tabia inchi tunazohubiriwa kwetu hazipo au wao wapo Sayari nyingine?
One thing hizo nchi mbili hapo juu they have in common uchumi wao umekua ukikua kwa 7%+ for the last 10yrs...and to be one of them lazima uinge mawili matatu kutoka kwao...Cheap Electricity, cheap production cost.
Soon the world will go green with electical cars and the likes, tabia inchi zitarudi km tupo in 1920's...au ulitaka tusubiri grean revolutions ndo tukurupuke kujenga hilo Dam?
Visionary are people who sees tomorrow, and JPM was one of them...unfortunately kwa ulichoandika hapa i dont see km u r among them.
Ni kweli tabia inchi ipo bt not to that extent Next time ukisikia kitu kifanyie research kuthibitisha, then changanya na zako, sio unatirika na pumba kwakua tu kuna watu fulani fulani wamesema hivyo.
 
View attachment 2388796
View attachment 2388797

Tunaposema Hayati Magufuli alikuwa mtu na nusu hasa kwenye mambo yaliyohusu kuamliwa kijasiri bila kujali faida na hasara zake hakika John yake ilikuwa namba moja.

Mfano ni uamuzi wa kujenga hilo bwawa hapo juu ( Bwawa la Nyerere) ki-ukweli ili ujenzi wake uanze ilihitaji mtu jasiri na asiyeyumbishwa kama Magufuli. Kelele, vitisho, hujuma na hata usaliti vilimea kwa kasi lakini mwamba hakujali na alisimamia kile alichokiamini!

R.I.P JPM.
Majangili ya ufipa hayatakuelewa.
 
Una ushahidi wa hayo mabaya?
Dah!

Wewe utakuwa umetoka sayari nyingine, sijawahi hata kukusikia hata humu JF kabla ya leo.

Kwa hiyo kudai kwako kwa "ushahidi" kunaweza kutokana na ugeni wa kuwepo kwako hapa duniani, eneo la Tanzania.
Huko kwenu ulikotokea pengine kuwa na ushahidi ni tofauti na huku duniani.
Inakubidi ujitahidi kuishi maisha halisi ya hapa duniani na siyo hayo uliyozoea huko kwenu.
 
Back
Top Bottom