CAG aibua ufisadi TPA ya Deus Kakoko, Ni mbaya kuliko wa Kigwangalla

CAG aibua ufisadi TPA ya Deus Kakoko, Ni mbaya kuliko wa Kigwangalla

Au labda watafutwe warokole tu ndo wafanye kazi bandari
 
Acha ajiachie tu kila mtu na zamu yake
Awamu hii ya kwake
Nyie mngepewa nafasi msingepiga au?

Ova
 
Kwa wiki zima mitandao ya jamii imemshupalia Dr Hamis Kigwangalla kwa ufisadi wa kutumia Tsh bilioni 2.58 bila idhini ya Bunge. Pengine Kigwangalla yuko kwenye "spotlight" kwa vile siku zote ni mtu wa majibizano kwenye mtandao ya jamii.

Sasa kuna manunuzi ya Tsh bilioni 22.69 yaliyifanywa na TPA ya Deus Kakoko. Katika DHAMBI au makosa makubwa ya manunuzi yanayo mhusisha mnunuzi moja kwa moja na RUSHWA ni kununua kwa SINGLE SOURCE.

Tumpunzishe Dr Kigwangala, tujikite na huyu Deus Kakoko anayejinasibu kuwa ni "home port" na JPM na huwa ana nguvu kuliko mawaziri wa wizara ya mawasiliano. Kumbuka alishindana na Waziri Mbarawa, na Mbarawa akang'oka.
View attachment 1413440
Kumbe wizi wa kigwangala Na kakoko wakwanza zamani
 
Mwaka wa mwisho huu kila mmoja huangalia jinsi ya kupiga Kodi zetu.
Ukiona watu wanataka upinzani ufe huku mlinda Kodi zetu kama Assad akifurushwa uhitaji kujua jibu la nia.

Tofauti na awamu iliyopita tulinufaika wote na ufisadi awamu hii wanufaika wa chache na upiga haswaa.
We nae Assad assad assad! Huyo tulishamtema na nafasi yake imezibwa barabara na hatumuhitaji! Aende kwa mabwana zake mabeberu alikokuwa analitukanisha taifa letu!🤔!
 
We nae Assad assad assad! Huyo tulishamtema na nafasi yake imezibwa barabara na hatumuhitaji! Aende kwa mabwana zake mabeberu alikokuwa analitukanisha taifa letu![emoji848]!
Uongo kama huu ndio maana mnakufa vifo vya aibu!
 
Uongo kama huu ndio maana mnakufa vifo vya aibu!
Kuwa makini na unayosema, utakufa kwa aibu mwenyewe na jamaa yako sio mimi!
Ww Assad, huna nafasi kwenye serikali ya kizalendo inayoongozwa na rais wetu mpendwa SSH! Nenda kafanye kazi na mabeberu wako!
 
Kumbe wizi wa kigwangala Na kakoko wakwanza zamani
Deus Kakoko alisema yeye ni untouchable na kaiba sana. Hata Kigwangalla CAG alishasema ni MCHAFU Ila Magufuli kwa watu wake alikuwa anakaa kimya.
 
Kwa wiki zima mitandao ya jamii imemshupalia Dr Hamis Kigwangalla kwa ufisadi wa kutumia Tsh bilioni 2.58 bila idhini ya Bunge. Pengine Kigwangalla yuko kwenye "spotlight" kwa vile siku zote ni mtu wa majibizano kwenye mtandao ya jamii.

Sasa kuna manunuzi ya Tsh bilioni 22.69 yaliyifanywa na TPA ya Deus Kakoko. Katika DHAMBI au makosa makubwa ya manunuzi yanayo mhusisha mnunuzi moja kwa moja na RUSHWA ni kununua kwa SINGLE SOURCE.

Tumpunzishe Dr Kigwangala, tujikite na huyu Deus Kakoko anayejinasibu kuwa ni "home port" na JPM na huwa ana nguvu kuliko mawaziri wa wizara ya mawasiliano. Kumbuka alishindana na Waziri Mbarawa, na Mbarawa akang'oka.
View attachment 1413440
Sasa inakuaje bavicha wanasema leo ndio cag kawafivhua sababu jpm hayupo?
 
Wale timu JPM kaeni mkao wa kutapika mlivyokula kwa hila na majivuno. Mama kaanza kuonesha makali yake. Huyu Engineer Kakoko alikua rafiki mkubwa sana wa JPM tangu ujanani. Wakati JPM akiwa waziri wa ujenzi alimpigia pande Kakoko akawa Meneja TANROADS mkoa wa Arusha.

Baada ya JPM kuwa Rais, Kakoko akapandishwa ghafla hadi kuwa Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya bandari baada ya menejimenti ya bandari kufumuliwa. Hapa ndipo akaanza kuiendesha bandari kama familia yake. Akajilipa madeni mengi hewa, akatoa zabuni feki kwa makampuni ya ndugu zake, akaandaa semina na warsha hewa ili kupiga hela.

Mwaka 2017 idara ya zabuninya TPA ililalamika mbele ya Rais JPM kuwa Kakoko alichukua milioni 700 kwenye account ya procurement na kumwambia Meneja ugavi atafute namna ya kujustify matumizi ya hiyo hela. Lakini badala ya JPM kufanyia kazi madai hayo akasema bandari waache majungu. Baada ya muda kitengo cha procurement kikafumuliwa na wafanyakazi wakahamishiwa taasisi nyingine za serikali wakaajiriwa wapya.

Unaambiwa wafanyakazi wengi wa bandari wameacha kazi kwa sababu ya Kakoko. Alikua na majivuno (si unajua wahaya) na tambo nyingi akisema hakuna wa kumuondoa bandari. Amewahi kumlaza sero Meneja wa operation baada ya kumpa dokezo la 200 milioni asaini akakataa. Alipouliza za nini akaambiwa wewe saini ni order ya Kakoko. Alipokataa akalazwa central siku tatu.

Alipotoka akahojiwa na gazeti moja akaeleza kuwa amelala rumande kutokana na kukataa kusaini dokezo la Kakoko la 200M. Lakini badala ya Kakoko kuchukuliwa hatua, yule mama akaambiwa ajieleze kwa sababu amekiuka maadili ya utumishi wa umma kwa kuongea na media bila kibali cha mwajiri wake. Baadae akawa demoted akatolewa bandari akatupwa PSSSF huko Songwe.

Kakoko alikua type za kina Bashite na Sabaya. Watoto pendwa wa mzee ambao hata waue mtu hawawezi kufanywa kitu. Walifurahia kuenjoy maisha kupitia machozi na damu za watanzania. Sasa mama amemua kuanza nao. Hizi ni salamu kwa Sabaya na genge lake waliozoea kutesa na kuumiza watu lakini wakatumia jina la Rais kujilinda.

Hongera sana mama Samia kwa kuanza vizuri kusafisha nyumba yako. Tunajua kazi hii ni ngumu na utakumbana na vikwazo vingi lakini tunakuombea.
 
Kuwa makini na unayosema, utakufa kwa aibu mwenyewe na jamaa yako sio mimi!
Ww Assad, huna nafasi kwenye serikali ya kizalendo inayoongozwa na rais wetu mpendwa SSH! Nenda kafanye kazi na mabeberu wako!
Upendo wa kinafki huu unaousema , rais wenu mpendwa hayupo , ambae mlitaka atawale milele , mmeimba mitano Tena, aongezewe muda mpaka mkataka kuitisha maandamano wa kumuongezea mda leo hii ukamwite Mh. SSH mpendwa wenu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom