CAG ni Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali. Kazi ya UDHIBITI hajaifanya ndio maana kuna madudu kibao kwenye ripoti yake, atimuliwe

Assad
Alifanya kama unavyoshauri lakini
Wapumbavu walimpiga vita
 
Halafu arudishwe professor Musa Assad na mutueleze Til 1.5 zilitumika kufanya nini. Kila aina ya takataka unayo iwaza kichwani mwako nilazima uilete hapa?
 
Nchi ilianza kwenda vizuri na Wananchi tukaanza kuelewa maana ya CAG na kumuheshimu wakati wa Utou hata Assad tulikuwa tumeshaanza kustaarabika na kujua na kuona umuhimu wa CAG.

Wapori pori walipoingia madarakani hata heshima ya Majaji na Mahakama haipo tena HAKIM anawapiga faini Chadema million 370 kwa kesi ya kubambikizwa mauaji bila kumleta muuaji aibu ya karne nahaita sahaulika milele Agullina Rip
 
Kwa kuwa ameibua uozo sio, vipi kama angekuja na yale mapambio yetu.
 
Ndugayi ni LA....FA...sana
Ukiangalia na alivyogeuka 180°..farisayo sijui sadukayo wa kizazi kipya aisee!

Everyday is Saturday................................😎
 

Wewee kaa utulie usiingilie majukumu ya CAG, huyajui vizuri, tafuta mtu anaejua akuelekeze
 
ni umeamka asubuhi ukaandika pumba au bado unaota?

udhibiti unafanyika na serikal kuu yeye anatoa mapendekezo tu. kazi inabaki serikali kuu wafanyie kazi au lah.
Yeye anadhibiyi nini? hicho cheo cha udhibiti anadhibiti nini? kama kazi yake ni kukagua tu angeitwa Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali lakini anaitwa mdhibiti na mkaguzi.Yeye kakalia tu kukagua.Hiyo ya kudhibiti anamwachia nani na ripoti yake mbona hatoi anatoa ripoti tu ya ukaguzi tu?

Huyu CAG mzembe atimuliwe hakufanya kazi ya udhibiti
 
unampangia jina au unampingia kazi au? udhibiti unakuja kutokana mapendekezo yake.
wanatako fanya hiyo kazi ni serikal kùu si yeye.

oh CAG mzembe? ume muajiri ww? so far amefanya kazi yake.
hupendi kashtaki kwa mama samia
 
Magufuli ebu fufuka uje uchukue watu wako.

Mailman

kama hautajali waweza weka job description ya cag hapa.

hii itamsaidia YEHODAYA kuelekeza lawama zake mahala sahih.

asante kwa maelezo yako kuhusu cag anavyokaguliwa.
 
Udhibiti unafanyika na serikal kuu yeye anatoa mapendekezo tu. Kazi inabaki serikali kuu wafanyie kazi au lah.
Kwa hiyo hicho chao cha kuitwa mdhibitin ni utapeli au? Mbona anaitwa Mdhibiti?
 
Wewe tulia hivyo hivyo kama unanyolewa, CAG piga kazi mkuu achana na machawa 🤣🤣🤣 wanataka utoe report inayosifu na kuabudu tuu. Mr kichere ukimaliza kaz nenda nyumba ya ibada kamsifu na kumuabudu Mungu aliezifanya mbingu na nchi yeye anastahili kuabudiwa 🙏
 
Juzi CAG amesema kuwa kwa sasa ndio amepata watu na uwezo wa kufanya real time audit. Kabla alikuwa anafanya postmortem audit tu!
Budget na rasilimali watu bado havijamruhusu kufanya udhibiti.
 
Hii mada iko juu ya uwezo wako wa akili kaa nayo mbali
 
Hivi kumbe ni kweli vijana wengi wa CCM masomo yanayohusisha hesabu mliyakimbia? Mbona kila mtu toka huko akisikia hesabu analeta longolongo zisizo na kichwa wala miguu?
 
Budget na rasilimali watu bado havijamruhusu kufanya udhibiti.
Kwa hiyo tukububaliane kazi ya kudhibiti hajafanya.Mbona kwenye ripoti yake hakueleza hilo? Kuwa mimi.kama mdhibiti sikufanya udhibiti ndio masna mnaona haya madudu kwenye ripoti
 
Naunga mkono hoja Chikumbalaga aondolewe haraka sana kwa manufaa ya taifa letu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…