CAG: TSh. milioni 140 ambazo Wizara ya Maliasili na Utalii iliilipa kampuni ya Wasafi hazikuwa na Mkataba uliosainiwa

CAG: TSh. milioni 140 ambazo Wizara ya Maliasili na Utalii iliilipa kampuni ya Wasafi hazikuwa na Mkataba uliosainiwa

Kigwa hajajibu huko twitter!?
Huyo
IMG-20210408-WA0036.jpg
 
Kifo humstiri mtu na pia kifo Inakuwa njia pekee inayomnyamazisha mtu aliyejifanya mwema na kuwapa watu nafasi ya kujua maovu yake ambao alijigamba kuyasitiri katika Wema. Sasa tunaaza kuyajua Haya Yote. RIP mwenda zako but kuna watu itawabidi wakalie kwenye kaburi aise maana si kwa kuumbuka huku
 
Kibwangala amejikita kuwahoji maprofessa pale muhimbili methodology za kufanya utafiti ili atusahaulishe namna pesa ilivyotafunwa pale maliasili kwa kisingizio cha kutangaza utalii wa ndani......watu wanalipana pesa kama hazina mwenyewe...
 
Mkurugenzi Clods/CMG na viongozi wengine wachukuliwe hatua za kisheria,
TAKUKURU chukueni hatua ushahidi huo hapo kwenye ripoti ya CAG
 
Alafu Kigwangalla anakuambia pesa ya kulipia zike pikpik za Mo ni pesa alizopata kwa kuuza mchele🤣🤣🤣
 
Kwa hiyo Kigwangwalla na Diamond walipiga deal na kutafuna pesa za umma?
 
Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) imeeleza kuwa Sh140 milioni ambazo Wizara ya Maliasili na Utalii iliilipa kampuni ya Wasafi hazikuwa na mkataba wowote uliosainiwa.

Wizara hiyo ililipa fedha hizo kwa ajili ya wasanii ambao wangetangaza utalii wa ndani katika mikoa sita nchini Tanzania.

Akizungumza leo Alhamisi Aprili 8, 2021 katika mkutano na waandishi wa habari mjini Dodoma CAG, Charles Kichere amesema, “Wizara ililipa Sh140 milioni kwa kampuni ya Wasafi kwaajili ya wasanii ambao wangetangaza utalii wa ndani katika mikoa sita, hata hivyo hakukuwa na mkataba wowote uliosainiwa baina ya wizara na kampuni ya Wasafi na kushindwa kuhakiki wigo na huduma iliyotolewa na kampuni ya Wasafi.”

Amesema kiasi hicho cha fedha kilicholipwa kwa Wasafi hakiendani na sheria za matumizi ya fedha za umma.

Amebainisha upungufu uliobainika katika uanzishwaji wa tamasha la Urithi haukuwa na nyaraka zilizowasilishwa kwa ajili ya ukaguzi kuhusu matumizi hayo pamoja na Sh487 milioni zilipelekwa kwenye taasisi saba na kwamba hakukuwa na nyaraka zilizowasilishwa kudhibitisha matumizi hayo.

“Matumizi ya Sh585 milioni yaliyolipwa na mhasibu wa mfuko wa tozo ya maendeleo ya utalii hayakuwa na nyaraka toshelezi na kushindwa kudhibitisha uhalali wa malipo hayo,” amesema

Chanzo: Mwananchi Online
Hawa si wapo? Wazirejeshe tu hakuna namna nyingine! Dpp fanya jukumu lako hapa kwani ndio jukumu lako! Ile mahakama ya mafisadi inaelekea kupata wateja wa kutosha Sasa! Dpp amka fanya kazi yako kwani ushahidi unao na huhitaji uchunguzi mwingine!
 
Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) imeeleza kuwa Sh140 milioni ambazo Wizara ya Maliasili na Utalii iliilipa kampuni ya Wasafi hazikuwa na mkataba wowote uliosainiwa.

Wizara hiyo ililipa fedha hizo kwa ajili ya wasanii ambao wangetangaza utalii wa ndani katika mikoa sita nchini Tanzania.

Akizungumza leo Alhamisi Aprili 8, 2021 katika mkutano na waandishi wa habari mjini Dodoma CAG, Charles Kichere amesema, “Wizara ililipa Sh140 milioni kwa kampuni ya Wasafi kwaajili ya wasanii ambao wangetangaza utalii wa ndani katika mikoa sita, hata hivyo hakukuwa na mkataba wowote uliosainiwa baina ya wizara na kampuni ya Wasafi na kushindwa kuhakiki wigo na huduma iliyotolewa na kampuni ya Wasafi.”

Amesema kiasi hicho cha fedha kilicholipwa kwa Wasafi hakiendani na sheria za matumizi ya fedha za umma.

Amebainisha upungufu uliobainika katika uanzishwaji wa tamasha la Urithi haukuwa na nyaraka zilizowasilishwa kwa ajili ya ukaguzi kuhusu matumizi hayo pamoja na Sh487 milioni zilipelekwa kwenye taasisi saba na kwamba hakukuwa na nyaraka zilizowasilishwa kudhibitisha matumizi hayo.

“Matumizi ya Sh585 milioni yaliyolipwa na mhasibu wa mfuko wa tozo ya maendeleo ya utalii hayakuwa na nyaraka toshelezi na kushindwa kudhibitisha uhalali wa malipo hayo,” amesema

Chanzo: Mwananchi Online
Nje ya box yupo aliifanya wizara kama mali yake,sote tunakumbuka ugomvi wake na katibu mkuu wake, halafu leo hii ndio wa kwanza kumnanga mwendazake akijifanya msafi, si ajabu hata hao Wasafi hawakupata kitu.
 
😂😂😂 sitashangaa mkuu.
Hata mimi nakubaliana nawe , kwa ahadi kuwa watapewa dili lingine,katibu mkuu na waziri wote wapo na sasa katibu mkuu ni waziri na aliyekuwa waziri kawa mchunga ng'ombe,hawa wote wapo na Wasafi nao wapo ,mahakama zipo, tuanzie hapo .
 
Back
Top Bottom