Mparee2
JF-Expert Member
- Sep 2, 2012
- 3,092
- 5,386
Mkuu naomba tuhusike na maada ya mezani inayojikita kujua sababu hani kwamba hata kama nchi ina 80 % wakristo , waislam wanakuwa huru lakini nchi ikiwa hata na 55% muslims basi christians wanaminywa,
Nadhani hilo ndio lengo la maada, sio statistics
Kuhusu mada iliyopo mezani...
Chanzo cha msingi cha Chuki ya Waislam juu ya Wakristo ni zile Nchi zinazojiona Taifa la kwanza
wanaojengea Chuki wananchi wa Nchi za Kiislam na pengine kuzipiga Nchi zenye Waislam wengi/za Kiarabu kwa sababu dhaifu za kuunga unga.
Nchi hizo za ulimwengu wa juu zimekuwa zinajenga chuki juu ya Waislam pamoja na kupeleka mamluki wa kuzichonganisha ili Vita ianze na wao kutoa silaha kwa kundi moja wapo ili tu kudhoofisha Dola ya kiislam....wakati hayo yakitokea kumekuwa na baadhi ya Wakristo au niseme kundi kubwa la Wakristo kwa kujua au kutokujua hufurahia sana kinacho endelea katika Nchi hizo zenye Waislam wengi
Matokeo yake, baadhi ya Waislam hushindwa kujizuia hisia zao na hivyo kupelekea uhasama unaaendelea Duniani kwa sasa......