Cassie amfungulia mashtaka Diddy yakiwemo madai ya ubakaji na unyanyasaji wa kijinsia

Cassie amfungulia mashtaka Diddy yakiwemo madai ya ubakaji na unyanyasaji wa kijinsia

View attachment 2816118

Cassie amefungua kesi ya dola milioni 30 dhidi ya Diddy akimtuhumu kwa ubakaji na unyanyasaji wa kijinsia. Mwanadada huyo anasema muda mfupi baada ya kukutana na Diddy mwaka 2005, akiwa na umri wa miaka 19, alianza tabia ya kumdhibiti na kumnyanyasa ikiwa ni pamoja na kumlazimisha kutumia dawa za kulevya, kumpiga na kumlazimisha kulala na malaya wa kiume huku akirekodi filamu hizo.

Kesi hiyo imeibua hisia za watu wengi mtandaoni wakidai kuwa inaweza kuibua watu wengi waliofanyiwa vitendo kama hivyo na Diddy na kudai kuwa inaweza kuwa ndio mwisho wa Diddy.
acha wapambane na yakwao sisi pia tuna ya kwetu
 
Mara wadai jamaa ni shoga.

Anyway, kuanzia 2010 mpaka sasa watu weusi mashughuli wamekua wakishambuliwa sana na mashtaka ni ubakaji na unyanyasaji.

Cassie hataki jamaa ashtakiwe akutwe na hatia na kufungwa ila anataka dola milioni 30.

Nenda kwenye mpira, golf, uigizaji n.k kote huko watu weusi wameshtakiwa na sisemi kwamba hawana hatia maana kwa baadhi yao tumeshuhudia mpaka videos ila nafikiri uchuguzi uwe wa kina usiendeshwe na bias.
Ukishamshtaki mtu hutoichagulia mahakama adhabu na kama kosa ni jinai sio tu madai.

Maana yake Cassie amedhamiria Diddy aende korokoroni. Poor him ana watoto wadogo bado.

Hata hivyo, hawa wanawake wajifunze kuwa watu wa kwenye hii industry ya entertainment kwa ujumla most of them ni Psychos. Kuna vitu huwezi fanya ukiwa sober, lazima kuwe na busta fulani fulani ili mambo yaende. Ni bahati mbaya zaidi kwa weusi kulingana na historia zao za makuzi, mazingira,elimu etc.

They could have known it better. Kama ushahidi utapatikan mbona Watafungwa sana.
 
Miaka yote alikuwa wapi kuleta hayo madai? Kutakuwa kuna kikundi kiko nyuma yake.
Ningelikuwa ni muamuzi, ningelifutilia mbali haya madai
 
View attachment 2816118

Cassie amefungua kesi ya dola milioni 30 dhidi ya Diddy akimtuhumu kwa ubakaji na unyanyasaji wa kijinsia. Mwanadada huyo anasema muda mfupi baada ya kukutana na Diddy mwaka 2005, akiwa na umri wa miaka 19, alianza tabia ya kumdhibiti na kumnyanyasa ikiwa ni pamoja na kumlazimisha kutumia dawa za kulevya, kumpiga na kumlazimisha kulala na malaya wa kiume huku akirekodi filamu hizo.

Kesi hiyo imeibua hisia za watu wengi mtandaoni wakidai kuwa inaweza kuibua watu wengi waliofanyiwa vitendo kama hivyo na Diddy na kudai kuwa inaweza kuwa ndio mwisho wa Diddy.
Hawa wahuni wa kitambo wataishia gerezani aisee. Kha!
Sijui mzee Bill Cosby kaishia wapi. Baada ya kuchomoa tuhuma za awali, walikuja kulianzisha tena. Mzee wa Gotham City anachezea mvua saa hii. Duh!
 
Didy ni target kwa sasa hata kama hatoshindwa kesi zake zote ila reputation yake itaharibika na pia atapoteza pesa nyingi kwenye kesi kama Michael Jackson.
Jamaa wanaenda kumpoteza kashaenda nao kinyume sasa watafukua makaburi ambayo hata hatuyajui utashangaa hizo shutuma zitakavyomuandama
 
Mmmh Cassie anatafuta attention. Alikua wapi siku zote? Si atulie na mume wake
Ukiangalia maisha ya black Americans wengi walipitia trauma na kama wametokea kwenye hoods, lazma kuna vitu vya ajabu huwa wanavifanya ambavyo hutumika baadae dhidi yao.
Ukiangalia situation nzima hutakiwi kujiuliza mara mbili kuwa Hollywood ipo after Didy
1700221560232.jpg
 
Back
Top Bottom