Pre GE2025 Catherine Magige: Luhaga Mpina ni mtu wa ovyo ambaye haamini uongozi wa mwanamke

Pre GE2025 Catherine Magige: Luhaga Mpina ni mtu wa ovyo ambaye haamini uongozi wa mwanamke

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Namuunga mkono Mheshimiwa Mbunge kuwa 2025 FOMU ya Urais ndani ya CCM Ni moja tu kwa ajili ya Mama Samia ambaye ndio chaguo letu wana CCM wote kwa umoja wetu.

Hata hivyo CCM Ni moja yenye umoja ,upendo na mshikamano mkubwa sana kuliko wakati mwingine wowote ule.
IMG_20201105_142029.jpg

CCM bila vyombo vya dola, katiba mbovu, TumeCCM .

Ni weupe kama kile kichwa cha Makonda kilichopata division 0 kidato cha nne.
 
Namuunga mkono Mheshimiwa Mbunge kuwa 2025 FOMU ya Urais ndani ya CCM Ni moja tu kwa ajili ya Mama Samia ambaye ndio chaguo letu wana CCM wote kwa umoja wetu.

Hata hivyo CCM Ni moja yenye umoja ,upendo na mshikamano mkubwa sana kuliko wakati mwingine wowote ule.
Wewe sio mwanaccm wewe ni chawa uliyejitoa faham kwa ajili ya tumbo;
 
Mbunge viti maalum Arusha Catherine Magige amvaa kwa matusi mbunge mwenzake.

Amemshambulia kwa matusi mbunge Mpina utadhani wapo vyama tofauti.

Hii ni dalili tosha kuwa CCM sasa hivi kuna moto unawaka chini kwa chini.

Hakuna amani tena.

Tuombe Mungu azidi kuukoleza na sisi wazalendo kazi yetu ni kuongezea Kuni tu.

View attachment 2877418
Mpina si wakupigwa mkwara na boya kama huyu
 
Mbunge viti maalum Arusha Catherine Magige amvaa kwa matusi mbunge mwenzake.

Amemshambulia kwa matusi mbunge Mpina utadhani wapo vyama tofauti.

Hii ni dalili tosha kuwa CCM sasa hivi kuna moto unawaka chini kwa chini.

Hakuna amani tena.

Tuombe Mungu azidi kuukoleza na sisi wazalendo kazi yetu ni kuongezea Kuni tu.

View attachment 2877418
Kwanza kabisa, nianze kwa kusema, tunavyosema Wanyamwezi, "I don't have a dog in this fight". Huu si ugomvi ambao nina upande wowote maalum kwa maana ya Mpina au Magige.

Inawezekana Mpina ana makosa yake, personally naona hata Mpina akiwa na point, presentation yake ni ya kukurupuka zaidi, kwa hivyo siko hapa kumtetea Mpina.

Lakini pia, kuna kitu nakiona kinajirudiarudia CCM, hususan kwa baadhi - msisitizo ni kwenye baadhi, si wote - baadhi ya wanawake wa CCM.

Hivi, kwanini mtu anayemsema Rais, kama Rais, si kama mwanamke, anachukuliwa kwamba anamsema Rais kwa kuwa ni mwanamke?

Kuna inferiority complex miongoni mwa wanawake hawa wa CCM inayowafanya waone kuwa, Rais anapokosolewa tu, basi ni lazima anakosolewa kwa sababu ni mwanamke, na si kwa sababu ni rais?

Watanzania tunataka Rais anayeweza kukosolewa, hatutaki Rais aliyevishwa bullet proof ya kutoweza kukosoleka kwa sababu ni mwanamke.

Ikiwa hivyo tutasema wanawake hawafai kuongoza, kwa sababu wakipata uongozi tunakatazwa kuwakosoa, tukiwakosoa tunaambiwa kwa nini tunakosoa wanawake?

Hawa wanawake wanaweza kumuangalia Rais Samia kama Rais kamili, kama Rais, na si kama Rais Mwanamke au Mwanamke?

Mlio nyumbani labda mtanisaidia vizuri, sijamfuatilia Mpina muda, I don't put anything past him either. So labda mimi ndiye niko out of touch na kauli zake za karibuni.

Kuna kauli mahsusi ya kunyanyapaa mwanamke ambayo Mpina ameitoa imemfanya Magige aseme hivi?

Labda kuna kauli mahsusi ya kunyanyapaa wanawake kaisema Mpina sijaisikia mimi jamani?

Maana isije kuwa wanasiasa wanaamua kujificha kwenye chaka la uanamke, na kutaka kupata kinga Rais asisemwe na mtu, na akisemwa tu, wanakimbilia kulalamika kwamba Rais anasemwa kwa sababu ni mwanamke.

Kufanya hivyo kutakuwa ni kumvunjia heshima rais na kuwavunjia heshima wanawake.

Mbona marais wote wamepingwa? Mbona Nyerere kapingwa mpaka kafanyiwa njama za kupinduliwa mara mbili?

Nyerere alikuwa mwanamke?

Mbona Mwinyi kapingwa mpaka kachorwa na Punch?

Mwinyi ni mwanamke?

Mbona Mkapa kapingwa mpaka kasomewa risala za kupinga ubinafsishaji?

Kwani Mkapa alikuwa mwanamke?

Mbona Kikwete kapingwa mpaka kwenye nomination za CCM urais kapata mpinzani kutoka CCM John Shibuda, wakati Kikwete akiwa Rais? (Kitu ambacho CCM wengine wanataka kuzuia 2025)

Kwani Kikwete ni mwanamke?

Mbona Magufuli kapingwa sana mpaka kapiga marufuku mikutano ya hadhara ya vyama vya upinzani Tanzania?

Kwani Magufuli alikuwa mwanamke?

Kuna kauli gani Mpina kaitoa kunyanyapaa wanawake kwa Samia?

Vinginevyo, msimnyime Rais Samia haki yake ya kupingwa sawa na marais wote waliopita, kwa sababu yeye mwanamke tu.

Ukubwa gunia la chawa. Kalitaka mwenyewe. Nyerere alisema Ikulu si sehemu ya kukimbilia pale, kuna matatizo chungu mbovu.
 
Haya yameshapangwa, huyo mpina 2025 hapitishwi na CCM, na kura zitaibwa ili asishinde
Huyu mdada ni collateral tu kwa kuwa ni non elect member ndio maana anatumika
Hii nchi hakuna wa kuishinda CCM, the rest is history
 
Nilichogundua hii nchi viongoz wengi hawana uzarendo kabisa ila wanateuana kwa lengo la kulindana na kulinda masrah yao tu.
Mkuu mbona Hilo la pili ndiyo uhalisia?

Nchi hii hakuna kiongozi mwenye nia ya dhati ya kuwaongoza wananchi kwenye kutafuta maendeleo.

Wote wanaingia kujitafutia mali
 
Back
Top Bottom