Uchaguzi 2020 Catherine Ruge: Kwa mateso haya niliyoyapata, siwezi kusaliti chama changu na Wananchi wangu wa Serengeti walioniamini

Mawazo yake yaheshimiwe
 
Ameandika hivi kupitia twitter:

Kwa Mateso na Maumivu haya niliyopitia Siwezi kusaliti chama Changu na Wananchi wa Serengeti walioniamini na Kunipa Heshima Kubwa Kama Msubhati wao.
Ni kwa kikosa hiyo mafasi, ndo kaandika hivyo,
Sasa asubili miaka mitano aone yeye anapauka wenzake wanapendeza kisha wanakutana wakiwa sawa kwenye chama.
 
Hapa naona unazungumzia wafadhili mara misaada..fanya kazi ww acha kuwaza kufadhiliwa fadhiliwa utapangiwa mpaka siku ya kulala na mkeo...wale ni wanachama na wanakadi halali sasa kama walichaguliww waache?? Kumbuka esther matiko ni mke wa mgombea mwenza je na yeye hajui kua mkewe anaenda kuapa?? Mpaka watu wanashona sare unadhani ilikua ghafla kama kichomi?? Toa upuuzi wako hapa au kwakua mkeo hayumo?? Nyau we
 

Mkuu hata Lissu hawezi Amini ulichoandika. Tena unaota mchana. Lissu asingeweza pata hata kula Mill 3.
 
Prof Kabudi juzi aliwaambia kuwa Tanzania 🇹🇿 haijawahi kushindwa vita, iwe ya ndani au nje.Watu walimtukana sana humu jf na mitandao.Huyo ni Profesa anajua anachozungumza.Sasa kaeni kimya yajayo ni neema.Catherine ajiandae kuanzisha kampuni ya biashara JPM anataka kutengeneza mabilionea anaweza kwenda line ile
 
wakiendelea na ubunge watakuwa wa chama gani
Salaam ndg mwananchi mwenzetu na mwanachama wa Chadema

Chadema ni chama kikubwa kabisa hapa nchini lakini kiukweli kuna vitu vinatokea ama kufanywa na wanachama ama viongozi wake vya kustaajabisha kiasi,,Chama kinakosa utulivu wa kutosha kwenye vipindi vigumu na wanachama mnatoa presha kubwa kiasi ambacho nafikiri maamuzi ya chama yanategemea mitandaoni watu wao wanaelekea mlengo upi..ni dhahiri hakuna kinachoeleweka kwa jamii kwa tukio la jana! Mdee anamshukuru Mwkti wakati KM hawatambui...ni kweli chama kinakosa namna ya kudeal na Jambo la naman hii kiasi linachanganya jamii namna hii??

Wazee huwasikii tena na mliwabeza kiasi fulani na wakatulia,,Prof Baregu na Prof Safari mlikosea pakubwa sana kuwaona hawafai...

Chama kuongozwa kwa mitazamo ya wanamitandao ni sawa lakini lazima kiwe na uwezo wake binasfi,,inatia aibu!
Dr mkasema msaliti,,Zitto msaliti,,Lwakatare na wenzake wasaliti,,leo Mdee,,Matiko,,Bulaya wasaliti,,,
Publicly figures wamebaki Lissu,,Mbowe,Mnyika,Sugu,Lema,Pro J, na Heche. Mnaiaminishaje jamii ya watanzania!

Wakumbukeni wazee wenu wa chama kwa ushauri msiwapuuze naamin Wana mchango mzuri kwa chama.
 
Kwa hiyo kwako wewe kila kitu ni kuwa wabunge tu? Unaamini kabisa kuwa na wabunge waliowekwa na chama tawala ndio kutafanya wananchi na ulimwengu uamini kuwa ni Bunge la vyama vingi? Hawa wakifukuzwa na chama chao watakosa legitimacy na wataonekana mbele ya jamii kuwa ni puppets. Mbaya zaidi mchango wao mkubwa waliotoa katika siasa za upinzani zitaingia walakini. Kwa mwana siasa mahiri legacy yake ni muhimu kuliko cheo au mshahara.

Amandla...
 
Umesahau yale ya bunge lililopita? Kuna wabunge wa CDM walihama chama, wakajitoa CDM na wakapoteza ubunge kwa mujibu wa sheria, Ndu-gayi akawabakiza mjengoni na wakaendelea na ubunge kwa "sheria" yake
Chama kiwafukuze, wamwachie Ndugai na CCM wawang'ang'anie ndio wazidi kuongeza chuki kwa wananchi!
 
Hao wakiendelea na ubunge nyinyi mtashindwa kufanya siasa? mbona hamjiamini au kwa sababu hamjachaguliwa mnataka kila mmoja akose.
 
Ameandika hivi kupitia twitter:

Kwa Mateso na Maumivu haya niliyopitia Siwezi kusaliti chama Changu na Wananchi wa Serengeti walioniamini na Kunipa Heshima Kubwa Kama Msubhati wao.
kwani chama ni mama yake?
atakufa masikini we muache tu.
 
Ameandika hivi kupitia twitter:

Kwa Mateso na Maumivu haya niliyopitia Siwezi kusaliti chama Changu na Wananchi wa Serengeti walioniamini na Kunipa Heshima Kubwa Kama Msubhati wao.
1. Catherine Ruge
2. Susan Kiwanga
3. Upendo Peneza
4. Devotha Minja
5. Yosepha Komba
6. Hilda Newton
7. Husna Said, yule binti wa Chato
8......

Bado kuna wapiganaji Bawacha. Msihukumu wanawake wote wa Chadema kwa matendo ya wachache.

Kuvunjika kwa koleo....

Amandla...
 
Wabunge wa mahakama. Wakitimuliwa wanaenda mahakamani kupinga then wanaendelea na ubunge wao. Zitto alishawahi fanya hii alipotimuliwa chadema

Zitto hakwenda mahakamani, fanya rejea vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…