CCM chini ya Mwenyekiti wake Samia Suluhu Hassan iko imara kuliko kipindi chochote

CCM chini ya Mwenyekiti wake Samia Suluhu Hassan iko imara kuliko kipindi chochote

Toka Chama cha Mapinduzi kuundwa mwaka 1977 kimepita baada ya kuunganishwa kwa vyama vya Tanganyika African National Union na Afro - Shiraz, CCM imekuwa Imara, Bora na yenye mshikamano kuanzia ngazi ya chini kabisa mpaka ngazi ya Taifa kuliko kipindi chochote cha uhai wa CCM.

Kabla Mama Samia Suluhu Hassan hajakabidhiwa kijiti cha kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, iliaminika ikuwa CCM ni chama ambacho kinabebwa na mfumo , iliaminika kuwa CCM ni chama ambacho hakipendwi na Vijana, kwa lugha nyepesi ilionekana ni Chama cha Wazee.

Mama Samia Suluhu Hassan amefanikiwa kwa asilimia 100 kurudisha imani kwa Vijana kuwa CCM ndio chama bora, chama rafiki, chama chenye kubeba maono ya Watanzania, CCM ya sasa chini ya Mama Samia Suluhu Hassan Hassani si kile chama kilichokuwa kinategemea nguvu ya dola.

Watanzania kwa sasa wanashuhudia CCM yenye siasa za kiungwana, hakuna tena yale matamko ya kibabe, majivuno na ya kutishana kutoka kwa Katibu Mkuu wa CCM au kutoka kwa Katibu Itikadi na Uenezi, CCM ya sasa ni ile inayoendesha siasa zake kistaarabu saana.

Mama Samia Suluhu Hassan ameweza kutenganisha vizuri kati ya mamlaka ya Serikali na Chama, CCM imeweza kuisimamia Serikali vizuri hasa katika utekelezaji wa miradi ya Maendeleo, ni CCM iliyo chini ya Mama Samia Suluhu Hassan ambayo imeweza kuhakikisha hakuna mwanafunzi anayekaa chini, imehakikisha kila mtoto mwenye umri wa kwenda shule ameanza shule, imeweza kumtua Mwanamke ndoo kichwani kwa kuhakikisha maji safi na salama yanafika kila kijiji, imehakikisha umeme umefika kata zote Tanzania, imehakikisha kila Kata kunakuwa na Kituo cha Afya, kila Kijiji kunakuwa na Zahanati yenye vifaa na madawa, CCM kwa kuisimamia Serikali vizuri imeweza kumalizia miradi iliyokuwa imekwama kwa miaka mingi ikiwa ni pamopja na umaliziaji wa maboma ya vyumba vya madarasa na Zahanati.

Hongera sana Mama Samia Suluhu Hassan, Hongera sana Daniel Chongolo kwa kuitengeneza CCM IMARA inayopendwa na Watu wote.

Ni hivi, mpake mafuta huyo mama kwa mgongo wa chupa utakavyo, lakini iko wazi kuwa ccm sio chama cha kizazi hiki. Ccm ni chama cha watu wa kizazi kilichopita, na wako madarakani kwa shuruti. Hawana uwezo tena wa kushinda uchaguzi wowote kihalali zaidi ya kutegemea vyombo vya dola. Ni kweli huyu mama hana siasa za kihayawani kama alivyokuwa Magu, lakini hana ubora wowote wa kiuongozi.
 
Toka Chama cha Mapinduzi kuundwa mwaka 1977 kimepita baada ya kuunganishwa kwa vyama vya Tanganyika African National Union na Afro - Shiraz, CCM imekuwa Imara, Bora na yenye mshikamano kuanzia ngazi ya chini kabisa mpaka ngazi ya Taifa kuliko kipindi chochote cha uhai wa CCM.

Kabla Mama Samia Suluhu Hassan hajakabidhiwa kijiti cha kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, iliaminika ikuwa CCM ni chama ambacho kinabebwa na mfumo , iliaminika kuwa CCM ni chama ambacho hakipendwi na Vijana, kwa lugha nyepesi ilionekana ni Chama cha Wazee.

Mama Samia Suluhu Hassan amefanikiwa kwa asilimia 100 kurudisha imani kwa Vijana kuwa CCM ndio chama bora, chama rafiki, chama chenye kubeba maono ya Watanzania, CCM ya sasa chini ya Mama Samia Suluhu Hassan Hassani si kile chama kilichokuwa kinategemea nguvu ya dola.

Watanzania kwa sasa wanashuhudia CCM yenye siasa za kiungwana, hakuna tena yale matamko ya kibabe, majivuno na ya kutishana kutoka kwa Katibu Mkuu wa CCM au kutoka kwa Katibu Itikadi na Uenezi, CCM ya sasa ni ile inayoendesha siasa zake kistaarabu saana.

Mama Samia Suluhu Hassan ameweza kutenganisha vizuri kati ya mamlaka ya Serikali na Chama, CCM imeweza kuisimamia Serikali vizuri hasa katika utekelezaji wa miradi ya Maendeleo, ni CCM iliyo chini ya Mama Samia Suluhu Hassan ambayo imeweza kuhakikisha hakuna mwanafunzi anayekaa chini, imehakikisha kila mtoto mwenye umri wa kwenda shule ameanza shule, imeweza kumtua Mwanamke ndoo kichwani kwa kuhakikisha maji safi na salama yanafika kila kijiji, imehakikisha umeme umefika kata zote Tanzania, imehakikisha kila Kata kunakuwa na Kituo cha Afya, kila Kijiji kunakuwa na Zahanati yenye vifaa na madawa, CCM kwa kuisimamia Serikali vizuri imeweza kumalizia miradi iliyokuwa imekwama kwa miaka mingi ikiwa ni pamopja na umaliziaji wa maboma ya vyumba vya madarasa na Zahanati.

Hongera sana Mama Samia Suluhu Hassan, Hongera sana Daniel Chongolo kwa kuitengeneza CCM IMARA inayopendwa na Watu wote.
3001942_SAMIA_KIJESHI.jpeg
 
Daaah! Mnamdanganya sana mama yetu.

Hatutaki afe na presha tunamhitaji ni hazina yetu.

Tumwambie ukweli.

CCMimemaliza mvuto kwa wananchi na wanachama wake. Sababu ni msoga
CCM iko imara, nimezunguka mikoa yote ya Tanzania nimeona imani ya Vijana na Watanzania kwa ujumla waliyo nayo kwa Chama cha Mapinduzi na kwa Rais Samia Suluhu Hassan
 
CCM ilikuwa ife 2015, kipindi kile hata ukivaa nguo ya CCM unapigwa mawe na kuzomewa.

Bahati nzuri wakamteua Magufuli, ikabidi atumie brand yake ya uchapakazi kuinusuru.

Huyu aliiheshimisha CCM. Akaachana na mafisadi na wauza madawa ya kulevya. CCM tena ikaanza kuaminika na kuwa na mvuto.

Ametoka Magufuli akaingia mama. Anakumbatiana na walewale waliotaka kuiua CCM 2015. CCM inapoteza mvuto kwa kasi ya ajabu.

Ni vile hatuna tu upinzani wa kweli, waliopo ni wachumia tumbo. Otherwise come 2025 CCM ingetoka madarakani!
Mkuu CCM hii ni imara kuliko kipindi chochote..Hakuna upinzani utakao wenza shindana na Ccm hii ya Samia
 
Kabisa!

Ukiona hata machadema yameunga tela kumsifia mama ili kumkomoa marehemu jiwe jua hapo kuna jambo.

Yani ccm na hangaya 2025 watakuwa na kazi rahisi sana.

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app

Dhalimu hakomolewi bali alikuwa kiongozi mshenzi. Ww ndio ulikuwa unashoboka naye.
 
Tunaomba CCM imara msimamie Serikali ya mama kwenye bei ya mbolea maana tunajua kuna vita huko Ukraine ila sio kwa kupanda hivyo.
Mkuu ROBERT MICHAEL kuwa na imani na Ccm, Ccm ya sasa ina macho na masikio, Mwenyekiti wetu anawaambia Wananch ukweli vitu vingi vinapanda bei kwa sababu ya vita ya Russia..
 
Yanatoka moyoni au ndio zile fitina mnazosema kinaa kuwa ni mwiko hapo mtaani kwenu[emoji848]
Nikiwa Mtanzania tena Mzalendo, nimetemebea kusini na kaskazin, mashariki hadi magharibi, kwa kweli vyumba vya madarasa vinavyojengwa, zahanati, vituo vya Afya, hospital, miradi ya maji etc kwa kweli haya ninayoongea yanatoka moyoni
 
CCM ilikuwa ife 2015, kipindi kile hata ukivaa nguo ya CCM unapigwa mawe na kuzomewa.

Bahati nzuri wakamteua Magufuli, ikabidi atumie brand yake ya uchapakazi kuinusuru.

Huyu aliiheshimisha CCM. Akaachana na mafisadi na wauza madawa ya kulevya. CCM tena ikaanza kuaminika na kuwa na mvuto.

Ametoka Magufuli akaingia mama. Anakumbatiana na walewale waliotaka kuiua CCM 2015. CCM inapoteza mvuto kwa kasi ya ajabu.

Ni vile hatuna tu upinzani wa kweli, waliopo ni wachumia tumbo. Otherwise come 2025 CCM ingetoka madarakani!

Chini ya Magufuli ccm ilitoka kuwa chama cha siasa na kuwa chama cha mumiani, chini ya utawala wa Magufuli chaguzi zote ziliendeshwa kihayawani. Kuteka, kubambikizia kesi, mauaji nk. Alitawala kwa kiburi cha madaraka, ndio maana idadi ya wapiga kura ilishuka kuliko maelezo, hadi ikabidi apike idadi ya wapiga kura. As a result wananchi kwa sasa wamelipuuza box la kura, na sitegemei kuona tena wapiga kura wengi, labda ipatikane katiba mpya.
 
Vijana wa CCM kazi yao kusifia hata kama nchi inaelekea shimoni
Mkuu nini nilichosifia ambacho ni uongo? Je hupiti vijijini ukaona Wananchi walivyo na furaha sasa? Wanafunzi wote wanakaa kwenye viti, Zahanati kila kijiji, vituo vya Afya kila Kata, Hospital za Wilaya zinaboreshwa, Maji safi na salama kila sehemu..Je yakufaa nini kudanganya fahari ya macho yako?
 
Mkuu CCM hii ni imara kuliko kipindi chochote..Hakuna upinzani utakao wenza shindana na Ccm hii ya Samia
Ccm ni chama outdated na haitakaa iwe na mvuto tena. Hiyo ccm ni kama bendi za sikinde na Ottu jazz, muda wake wa kung'aa ulishapita. Usitegemee kama bendi hizo zitakaa zipate mvuto tena maana kizazi chao kilishapita.
Labda kama unaishi Sayari tofauti na hii lakini kiuhalisia Ccm kwa sasa hali ni mbaya hamna mvuto tena kama kipindi cha Mzee JPM

Chini ya Magufuli ccm haikuwahi kuwa na mvuto bali ya vitisho na ulevi wa madaraka.
 
Hivi kwanini kauli kama hizi msingekuwa mnazitoa wakati kuna uwanja sawa wa kufanya siasa jamani. Kuna faida gani kujidanganya?

Nashauri, mwambieni mama ukweli! Ukweli utawaweka huru.

Wekeni mazingira sawa ya siasa. Wekeni uhuru wa kufanya siasa, wekeni Tume huru ya uchaguzi, Tangazeni matokeo jinsi yatakavyokuwa kisha ndio mkae mseme mvuto umeongezeka wakuu. Unasemaje mvuto umeongezeka ilhali ni wewe peke yako ndio unakimbia nchi nzima kufanya siasa?
Mkuu Amini nakwambia, kama Wapinzani watashindwa kufanya siasa kipindi hiki basi ni bora kuwa na mfumo wa Chama kimoja, mnyonge myongeni ila haki yake mpeni, Mama Samia ametengeneza neutral ground katika nyanja ya siasa ndani ya mwaka mmoja...Ndugu yetu Mbowe alienda kwenye kongamano Iringa hakuna aliyemzuia..
 
Back
Top Bottom