CCM ikitaka kupata Airtime ya kutosha iwanunue Mbowe, Mnyika na Tundu Lissu hawa mnaowanunua mtafirisika bila mafanikio

Neno kununuliwa!! Tunanunua mbuzi, kuku nk siyo kiumbe chenye akili. Kiumbe chenye akili hufanya maamuzi yawe is anakufurahisha kama ya Nyalandu au ya kukukera kama ya mashinji.
 
Neno kununuliwa!! Tunanunua mbuzi, kuku nk siyo kiumbe chenye akili. Kiumbe chenye akili hufanya maamuzi yawe is anakufurahisha kama ya Nyalandu au ya kukukera kama ya mashinji.
Je ikitokea binadamu mwenye akili akajiuza anakuwa na tofauti gani na mbuzi ?
 
Lawama zote kwa mwenyekiti, 2015 alibadili gia angani sasa tunaelekea siko. Aliwaacha watu waliopambana na chama na kuchukua mamluki, ona sasa mamluki wanachofanya. Dr slaa tutamkumbuka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaaa, ninyi mnaoanza kuifahamu siasa juzi mnashida sana. CHADEMA toka kuanzishwa kwake haijawahi kuwa na mtu kama DR. WILBROAD SLAA huyu alikua injini kweli kweli.

Ukimuuliza mwanaccm yeyote atakuambia huyu mtu alitupasua kichwa ges what karudi CCM mwee jamaniiii.

Huyu Bw. alikua mtu na nusu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hujanitaja mimi,kwanini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Slaa alipokelewa chadema baada ya kukatwa ccm , kwahiyo hakutokea chadema , alikuwa kama lowassa , mwambe au Sumaye
 
Esli
nunua hadi Msando sasa hivi Msando anakula.Maisha huko Songwe walimpa ajira. Hawakuambulia chochote
 
Mimi naomba nikuulize swali moja tu mkuu Erythrocyte:

Hivi huko vijijini, mijini na mitaani, bado mnao madiwani?

Kama bado wapo, hao ndio watu wa chama. Hao ndio watu wa kuwekeza kila raslimali mlizonazo.

Ni bahati mbaya sana mnawekeza sehemu ambazo matokeo yake kwa chama ni hafifu.

Chama kinatakiwa kiwe zaidi huko mitaani, nyinyi mnang'ang'ania makao makuu!
 
Baada ya ulaghai wote huu natamani kwa mara ya kwanza kabisa waTanzania waonyeshe uelewa na ukomavu wao na kutoa somo linalostahiri.

Wakiweza kufanya hivyo, nitaelewa Tanzania tumepiga hatua mhimu sana kwenda mbele.

Hawa watu wamepiga kampeni miaka minne mfululizo peke yao bila ya pingamizi lolote.

Baada ya yote hayo, bado wanao wasiwasi mkubwa juu ya uamzi wa waTanzania juu yao, na ndio sababu ya purukushani hizi zinazoendelea sasa.

Ni wazi kabisa wanayo hofu kubwa, na hili litawasababisha wafanye mambo yasiyostahiri kufanyika ndani ya taifa hili.
 
Up to now, you should have known that, politicians have price tags, the people you have mentioned are not gold standards for opposition parties in Tanzania meaning that they can be bought too.

Na ukiweza imani kwa watu basi hauna imani na mile unacho sema unakiamini.
 
Lipumba naye mpinzani/?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…