CCM imempa Mbowe nguvu isiyokuwa na mfano

Hilo lipo kila mahali. Nilikuwa naenda Mwanza, kupitia Bariadi, nikiwa Bariadi, tena siyo Bariadi mjini, eneo moja linaitwa Dutwa, watu ambao sikutarajia, nikawasikia watu wanakijiji wanaongelea suala la Mbowe...
Mkuu walimdharau Sana na kudhani wakishampa kesi kubwa Basi watapumua, ndo maana Kingai alimwambia Mbowe kuwa 'safari hii hutoki' Ila kwa Hali ilivyo wameshajuta Sana ila ndo hivyo wanashindwa watamchomoaje.

Kwa mkoa wa Arusha juzi nilikuwa kule nilikutana na wamama Wana hasira na Samia hatari
 
Uwape nchi wewe na nani?.maana inaonekana unaongea mambo usiyokua na uhakika nayo.hizo stori za ukabila ni hoja mfu zilizotengenezwa na wahasimu wa chadema kisiasa kwakukosa hoja lakini hazina msingi wowote nani wimbo uliokosa kiitikio kwa sasa na ni aibu wewe kuuleta sasa kwenye dunia ya wastaarabu.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Wajuzi wa mambo wanaeema kwamba, kumuweka Mh. Freeman Mbowe ndani kwa kesi ya ughaidi, imemuongezea Nguvu kubwa mno kisiasa...
Kwa mavoni yako ni nani jajizolea misifa kati ya Tundu Lissu na Mbowe, wote wameumizwa.
 
Hiyo ndiyo shida, pale mnapokataa kufanya image analysis yenu.
 
Ndiyo maana ccm wameng`ang`ana Mbowe aombe msamaha kupitia vibaraka wao act wazalendo ili wakifanikiwa katika hilo watakuwa wamemmaliza kisiasa, lakini kitendo cha Mbowe na viongozi wa chadema kubaki ngangari kinawauma sana ccm na vibaraka wao
 
Kesi ikiendelezwa hadi 2025 je?
 
Hahahaaaaa sio wananchi hao ni abiria mkuu
 
Kumbeeee
 
Wakimdharau yeye Samia anapata hasara gani?
 
Akina Mashinji tuliwapa nafasi ktk hatua za kutaka kufita ile notion ya ukabila unaona alichofanya??

Akina Zitto waliewa nafasi ili kuondoa kile mnachoamini kama udini lakini unaona alichofanya??

Watu shupavu na wenye ujasiri wanafanikiwa sana. Wakishafanikiwa wanaitwa wakabila na wabaguzi sio kweli.

Miaka ya Nyuma wachaga walikuwa wanalaumiwa sana kuwa wanapeana ajira kwa undugu.

Nilipotembea nikasoma na kukutana nao pande nyingi nilikuta hawa jamaa ni wapambanaji sana. Wanajituma. So ikitokea nafasi mathalani Ajira utakuta wana sifa na vigezo vya kutosha. Wakipaya hiyo fursa utaona waoa tu ndio wanajaa ni rahisi kudhani wanapendeleana.

Mama wa kichaga mjane anafuga ng'ombe watatu wa maziwa na mbuzi kadhaa lakini anasomesha watoto wake wawil St Mary's wakati mnyamwezi mwenzangu ana ng'ombe 200 na watoto 30 hakuna hata anayesoma form four.

Kijana wa kiume au wa kike mpatie Laki tano aende mjini baada ya miaka 5 atakukabidhi duka la milioni tano. Wakati kijana wa kike au kiume mhehe mwenzangu baada ya miezi miwili hana hata mia. Akiwa wa kike anarudi nyumbani na mimba au watoto wawili wasiojulikana baba zao.

Mifano inatosha.
 
Umesema sahihi, na mimi naomba ku declare interest kwamba siku zote nimekuwa nikipigania equal distribution of opportunities but based on qualifications rather than kujaza namba.
Katika msingi wa mifano yako, haina maana kwamba huko St Mary's wanaosoma kule ni Wachaga tu, au wapambanaji niwao peke yao, ili uhalalishe kwamba hakuna uwezekano wa kupata watu wenye sifa kutoka sehemu zingine.

Hakuna mpambanaji kama Mkinga nchi hii. Na kwa umoja wa kitaifa, mara nyingine inahitajika mikakati maalumu ya kupromote kule kuliko backwards ingawa si kuwapa vyeo kama lizimonko alivyobadilishwa na Lukuvi.

La mwisho ambalo umesema, ukweli kabisa "MLIWAPA", kina zito, mashinji n.k. Huko kuwapa ndiko tunakokutaaa. Hata wao walijiona "WAMEPEWA", na hivyo wakajiona bado ni wakuja ndani ya chama. Hiyo dhana ndiyo mnapashwa kuindoa. Hampashwi kujiona ninyi ndio first class na mnaowapa Wanakuwa 02nd class, third nakuendelea.

Huko "kuwapa", inasura, rangi na harufu ya ubaguzi... Na hii inawafanya wajisikie wakuja, strategic tools na hawana haki. Sasa mnachopashwa kukifanya siyo kuwapa.

Ninyi "mnaowapa" ni nani kwanza? Wanagundua kwamba mnawatumia kuwafunika na kusukuma agenda zenu kama objects. Kwa kutokujisika at home, ndiyo sababu waliondoka.

Sasa acheni hiyo "notion", ya kujiona ninyi ndio wenye chama, wengine "mnawapa".Ondoeni huo u "mimi", muone chama ni cha Watanzania wote na kila mwanachama anapoingia ajisikie "Nyumbani", na si mgeni. Achieni madaraka si kwa bendera, bali kwa uhalisia kwa watu wengine.

Mfano Mkti atoke Mtwara, Katibu atoke kaskazini, Na wengine watoke central, coastal n.k. n.k. na wawe na sauti na treatments sawa ndani ya chama. La sivyo, hizo itikadi za kusema "tuliwapa", ndizo haswa zinazofanya watu wa waone hamfai kuongoza taifa.
"Kuwapa watu vyeo halafu remote mnabaki nayo ninyi ambao "mnawapa", ndio huo ukabila, na kufanya chama kama mali ya kundi fulani wengine ni wakuja, ama nyenzo tu".
 
Ndiyo maana ccm wameng`ang`ana Mbowe aombe msamaha kupitia vibaraka wao act wazalendo ili wakifanikiwa katika hilo watakuwa wamemmaliza kisiasa, lakini kitendo cha Mbowe na viongozi wa chadema kubaki ngangari kinawauma sana ccm na vibaraka wao
Tena sana
 
YAANI MTU ANAFUNGWA HALAFU UNASEMA WAMEMPA NGUVU?URIO KESHAMMALIZA HUKO
 
Kwani wataishi milele? Sio Mbowe, Hangaya, Kingai ambae ana uhakika wa 2025 atakuwa hai, tenda wema
Si ndio kama hivi wanawarithisha watoto wao ili mfumo wao wa kiutawala udumu?. Watoto nao watawarithisha watoto wao.
 
Ni uongo kuwa uongozi wa juu ktk CDM umetekwa na ukabila?
 
Ndyo kinachowafanya ikulu waisikie tu watu wanaogopa CDM itakuwa hatari kuliko Ccm na ndyo ukweli wasipobadilika tutawapa pole tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…