CCM ina misingi imara sana; kama wewe ni mpinzani na unabisha umeshafeli

Huo ndio ukweli Mama D, hakuna vyama vya upinzani na vilivyopo ni CCM (B), CCM (C) etc. Kitu pekee kitakachowatoa CCM madarakani ni nguvu ya umma yani ifike siku watanzania wote kwa umoja wao waseme enough is enough kama kule Sri Lanka ndio siku CCM itatoka kabisa na siku hio sio leo wala kesho. Hawa upinzani wa sasa ni wachumia matumbo tupu ambao ni hatari kuliko hata hawa ccm wenyewe.
 
wewe mama D na Mnyeti ARUMERU inawakumbuka kwa kuwafikisha madiwani na wabunge bei. Na bado unajisifu kuwa ni msingi bora wa CCM?
 
TUNAELEWA SANA.

HUWEZI WAPA DOLA WATU WASIOJIELEWA, WASIOELEWEKA, WASIO NA MISINGI IMARA KWA WATU WAKE
Kwani hii dola ni Mali binafsi ya nani hadi awe na mamlaka ya kuigawa apendavyo?
 
Hakuna chama cha siasa kinaitwa CCM ndugu, CCM ni dola inayotawala Tanzania kwa njia ya mabavu, kwa kutumia advantage ya unyonge wa Katiba yetu kutetea wananchi wake, Katiba ambayo tuliyokopi toka kwa wakoloni.
 

Hizi porojo ndio matamanio ya kila mwanaccm.
 
wewe mama D na Mnyeti ARUMERU inawakumbuka kwa kuwafikisha madiwani na wabunge bei. Na bado unajisifu kuwa ni msingi bora wa CCM?

Moja uwezo au nguvu ya chama imara ni kuyabadilisha wananchi kurudisha imani kwa chama

Sio kama kina tundu wanaenda kula na watoto wao ughaibuni kisha wanakuja kuomba kura huku
 

Jambo la kwanza kulishughulikia ni kujenga uelewa kwa wananchi. Ni kuwaelimisha kwamba serikali ni tofauti na sisiem. Serikali ni jambo lingine na ccm ni kitu kingine. Kwa hiyo wasichanganye akilini mwao kwamba sisiemu ndiyo serikali na serikali ndiyo sisiem.
 
Kwani hii dola ni Mali binafsi ya nani hadi awe na mamlaka ya kuigawa apendavyo?

Dola haijagawanywa na chama. Dola inatenda haki kwa kuzingatiwa maslahi mapana ya taifa
 
Endeleeni kuziita porojo ila mjue tuu kwa style hiyo hamtoboi
Tunatakiwa tuwe na style ya kuisujudia CCM ndio tutoboe ama? Endeleeni kutegemea vyombo vya dola, siku hao wanajeshi wakibadilika tutawazika kaburi moja na KANU ya Kenya.
 
Pole hakuna mtu hapo karibu akupeleke hospitali?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…