CCM itakaa madarakani milele kwa sababu ya upinzani dhaifu

Kwa jinsi nilivyoona siasa za hii nchi yaani chama kama CCM hakitotoka madarakani. Sababu moja wapo ni upinzani dhaifu nikisema hivyo nadhani mnanielewa.
Japo ni mchungu lakini ndio ukweli wenyewe wa mambo. Tanzania hatuna any serious opposition, hivyo CCM itatawala milele. Kupata maendeleo ya kweli, Watanzania ni lazima tujifunze kuukubali ukweli!. Hili la CCM kutawala milele ni kweli!.
Tanzania hatuna upinzani wa maana Japo kazi ya upinzani ni kupinga, lakini sio kupinga kila kitu. Kwenye maslahi ya taifa, tutangulize utaifa, tuwe wamoja, wakweli na tusipotoshe
P
 
Illogical.

Hakuna kabila la wapinzani, hakuna mtu anayemiliki upinzani wala hakuna hatimiliki ya upinzani. Kama wewe unaona hivi sasa upinzani uliopo ni dhaifu na unatamani upinzani wa nguvu, basi anzisha na kuuimarisha wewe mwenyewe. You have to be the change that you want.

Kama roho yako ni kwatu huko CCM, basi achana na masuala ya upinzani, endelea kufaidi raha za chama dola.

Kama Mbowe anakukereketa, mchukulie hatua. Halazimiki kuwa mpinzani wala chochote kile. Anaweza hata kuendelea kula bata na kuwaachia wajinga msala wenu mhangaike nao wenyewe.
 
Pimbi za UVCCM huwa zinadhani UPINZANI ni kama shirika fulani la mtu, chama si mali ya mtu ni cha wote, ndio maana waanzilishi wanakufa na vinaendelea.

Tabaka nufaika na mfumo hawajali, siku wakiguswa a korodani wanatoa milio yote, refer Ole Sendeka na wengine.
 
Upinzani ni nini? Nguvu ya upinzani inatoka na nini? Mbona Kenya wameleta mabadiliko makubwa bila kuhusisha vyama vya upinzani? Nataka tu kukuonyesha kuwa tatizo la Tanzania ni wananchi na siyo upinzani.
 
CCM haiwezi kutoka madarakani kwa sababu ni chama dola na pia watanzania wengi ambao ni wapiga kura hawaelewi yanayoendelea. Wao wakishapata buku 3, kanga na muziki basi wanachukua wanaweka waaa.
Chama dola unadhani hakiwezi kutolewa? Tatizo la watanzania nakubaliana nalo na ndilo tatizo.
 
Upinzani ni nini? Nguvu ya upinzani inatoka na nini? Mbona Kenya wameleta mabadiliko makubwa bila kuhusisha vyama vya upinzani? Nataka tu kukuonyesha kuwa tatizo la Tanzania ni wananchi na siyo upinzani.
Wananchi tatizo lao nini
 
Pambana na maisha Yako mzee ccm ipo milele
 
Upinzani sio mtu, rudi shule ukasome upya.
 
Wananchi tatizo lao nini
Kukaa kimya bila kuwawajibisha viongozi wazembe. Leaders are shaped by wananchi! Ukali wa mbwa ni msasi. Wananchi wakiwa legelege viongozi nao wana-relax. Huoni yanayotokea Kenya? Jaribu kutembea duniani uone. Ulaya yenyewe kila siku kuna migomo na maandamano ya wananchi kuhusu serikali zao. Viongozi wanatakiwa kuchungwa kama ng'ombe... muda wote.
 
Ruhusuni tume huru ya uchaguzi uone kama misa ya kwanza itatoka kabla ya chama kupigwa mwereka
 
Si waweke vitu huru tu, waone kama watakaa hata mwaka mmoja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…