CCM MP has said that ATCL air hostesses are not attractive

CCM MP has said that ATCL air hostesses are not attractive

Umeona halafu ndiyo maana siku zote tunasema adui wa mwanamke ni mwanamke hebu jaribuni kupendana hata kwa uongo uongo hoja hiyo tungeileta sisi wanaume kwa sababu hatuwezi kukonyeza mabinti hawana mvuto yeye wanawake wenzake mvuto wa nini kwake nimepata mashaka na huyo mama CELLULAIRE,
 
Kuna kitu nilitaka niseme ila dah naogopa BAN, anyway huyu mama ni attention seeker na ka hit target at right time and angle,kwa akili na mitizamo ya viongozi wa aina yako tuna safari ndefu sana..


















 
Kuna mtoto wa kichagga hapo Benjamini Mkapa CRDB chini pale acha kabisa. mwaka juzi alikua pale sijui kama bado yupo au la. Yule anafaa aisee white kapanda very charming & beautiful.
Jina simjui wakaokote pale ATCL.
 
Hajawahi fika Schipol Int'l Airport kuwaona hao vikongwe wao huita nyanya wakiingia na kutoka....

Dutches wanawaamini sana vibibi

Bro nilishangaa kuona viajuza vimeongozana na mabegi Schiphol airport vikichoma ndani.
Lkn pengine kwa sababu population yao ina wazee wengi (population decay).
 
[emoji23]
Screenshot_20191108-093135_Facebook~2.jpeg
 
halafu unakuta ni mchumba au mke wa mtu huu ni uchonganishi[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Naunga mkono mbunge kwa hoja yake kwani kila kitu kina masharti hasa kazini,kwenye mchezo wa mpira mara nyingi golikipa na beki kati lazima wawe warefu kwa kimo,hivyo ajira kwenye ndege zetu ni vizuri wazingatie mvuto/urembo.Pia napendekeza hata watangazaji wa TV yetu ya taifa wa kike baadhi yao hawana mvuto wapewe kazi nyingine.
Nani kakwambia makipa wote Ni warefu, kaseja Ni mfupi


Nani kakwambia mabeki wote Ni warefu canavaro alikuwa mfupi na akachukua mpaka Balon D'or... Kelvin Yondan Ni mfupi pia
 
Mbunge wa Kigoma Kusini nchini Tanzania (CCM) Husna Mwilima amesema wahudumu wa ndege wanaoajiriwa na Shirika la Ndege Nchini (ATCL) hawana mvuto kwa wateja.

Mwilima ameyasema hayo leo Alhamisi Novemba 7, 2019 wakati akichangia Mapendekezo ya Mpango wa Taifa wa Maendeleo bungeni jijini Dodoma.

Mwilima amempongeza Rais John Magufuli kwa kutimiza ahadi yake ya kuifufua ATCL na kuwataka mawaziri pia kutimiza ahadi zao.

“Mheshimiwa waziri mimi nataka nitanie kidogo hizi ndege zetu zinafanya vizuri sana lakini mle ndani hebu tuangalie tunaowaajiri. Wale maair hostess (wahudumu) hata ukimuita mle ndani akigeuka abiria anaona kweli tuna maair hostess mle ndani,” amesema na kuongeza:

“Sijui mnatumia vigezo gani? Unakuta air hostess mfupi, hana mvuto wa kuifanya ndege zetu zionekane. Leo mimi hapa nimezeeka na miaka 50 na ukiniweka…”amesema kabla ya kukatishwa na utaratibu uliombwa na Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Musukuma.

Musukuma amesema huo ni ubaguzi na kwamba kuna wengine wanazaa watoto ambao hawana maumbo kama anayoyasema mbunge huyo.

Akiendelea kuchangia Mwilima amesema sifa ya mhudumu wa ndege ni lazima awe mrefu na amenyooka akiwa mwanaume ama mwanamke na kuomba jambo hilo lizingatiwe.


Chanzo: Mwananchi


ATCL YAJIBU, HATUAJIRI WANAWAKE KUONESHA UZURI

Wakati mbunge wa Kigoma Kusini (CCM), Husna Mwilima akisema wahudumu wa ndege za ATCL hawana mvuto kwa wateja, shirika hilo limesema haliwachagui kwa ajili ya kuonyesha sura.3

“Hatuchagui wanawake kwa ajili ya kuwapeleka kuonyesha uzuri kuna vigezo lazima tuwapime uelewa. Lazima kujua wana uwezo upi wa kufuatilia mafunzo watakayopewa ili watoe huduma inayotakiwa kwa wateja wetu na si sura,” alisema Ladislaus Matindi, mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL).






Pia soma
Duuuh jamani kumbe urefu unafaida?
 
Kumbuken hata mtu akipenda ndege haangalii Uzur au urembo Ila huduma na ukalim anaoutoa mtu...!!! Pia waweza Kuwa mzur wa kuvutia kutoa huduma ukawa hovyo...!! Au kule ndan wanatakiwa wenye mvuto wawe wanatamaniha wanaume ili wajiuze...? Achen ubaguzi wa rangi au Sula we ni mwanamke km wanawake wengne usiwakejel wenzio..!!! Huyo mbuge achunguzwe historia yake ya nyuma maana huenda....!!!! Eeeh
 
Jamani biashara ya airline ni kama biashara nyingine.Huwa zina standard zake kwa kila kitu kuanzaia chakula,ulinzi ,usalama ,mavazi nk.Na kuna vyuo au sehemu ya kutoa mafunzo kwa ajili ya vitu vyote vinavyohusiana na biashara ya ndege.Sasa ,mbunge yuko right kabisa,wale wanaoajiriwa wawe katika standards zinazokubalika kutokana na biashara yeneyewe inavyosema mfano wanataka
Physical Standards
Minimum height requirement is 157 cm (for females) and 170 cm (for males). This requirement may differ from one airline to another. Weight of the candidate should be in proportion to his/her weight. Spotless skin complexion will give candidates an edge
OR
  • Minimum age: 18 to 21 years, depending on the airline.
  • Height: 4ft 11in and 6ft 3in, or 150cm and 190cm, tall. ...
  • Weight: Just be a “healthy weight” for your height!
  • Reach: 208cm (on tippy-toes if you have to!)
  • Vision: 20/30, with or without corrective measures.
Sasa tusidanganyane hizo hapo ni baadhi tu ya standards na hizo zinawekwa ili kuweza kukabiliana pia na majanga yanayotokea kwenye ndege especiaaly kama kuna mtu either mgonjwa na anaitaji kubebwa,or kufunga cabin za ndege unahitaji mtu mrefu nk.So kuwa mrembo au la akifikia hivyo vigezo lazima atameet hiyo ya urembo.Hata namna anavyojiweka .Hivi kweli ukute ameweka "rough dread" au twende kilioni ya ajabu kabisa imefumuka left right au mawigi kama yale ya akina "wema" anafanyaje kazi lazima awe mbaya.Mbunge mimi nakuunga mkono kabisa
 
Jamani biashara ya airline ni kama biashara nyingine.Huwa zina standard zake kwa kila kitu kuanzaia chakula,ulinzi ,usalama ,mavazi nk.Na kuna vyuo au sehemu ya kutoa mafunzo kwa ajili ya vitu vyote vinavyohusiana na biashara ya ndege.Sasa ,mbunge yuko right kabisa,wale wanaoajiriwa wawe katika standards zinazokubalika kutokana na biashara yeneyewe inavyosema mfano wanataka
Physical Standards
Minimum height requirement is 157 cm (for females) and 170 cm (for males). This requirement may differ from one airline to another. Weight of the candidate should be in proportion to his/her weight. Spotless skin complexion will give candidates an edge
OR
  • Minimum age: 18 to 21 years, depending on the airline.
  • Height: 4ft 11in and 6ft 3in, or 150cm and 190cm, tall. ...
  • Weight: Just be a “healthy weight” for your height!
  • Reach: 208cm (on tippy-toes if you have to!)
  • Vision: 20/30, with or without corrective measures.
Sasa tusidanganyane hizo hapo ni baadhi tu ya standards na hizo zinawekwa ili kuweza kukabiliana pia na majanga yanayotokea kwenye ndege especiaaly kama kuna mtu either mgonjwa na anaitaji kubebwa,or kufunga cabin za ndege unahitaji mtu mrefu nk.So kuwa mrembo au la akifikia hivyo vigezo lazima atameet hiyo ya urembo.Hata namna anavyojiweka .Hivi kweli ukute ameweka "rough dread" au twende kilioni ya ajabu kabisa imefumuka left right au mawigi kama yale ya akina "wema" anafanyaje kazi lazima awe mbaya.Mbunge mimi nakuunga mkono kabisa
Huyo mbunge ana miaka 50, anamtaka mkijana mwenye mvuto wa hiyo age ya 18-21 wa nini?
 
Back
Top Bottom