CCM na wanaccm, nini kosa la Bashiru? Demokrasia kwenu ni nongwa?

Dr Bashiru bwana alikuwa katibu Mkuu wa hovyo wa ccm ambapo chama kiligeuka Mungiki na wanywa damu
 
Kosa lake ni kusema uongo katika zama za ukweli
 
Wanajua udhaifu wa sa100..mwanamke akisifiwa hufurahi na kuringa zaidi..akiambiwa mbaya hununa na kuchukia.

Soon utasikia nafasi yake imetenguliwa ama kapewa ubalozi wa somalia...ccm wengi mawazo yao yameshikiliwa na mwenyekiti.

Katiba mpya muhimu sana.

#MaendeleoHayanaChama
 
Tanzania na hasa CCM ni kundi la wanafiki. Leo hii hata ukimuweka kichaa yeyote akawa rais/mwenyekiti wao lazima wataimba na kumsifia wakisema hajawahi kutokea kama yeye tangu dunia iumbwe
 
Tanzania na hasa CCM ni kundi la wanafiki. Leo hii hata ukimuweka kichaa yeyote akawa rais/mwenyekiti wao lazima wataimba na kumsifia wakisema hajawahi kutokea kama yeye tangu dunia iumbwe
Lejea ya Pompeo alikua chizi na anasifiwa mpaka Leo pamoja na uchizi wake.
 
Hili halina shida kama unaongea nje ya mfumo kwa maana ukiwa mwanachama wa chama fulani huwezi kukisema chama nje ya mfumo wake unashida wana sehemu zao za kuongelea mambo ukitoka nje wewe ni kama Ronaldo tu. Huwezi kuwa mfano sehemu ya Yanga au Simba halafu ukatoka nje ukawasema viongozi wako mshabiki anaweza lakini wanachama wa vikao vyao. Ronaldo anafukuzwa sio kwa sababu kasema uwongo ni huwezi kuwa mchezaji ukaja nje ukaongelea ziko sehemu zake. Huyu ni mnafiki hakuna chama cha siasa duniani mwanachama akamsema mwenyekiti wake na ukabaki salama, ndani ya vikao vyao wanasemena wakitoka nje wanashikama. Atokee mtu Chadema amseme Mbowe kama atabaki salama.. angalizo tu. ukitaka kuwa huru toka baki kuwa huru ongea unachotaka
 
Dr Bashiru anyamaze kabisa. Alitumika kuumiza watu
 
Huyu ni mnafiki hakuna chama cha siasa duniani mwanachama akamsema mwenyekiti wake na ukabaki salama
Bashiru hajamsema mwenyekiti. Yeye amewataka wananchi na viongozi wengine kuacha kumsifia rais
 
Kosa la nchi hii. Ni ku apply elements za ki communist ktk utendaji wa serikali na chama.
Ktk u communist, ni kusifu na kuabudu kiongozi aliepo au chama tawala.

U communist hausadiki kwenye mawazo huria . Kenya ingekuwa ndiyo Tanzania. Ruto asingepenya dhidi Rais aliyekuepo .
 
Bashiru ni kinyonga
 
Hii nchi ina mambo ya ajabu sana, mentality zetu wengi ni za kibinafsi sana, tunaojiona malaika tusiokosea ambao tuko sharp kuwanyooshea vidole wengine.

Nimeshangaa mpaka Fatma Karume nae twitter anamponda Bashiru, anatoa kisingizio cha Bashiru kupewa ubunge na Samia kama ndio alitakiwa kufunga mdomo, a very stupid reasoning.

Huyu mwanamke anayejinadi kuijua demokrasia siku zote, leo anasimama upande wa kidikteta kumfunga Bashiru mdomo kisa alipewa ubunge na Samia?!

Taifa letu linaendeshwa kimahaba sana, na kibinafsi; hakuna wakumuamini wengi wapo kimaslahi zaidi, na maslahi yenyewe yanatofautiana kuanzia kiuchumi, mpaka kwenye mahaba ya vyama yaliyopitiliza, urafiki nk.
 
Kwa mujibu wa Dr. Bashiru huduma ama kazi hizi zinafanywa kwa kodi zetu hivyo ni haki yetu. Hatupaswi kusema "mama anaupiga mwingi" ama "asante mama". Kosa la Dr. Bashiru hapa ni lipi?
Kwani wakati wa JPM fedha zilikuwa zinatoka wapi, mbona wao wakimsifu sana tu na baadhi hata walifika kumwita Mungu (Astaghfirullah). Na Ndugai aliyoyafanya ya kuapisha wabunge gereji ndiyo demokrasia au nini?

Bora angenyamaza tu akaacha angalau miaka michache ipite kwanza na watu wamesahau.
 
😁😁😁
Your browser is not able to display this video.
 
Sasa Raisi ni nani? sio mwenyekiti wa CCM, serikali sio ya CCM. Mwamba pekee aliongea haya wakati JPM yuko hai ni Mkapa lakini wakaziba masikio, aliwaambia sifieni serikali ya CCM sio mtu maana dhamira ya CCM ni kutawala haya mambo ya kusifia mtu yalianza wakati yeye anaongoza CCM. Huyu kaingia kwenye 18 kama alivyoingia Ndungae safari imemfika utasikia tu
Bashiru hajamsema mwenyekiti. Yeye amewataka wananchi na viongozi wengine kuacha kumsifia rais
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…