CCM na wanaccm, nini kosa la Bashiru? Demokrasia kwenu ni nongwa?

Wakati wa Magufuli walitekwa wafuatao;- Mo, Gwanda, Ben Sa8, TitoMagoti, Lwajabe, Ney wa Mitego, Roma Mkatoliki, n k

Haya na wewe tutajie waliowahi kutekwa kabla ya Magufuli.
Sengondo Mvungi Dk,Holimboka dk,Mwangosi,mwandishi.
 
Serikali ya awamu ya 5 iliyoongozwa na chama cha mapinduzi (Katibu mkuu akiwa Bashiru) ilifanya maovu ambayo hayawezi kusahaulika katika historia ya nchi yetu. Namuona Bashiru huyu kuwa kwenye vita kali na Bashiru yule. Bashiru ni mnafiki sana. Anazungumza utadha si yeye aliyekuwa akitoa sifa lukuki kwa mwendazake leo anawazuiaje wanaccm kumsifia mama.

Anyways, truth be, huyu mkomunist/ msosholost ni mnafiki sana ila ukweli aliousema utabakia kuwa ukweli. Mama anaweza kuwa anapenda kusifiwa lakini hawezi kupenda kitu ambacho hakina maslahi kwa taifa. Kumsifia mama kwa matumizi mazuri ya kodi zetu hakuna maslahi kwa taifa. Hebu mama aambiwe ukweli kuwa hali ni ngumu sana kitaani. Bei za bidhaa ziko juu mno, maji hakuna ila bili za maji zipo, umeme hakuna na uchumi umezorota.

Miaka 61 ya uhuru nchi yetu yenye mito mingi na maziwa makubwa, bado ina tatizo la maji kuliko nchi zilizo jangwani. Hii ni aibu tosha kwake na kwa raia.

Namuunga mkono mnafiki.
 
Sengondo Mvungi Dk,Holimboka dk,Mwangosi,mwandishi.
Hawa hawakutekwa. Sengondo Mvungi aliuawa na wahuni, Dr. Ulimboka aling'olewa kucha na wahuni, wakati mwandishi Mwangosi aliuawa na mabomu ya polisi.
 
Uaneni tu ,we don't care ,fisiemu ni fisi
 
Yeah alikuwa madarakani hivyo hakuwa kwenye nafasi ya kukosoa bali utekelezaji.
 
Hawa hawakutekwa. Sengondo Mvungi aliuawa na wahuni, Dr. Ulimboka aling'olewa kucha na wahuni, wakati mwandishi Mwangosi aliuawa na mabomu ya polisi.
Kwani hao wakina saa8 Ninani kawadhibitisha kuwa waliuwawa na Magufuli Sio wauni?,hakuna utawala usio uwa kama utafuata Sheria za nchi hata Sasahivi watu wanauwawa kwa jina la panya lord.
 
Huyo Ndugai anajua kabisa hakutakiwa kujiuzuru lakini anazijua internal dealings za CCM zinavyofanya kazi na ameshazitumia sana tuu, kumbuka alipigwa risasi mbunge wake ,karibu na maeneo ya bunge na chini ya uongozi wake, lakini hata uchunguzi hakuwahi kufanya, asingejiuzuru nisingeshangaa kusikia speaker yuko nje kwa matibabu na usingemsikia tena, au wangemvua uanachama wa CCM na kupoteza ubunge wake na haki ya kuwa speaker, kumbambikizia kesi na kumuondolea security zote, kujizuru kwake ilikuwa ni kutetea uhai wake sio siasa
 
swadktaaa
 
Panya road ni wahalifu wa kawaida, ila watekaji ni wahalifu waliokuwa sponsored na Magufuli
 
Mbona kipindi Cha magufuli hakusema hayo na wakati watu walikua wanamsifia magu wakati na yeye pia alikua anatumia Kodi zetu .
Angekaa kimya tu nadhani kajiharibia zaidi aisee
Hapa ndio nakumbuka alichosema Einstein kwamba akili ni kile kinachobaki ukitoa ulichofundishwa.
 
Wengi wanaomkosoa Bashiru hawakosoi kwa hoja zaid ya personal attack, hawasemi kosa lake ni nini!
 
Panya road ni wahalifu wa kawaida, ila watekaji ni wahalifu waliokuwa sponsored na Magufuli
Watu wanapigwa mapanga ya kichwa na wengine wameuliwa kabisa halafu wewe unaita uhalifu wa kawaida.
 
Watu wanapigwa mapanga ya kichwa na wengine wameuliwa kabisa halafu wewe unaita uhalifu wa kawaida.
Sio uhalifu ambao ulikuwa sponsored na serikaki, tofauti na ule wa Magufuli ambaye alikuwa akituma watu kutekwa na kupigwa risasi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…