CCM rudini shule mkasome Kiswahili. Rais Samia ni mwingi wa tafsida

CCM rudini shule mkasome Kiswahili. Rais Samia ni mwingi wa tafsida

Sexless

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2017
Posts
23,683
Reaction score
55,898
20210418_203822.jpg


Maana ya neno tafsida ni utumiaji wa lugha ya adabu na heshima ili kuondoa ukali/ukakasi wa lugha na kuleta staha.

Kundi fulani la wanaCCM limeshangilia sana mama Samia aliposema yeye na JPM ni kitu kimoja. Wanasahau kuwa huyu mama mtu wa Pwani ambako kiswahili ndiyo chimbuko.

Angekuwa sawa angemtumbua Bashiru?
Angekuwa sawa angepiga marufuku uporaji wa TRA?
Angekuwa sawa angetoa Uhuru wa vyombo vya habari?
Angekuwa sawa Safari za ndege za Chato zingesitishwa?

Muungwana ukimuomba kitu akikujibu "tutaangalia" ujue kakataa.
Sasa ninyi wakoromije endeleeni kupiga makofi.
 
Kwa kifupi rais SSH ameliambia bunge lipuuze ya mitandaoni
 
Safi sana mama. Ngoma inapigwa mtandaoni inachezwa bungeni. Tena wabunge wanaicheza sana ngoma utafikiri bungeni ni sehemu ya kucheza ngoma!!!
 
Rais amesema kuna kuboresha kwenye baadhi ya maeneo. Hili ni pamoja na kubadilisha viongozi kadhaa wasiona tija. Hicho hakikwepeki hata haysti JPM mara kadhaa alibadilisha watu na taratibu, hilo ni zoezi endelevu kwenye uendeshaji wa serikali.Haina maana wanatofautiana na JPM.Ila Kimsingi,kisera na mwelekeo ni wazi atafuata nyao za JPM kasema.
 
Rais amesema kuna kuboresha kwenye baadhi ya maeneo. Hili ni pamoja na kubadilisha viongozi kadhaa wasiona tija. Hicho hakikwepeki hata haysti JPM mara kadhaa alibadilisha watu na taratibu, hilo ni zoezi endelevu kwenye uendeshaji wa serikali.Haina maana wanatofautiana na JPM.Ila Kimsingi,kisera na mwelekeo ni wazi atafuata nyao za JPM kasema.

Mwana acha kupiga mayowe, acha tuone wenyewe!

Yanini kumsemea mama. Si yupo?

Hapo mbona ni ku cheki tu na kujisemea hiiiiii!

Bashiri wape mrejesho tokea kwenye mdomo wa farasi mwenyewe.

Hiiiiii bagosha!
 
Back
Top Bottom