Uchaguzi 2020 CCM taa nyekundu na muda unawatupa mkono mtoseni Yoha baharini mpone tufani

Uchaguzi 2020 CCM taa nyekundu na muda unawatupa mkono mtoseni Yoha baharini mpone tufani

Hahahah... Yohana ni sikio la kufa. Me naomba tu hali iendelee kuwa tete. Mwisho wa siku labda yohana atatoswa tu...
CCM sikio la kufa halisikii dawa kumbukeni hadithi ya Yona kwenye merikebu pia kumbukeni hadithi ya belshaza na maandishi ya ukutani menemene tekeli na peresi chanzo cha yote haya ni Rais Magufuli.

Washauri wake wabaya wanamzamisha yeye na nyie pia.

Wenzenu kina Rais Mstaafu Mkapa na Kikwete walifanikiwa kwasababu waliamini katika kugawana keki ya taifa kwa wote nyie mnatumia falsafa ya the winner takes it all alone hamuwezi kutoboa.

Mlikosea sana kumfumbia macho Rais Magufuli alipopiga marufuku mikutano ya siasa wakati nyie mkiendelea nayo.

Tena msijifiche kwenye mambo ya ushoga hizi ni propaganda zenu za kitoto sababu kubwa ninamna jiwe alivyoendesha nchi kibabe kwa kutumia vyombo vya dola.

Kulikuwa na sababu gani ya kumpoteza Ben Saanane na Azory Gwanda au kumpiga risasi Lissu?


Kwakweli hili mmelikoroga wenyewe na mtalinywa wenyewe.
Hatuwezi kuiombea nchi na viongozi wake wakati neema yenu ni mateso yetu.

Mjue tunawaombea kila lililo baya ili mlipe uhalifu mliolifanyia taifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao sasa ni sawa na sikio la kufa yaani wanazidi kujikaanga kwa mafuta yao.
Na Cha ajabu wanahangaika na zitto lakini hawajibu hoja zake, Mimi nikitegemea hizo tuhuma ambazo wanamtuhumu zitto wangesema ya Kuwa hakuna hata moja ambayo Ni ya kweli, lakini Kama hawakanushi yaliyomo badala yake wanabaki kumtuhumu zitto maana yake Ni kwamba wanayafanya hayo na zitto kawaumbua. Siku zote ukiziba watu midomo watatafuta njia mbadala ya kusemea mawazo yao na haya ndo madhara yake. Waliamini ya kwamba haitawezekana kufahamika yanayoendelea lakini dunia Sasa inaelewa
Screenshot_20200201-181929.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu ni mwema kila wakati na atatutendea Taifa letu yaliyo mema tu. Naamini Magufuli amechokwa na kila mtu mpaka na wale waliomsaidia kuiba kura akina Lubuva, Kipilimba, Nape na Kinana. Na lazima Mkutano Mkuu umtose kama mgombea wa CCM hapo August 2020. Kama washauri wake aliamua wawe ni akina Makonda, Bashiru Ally na Pole pole badala ya wazee wetu wastaafu wenye busara na upeo basi anawajibika kwa haya yanayotokea.

Naamini kama CCM wasipomtosa 2020 tutarajie machafuko makubwa nchini kwa kuwa Magufuli hawezi akapata hata 20% ya kura za kupigwa kwa sanduku la kura. Badala yake atafanya vituko zaidi kuliko uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2019. Na wananchi hawatavumilia.

Atambue tu kuwa toka Uhuru wa Tanzania mwaka 1961 Taifa letu halijawahi kuwa na mstakabali mbovu wa kisiasa na kidiplomasia ya Dunia kama kipindi hiki. Kitendo cha Paul Makonda kuzuiwa kwenda Marekani ni ujumbe tu kuwa kuna mengi yanafuata. Mojawapo ni hili hapa;


Magufuli asijidanganye kuwa kwa vile huwa hasafiri nje ya Tanzania basi hayamhusu. Hapana, jina lake na la Kabudi, Mambosasa lipo tu kwa watu ambao hawatakiwi kwenda US, muda tu wa kutaja haujafika

Wamarekani wanazo details za udhaifu wa Serikali ya Magufuli ikiwa ni pamoja na ukiukwaji wa haki za binadamu, ukosefu wa utawala wa sheria, utekaji wa wakosoaji, kubambikia watu kesi, mauaji na ukandamizaji wa demokrasia ya vyama vya upinzani.

Magufuli asijidanganye kuwa anaweza kufanya Tanzania anavyoyaka kama anavyofanya kwenye familia yake, hapana!! Utulivu wa Tanzania una masilahi makubwa kwa nchi za Magharibi hasa US, UK na Germany. Tanzania ikitulia maana yake eneo zima la maziwa makuu limetulia. Waganda walipochafuana miaka ya 1970s walikimbilia Tanzania, Warundi na Wanyarwanda walipochafuana miaka ya 1960s nao walikuja Tanzania. Kuanzia 1960 mpaka 1990s Tanzania ilikuwa Makao makuu ya vyama vya ukombozi vya Afrika kama SWAPO, MPLA, ANC, PAC na ZANU.
Hata Wakenya mwaka 2008 walipouana ni Tanzania iliyohusika kuwapatanisha.

Nchi za Magharibi haziwezi kukubali Magufuli na Makonda waharibu amani ya nchi hii. CCM hamujachelewa mtupeni huyu Magufuli kwenye bahari kama Yona alivyotupwa alipokataa kwenda NINAWI ili chombo kiendelea na safari. Mkishindwa ataondolewa kwa nguvu na CCM itakuwa imekwisha kama iliyokwisha UNIP ya Kaunda au KANU ya Kenyatta. Uchaguzi ni wenu na muda munao, na uwezo munao.

Aka kakundi ka wasukuma hapana
 
Mimi nafikiri hoja sio kwenda Marekani, Marekani ni nchi kama nchi nyingine. Tanzania yetu itajengwa na watanzania wenyewe na sio Marekani. Hatuwezi kuwapigia magoti Marekani. Tuna imani na Rais wetu Mhe. Magufuli na viongozi wote aliowateua kwa kufanya kazi usiku na mchana kwa ajili ya nchi yetu. Watanzania tuache fikra tegemezi, tuchape kazi.

Upumbavu mtupu. Foolish
 
Mbona unazunguka kueleza sababu? Sababu au hizo Haki zinazotajwa ni mambo ya ushoga, uko tayari tushangilie haki za mashoga? Kuweni wawazi tu! Hakuna haja ya kuzunguka. Tena iwe jukwaani maana sasa munazomea bila hata kujua maana yake ni nini.
Hivi Mzee watu hawawi abducted? Hawapotezi maisha yao? Hawafungwi just because they criticize the government? Kwanini haya mambo yamezidi utawala huu? Unaona sawa damu za watu kumwagika kwa sababu za kipuuzi? Criticizing the government? Tuwe na busara na hekima, Mimi sitetei marekani, I just want to live in peace in my own country, criticize the government and praises it when it deserves, tunauwana kwa sababu IPI? Tunafungana magereza indefinitely kwa sababu zipi? Tito kijana mdogo mmemuweka ndani kwa sababu za kutunga tu just bcz anai criticize government on Twitter? Mkipotezea reli haitafika. Dodoma? Iam done...msituchoshe!
 
Naona watu wanajadili zuio la Makonda kuingia Marekani badala ya kujadili sababu zilizopelekea hilo zuio. Wenye akili ndogo wameanza kusema "Kwani Marekani ni mbinguni? Kwani asipoenda atapungukiwa nini?" Hii ni comment ya Mbunge mmoja wa CCM kule Twitter.

Lakini hoja si Makonda kuzuiwa kuingia Marekani au kuingia Chato. Hoja ya msingi ni madai yaliyotolewa na Marekani kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na Makonda.

Pamoja na mambo mengine, Pompeo amesema Marekani ina USHAHIDI kuwa Makonda ameshiriki KUDHULUMU HAKI YA KUISHI KWA WATU KADHAA. Hii ni kauli ngumu sana, inayotafakarisha sana.

Kudhulumu haki ya watu kuishi means kuamua kumuondolea mtu uhai kabla ya wakati wake. Je ni kweli Makonda amefanya hayo? Kwa akina nani? Kwa ruhusa ya nani? Kwa sababu gani? Lini? Wapi? Na kwanini?

Kumbuka taifa lenye teknolojia kubwa kama Marekani linaposema lina USHAHIDI juu ya jambo fulani bila shaka limejiridhisha vya kutosha.

Kwahiyo ili tuwe na mjadala wenye tija tuachane na kujadili zuio, tujadili sababu zilizopelekea hilo zuio. Hata kama asingezuiwa kwenda Marekani, lakini tuhuma alizotajwa nazo ni kubwa sana. Zinaogofya, zinatafakarisha, zinatisha. Kumbuka Marekani imesema ina USHAHIDI na kumbuka Pompeo alikua Mkurugenzi wa CIA kabla ya kuwa Waziri.!
Sikio la kufa halisikii dawa. Usijeshangaa mtu tofauti akawajibishwa ili kumlinda mtu fulani. Nchi yetu iko kwenye giza nene.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
safari ya magufuli kwenda the hague bila kulipa nauli imewiva. kucheza na mabeberu ni kucheza na moto. time will tell.
 
Mkuu umesema kitu sahihi kabisaaa..
Hii nchi kuna wajinga wengi waioelewa lolote hapa duniani Ila ukiangalia Kwa jicho la tatu tunapata picha kuwa hii message imefika Kwa magufuli mwenyewe kuwa DUNIA imemvua nguo Kwa matendo alivyofanya,Kwa akili za kawaida haiwezakani Mkuu wa mkoa afanye unyama na ugaidi alafu ikulu isijue!!

America wametumia indirect speech Kwenye suala hili.PIN iliyowekewa MAKONDA ni ya serikali yote ya magufuli
Ni watu wachache kwenye akili tu.watagundua kuwa US wamemtarget magu. Kupitia kwa bashite
 
Back
Top Bottom