Uchaguzi 2020 CCM Vijijini Tundu Lissu ametikisa ngome ni muda wa CCM kubadili itikadi na mikakati

Uchaguzi 2020 CCM Vijijini Tundu Lissu ametikisa ngome ni muda wa CCM kubadili itikadi na mikakati

Mkutano wa Tundu Lissu huko Tunduru leo umenifanya nibadili taswira ya chama chetu ccm kuwa lazima sasa tubadilishe mfumo mzima wa itikadi na mawazo juu ya wananchi wa vijijini.
24 October 2020
Tunduru, Tanzania

LIVE # TUNDU LISSU ASEPA NA WAKAZI WA TUNDURU MAELFU WAJA KUMLAKI

 
Mkuu sidhani kama wewe ni mwana ccm

Unaleta mipasho na taarabu tu ,Kuna muda yapasa utumie kichwa chako kufikiri sio kukibeba kichwa juu ya mabega kama mzigo sawa na mizigo mingine

Mkuu hapa sio Facebook au Instagram hapa kuna wataalamu ,wabobezi na wasomi ,Ujinga wako peleka Facebook huko,Hapa ni takwimu na data zinaongea

Poroja na ujinga waachie wana ccm wa facebook huko

Sisi wana ccm wa JF ni wasomi na wataalamu wa report na tumefanya kazi duniani huko ,kwanini unaleta ushamba na ujinga ?

Waanzilishi wa chama ccm Mwalimu Nyerere alikuwa anajenga hoja na alishawishi watu tutafute uhuru

Hotuba ya kikwete akiwa Mwalimu Nyerere Memorial university alieleza kuwa Mwalimu Nyerere hakuogopa hoja na hoja hazipigwi lungu

Wewe unajiita mwana ccm huna kazi hapa JF zaidi ya kuleta ngonjera,mipasho na taarabu

Jaribu kushauri Chama nini kifanyike na wapi kunahitajika maboresho

Taarabu,Mipasho,Ngonjera ni mambo ya kiswahili na kishamba sana

Tushauri chama
Msamehe tu huyo kichwani hamna kitu kabisa na hajielewi ,ana miaka 34 lakini Bado analala sebureni kwa dada yake huyo ni mzigo kwa familia na nchi pia
 
Msaliti wa Nchi Lissu anasimama stend na sokoni
Hakuna mtu atapoteza muda kwenda kusikiliza matusi
Mkuu kwa hoja hii dhaifu nimeona ni busara zaidi nikae kimya.Lissu anaenda sokoni na stendi?Hivi mikutano na viwanja vya kufanyia mikutano so vinawekwa kwenye ratiba na NEC?Au NEC ndo wanampangia sokoni na stendi?
 
Mkuu kwa hoja hii dhaifu nimeona ni busara zaidi nikae kimya.Lissu anaenda sokoni na stendi?Hivi mikutano na viwanja vya kufanyia mikutano so vinawekwa kwenye ratiba na NEC?Au NEC ndo wanampangia sokoni na stendi?
20201024_210143.jpg
 
Wanabodi,Siku nne kabla ya uchaguzi ngome zetu wana CCM hasa vijijini zimechakazwa na kutikiswa na Tundu Lissu.

Wilaya ya Tunduru Ruvuma, Mambo sio mambo ni ngome yetu wana CCM lakini wananchi wa miaka mitano iliyopita sio wananchi wa mwaka huu 2020 wamebadilika na kutugeuka kabisa.

Hii wilaya ni picha au taswira tosha kuwa sasa kunakoitwa vijijini sio vijijini tena kuna werevu na waelewa wengi kuliko mtazamo wetu ndani ya chama chetu CCM.

Mkutano wa Tundu Lissu huko Tunduru leo umenifanya nibadili taswira ya chama chetu ccm kuwa lazima sasa tubadilishe mfumo mzima wa itikadi na mawazo juu ya wananchi wa vijijini.

Mosi, CCM ikishinda na tutashinda ni muda wa kuanzisha siasa za usawa ,Maeneo tuliyoyaita vijijini leo sio vijijini tena kwani yana michanganyiko ya watu kutoka mijini hivyo madhara ya mitazamo juu ya CCM imetapakaa kila kona.

Pili, Uelewa wa wananchi umeongezeka sana kutokana na teknolojia ya mawasiliano hasa simu za mikononi hivyo imepelekea watu kujua ukweli halisi wa nchi inavyoendeshwa. Haya ndio madhara ya shule za kata kwa ccm wale wanafunzi hata kama wengi walipata sifuri lakini kuna kitu waliondoka nacho kidogo shule ambacho wanawaeleza ndugu na jamaa huko vijijini.

Kuanzia mwaka 2021 kuelekea mwaka 2025 ni muda wa kuanzisha mahusiano mema kwa kila chama na kurudisha furaha kwa wananchi tena. Madhara ya chuki yameshaonekana huko vijijini kwa wananchi kuanza kukisaliti chama cha mapinduzi.

Kuanzia 2021 ni muda wa kuwa waumilivu na kuruhusu hoja mbadala, Tuache watu waongee ya moyoni, wataongea kwa hasira lakini usiku watalala, Baada ya miaka mitano hawatakuwa na kinyongo kama sasa ambapo wanakwenda kutuadhibu mpaka wilaya kama Tunduru porini huko.
Tunduru hii sio ya miaka ya 90,useme ni kijijini.. ni moja ya wilaya kongwe. Imepiga hatua sana.
 
Kwa ubabe 90% tumezibwa midomo..Lissu pekee ndie anaweza kuongea ukweli nchi hii..Na walidhani kwa kukandamiza Wangeshinda 100% ..Kumbe nchi c ya mmoja..28-10 nnajambo langu privatini
 
Unamaanisha huyu ndo awe rais wa JMT!!?? over my dead body.
FB_IMG_1603530344092.jpg
 
Mleta mada umeandika vitu vya msingi sana, jambo moja pekee ninaloweza kukukosoa ni kuhusu namna ya kuirekebisha CCM.

CCM imeshafika kilele cha juu kabisa cha ulevi wa madaraka (ni level ya umateja) inaamini inaweza kufanya jambo lolote na hakuna mtu yoyote duniani mwenye uwezo wa kuwazuia. Kiwango hicho cha ulevi wa madaraka huwezi kukirekebisha kwa njia ya kukishauri au kukionya, njia pekee ni kukiadhibu vikali. Na adhabu pekee ni kukitoa kwanza madarakani, kipumzike (kiende soba) huko ndio kinaweza kujirekebisha.
 
Back
Top Bottom