Pre GE2025 CCM yamchagua Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza katika Uchaguzi wa Oktoba 2025

Pre GE2025 CCM yamchagua Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea Mwenza katika Uchaguzi wa Oktoba 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mpango alikataa dp world wasiuziwe nchi ugomvi ulianzia pale

Mpango aligoma kabisa waarabu kuuziwa nchi akaambiwa jiuzulu akagoma

Akaanza kunyimwa na safari za kumwakilisha Rais akawa anapewa majaliwa

Huyu mama alitendewa vyema na magufuli ila anawatendea vibaya wenzake

God is watching
Vip swala la URAIA unalifahamu mkuu?? Unalikumbuka speech ya mkuu wa majeshi wakati anamaliza muda wake?? Kabaki jamaa naye atashangazwa soon

Kimsingi Kuna nchi haiamini yanayoendelea🤣🤣🤣🤣
 
M

Mkapa aliwahi au kikwete aliwahi badilisha Gharib Bilala na Dr Shein
Mkapa alibadilisha kwa sababu Dr. OMARY ALLY JUMA alifariki mwaka 2001 au 2002 namba yake ikachukuliwa na Dr. Alli Mohamed Shein, Kikwete alifanya sub ya Dr. Alli Mohamed Shein baada ya kusajiliwa kugombea Zanzibar mwaka 2005 na namba yake ikachukuliwa na Dr. Gharib Bilal.
 
Yule wa Zanzibar kwahiyo anaemda awamu ya tatu, hii kikatiba imekaaje?
 
Mwenyekiti ndiye anaamua, siyo katiba wala ilani.

Kila kitu kimeenda tofauti na matarajio ya wajumbe.

Walidhani walienda kufanya maamuzi, hawakujua walienda kupewa maamuzi kutoka juu.
Yani inashangaza, wajumbe wengi hawajapenda
 

Hiyo ndio habari mpya toka mkutano Mkuu wa CCM Taifa kuwa Dkt Emmanuel Nchimbi ndio Mgombea mwezi wa CCM katika Uchaguzi Mkuu Ujao.

Mabadiliko haya yatakuwa na effect kuanzia mwezi July baada ya Bunge kuvunjwa hivyo Dkt Mpango na Dkt Emmanuel Nchimbi wataendelea katika nafasi zao hizo hizo.
===

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameridhia kwa kauli moja kumpitisha Katibu Mkuu wa CCM Taifa Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa Mgombea mwenza (Makamu wa Rais) kwa Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu wa 2025.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambaye pia ni mgombea urais, Samia Suluhu Hassan alimpendekeza Katibu Mkuu wa chama hicho, Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa mgombea mwenza katika uchaguzi utakaofanyika Oktoba 2025 baada ya Makamu Wa Rais, Dkt. Philip Mpango kuomba kupumzika.

Soma: Breaking News: - Uchaguzi 2025 - Dr. Mpango aomba apumzike kuwa Makamu wa Rais, Rais Samia aridhia ombi hilo

Dkt. Nchimbi aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM Januari 15, 2024 katika Kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho kilichofanyikia Unguja, visiwani Zanzibar.

Dkt. Nchimbi alichukua nafasi iliyoachwa wazi na Daniel Chongolo aliyejiuzulu Novemba 29, 2023.

Rais Samia amempendekeza Dk Nchimbi leo Jumapili, Januari 19, 2025 katika mkutano mkuu maalumu jijini Dodoma.

Chama Dola ..
 
Mkapa alibadilisha kwa sababu Dr. OMARY ALLY JUMA alifariki mwaka 2001 au 2002 namba yake ikachukuliwa na Dr. Alli Mohamed Shein, Kikwete alifanya sub ya Dr. Alli Mohamed Shein baada ya kusajiliwa kugombea Zanzibar mwaka 2005 na namba yake ikachukuliwa na Dr. Gharib Bilal.
Kwa hiyo sub sio kitu kigeni
 
Back
Top Bottom