CCM yamfukuza uanachama Bernard Membe, Kinana apewa karipio kali huku Makamba akitoka salama

CCM yamfukuza uanachama Bernard Membe, Kinana apewa karipio kali huku Makamba akitoka salama

Habari zinazoenezwa kila mahali ni kuwa nchi imepata maendeleo makubwa kwa miaka hii minne. Mtu tunayeambiwa ameyaleta haya yote anamwogopa nini mtu ambaye katika miaka hiyo minne alikuwa tu nyumbani kwake hajaleta maendeleo yoyote? Hivi hawa wawili wanaweza kushindanishwa uzani mmoja? Sasa hofu ya nini mbona mimi sielewi?
Au labda tunayoambiwa ni mafanikio siyo kweli?
hawa ndugu walitofautiana kambi toka wakati uleee! mmoja alikuwa timu Membe ambaye ni Membe mwenyewe mwingine alikuwa timu Lowasa na ukiangalia timu Lowasa wote wanarudi kundini. hawajawahi kukubaliana na sasa inaonekana timu Lowasa wananguvu katika chama (hii ni kwa jinsi nionavyo mimi)
 
kama ni mshindi ahamie ACT watu wakutane kwenye ballot paper, mi nimefurahi sana, jamaa alikuwa akijimwambafayi mno....aanzishe chama chake aone kama wale waliokuwa wakiongea chobis watamfata huko.
Ni dhahiri Membe wamefukuza kwa sababu wamemwogopa..

Kwa hili Membe ni mshindi.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dunia hugeuka sana leo Membe kafukuzwa chamani na Pole Pole siku nyingine ni Mwingine ha haaa
 
Sasa Chdema wampokee na kumsafisha, then Magufuli atatangaza kumsamehe, Finally anaunga Mkono Juhudi, hapo Chadema watadai walimshtukia tomea mwanzo.
 
ukweli ndo huo hakuna sababu ya msingi athari zake wataziona mbeleni
Leo hii ukimuuliza mwanachama yeyote wa CCM kwanini Membe kafukuzwa hana jibu. Magufuli kamfukuza kwa chuki binafsi kwa kuwa membe ni mpinzani wake ndani ya chama. Wana CCM kuweni makini sana magufuli kaiweka CCM mfukoni mwake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makada wa CCM ni wakati sasa wakutubu na kusimamia haki na kuacha mambo yenu ya gizani gizani.
Makada wa CCM ni wakati sasa wakuisimamia Tanzania sio CCM, Tanzania kwanza CCM baadaye.
CCM lazima mtambue CCM ni genge la watafuta maslahi, na kila wakati lazima magenge haya yatofautiane.
CCM kwa sasa ina genge jipya linalojaribu kupambana na magenge mengine, Genge moja lakina Rostam na El tayari limeshacompromise na maslahi yao yamehakikishwa, Genge lingine lakini Membe limeleta jeuri na halitaki kucompromise zaidi ya ofisi kubwa hapo mziki ndio ulipo na anayeumia ni Tanzania na Watanzania.

Ni ukosefu wa akili mtu timamu kusimama mbele za watu na kuiambia dunia eti CCM ni taasisi imara inayojielewa, labda kama unaongozwa na hisia za ushabiki na wewe ni mnufaika wa magenge maslahi ya siasa za CCM na Bongo kiujumla.

Ni wakati sasa wa Watanzania kustuka na kuachana na hili Genge la CCM na baadala yake nchi iende kwa magenge mengine ili heshima irudi kwa wananchi. CCM aiheshimu tena utu wa WAtanzania zaidi ya maslahi ya CCM na watu wake..
Samurai ukimusikiliza Sumaye baada ya kutoka Chadema nako ni mchang'anyiko pia sasa Wa Tz twende wapi au ni wapi penye unafuu?
 
Kosa la membe ni lipi? Au na wewe maamuma unafuata mkumbo kwa sababu magufuli kaamua?
Hii ndiyo CCM, ni chama ambacho hakuna mwenye hati miliki, ni chama cha wananchi! Hakuna mkubwa au mzoefu ndani ya chama, ukikosea utaonywa, ukishupaza shingo lazima wakufukuze uanachama. Mzee Membe kama anatumika basi wanaomtuma hawakuwa na nia njema naye. Sasa ataucheza mpira nje ya uwanja maana hata mkia wake umekatwa kweli kweli.
 
Katika siasa za Afrika ni chama kimoja tu cha kijamaa kimebaki na nguvu na hiki ni CCM bila shaka! Nguvu kubwa ya vyama hivi ilikuwa ni Chama KUSHIKA HATAMU! Na katika KUSHIKA HATAMU vyama hivi kupitia propaganda vilizalisha wafuasi wajinga wengi sana!ambao wao huwaambii kitu kuhusu VYAMA VYAO! Vanguard Party!
Bahati mbaya sana Dunia ya KILIBERARI inakua kwa kasi ya ajabu ! Hata CCM Kuendelea kuwepo hai/Imara hadi leo kulinganisha na wenzake kama UNIP,MPLA ni matokeo ya akili kubwa ya Nyerere!
Lakini tunakoelekea, nguvu ya ushawishi wa CCM inapukutika kwa kasi,kutokana na nature' ya viongozi wa sasa na hali ya kisiasa ya leo,ndio maana tunashuhudia CCM ikichagua viongozi kwa kupima upepo na Sio wale makada waliondaliwa ,hata hii ya kuchukua viongozi wa upinzani inadhihirisha kuishiwa pumzi kwa Vanguard Party!
Kwa hiyo siku chache zijazo tutegemee kupungua kwa nguvu za CCM,na kuibuka upinzani imara ambao kama alivyotabiri Nyerere utatoka ndani ya CCM!
Mtikisiko huu ulianza polepole kipindi cha Lowasa na sasa anakuja Membe!
Mwisho tutafikia kama Kenya ambako wanasiasa wanatambaa kama Kambale kwenye dimbwi!
Na ikifikia hatua hii ndipo utaona umuhimu wa Katiba ya Wananchi kama alivyopendekeza Jaji Warioba!
 
Haya mambo ni ya kisiasa zaidi, hao upinzani waendelee na yao na mikakati yao huyo asubiri uchaguzi upite ndio ajiunge na kama watampokea basi asipswe nafasi ya ushauri na si kugombea kama yule mwingine.
 
Back
Top Bottom