CCM yatoa Baraka zote kwa DP World kufanya uwekezaji wa Bandari

CCM yatoa Baraka zote kwa DP World kufanya uwekezaji wa Bandari

Kwa kuwa unajua kiasi kikubwa hicho atakachowekeza, ambacho ni nje ya kiwango kilichowekwa kwa Sheria, Kanuni na Taratibu zetu za uwekezaji, ITAPENDEZA ukikitaja humu JF.

Je, unakielewaje KIFUNGU CHA 4: UPEO WA USHIRIKIANO NA VYOMBO VYA UTEKELEZAJI, kifungu kidogo cha 5. DPW na taasisi tanzu zitawajibika kutafuta ufadhili kwa Makampuni ya Miradi husika kwa ajili ya kuendeleza Shughuli za Miradi.?

Kwenye kifungu kidogo hicho, DPW itatumia Makampuni mengine kutekeleza miradi bandarini, Je, JMT haina uwezo na ujuzi wa kutafuta makampuni kwa miradi ya kuboresha bandari, ikiwekeza kupitia wafadhili?

Kutokana na kifungu hicho, na kwa hoja yako kuwa uwekezaji wa DPW utakuwa mkubwa, wakati itahitajika kutafuta wafadhili, Je, ni nani mwenye uhalali wa kufadhiliwa kati ya nchi (JMT) au kampuni (DPW)?

Nawaza pia kwa sauti na kuuliza, Je, nchini hakuna wawekezaji wa nje, km wa madini, ambao pia gharama za uwekezaji ni kubwa?
Mkuu hao DP wamekubali kuja kuendeleza sekta nzima ya bandari. Kutoa utaalam wa masuala ya uendeshaji kwa chuo cha bandari DMT. Kuongeza uwezo wa wafanyakazi wa bandari pia ni jukumu lililoandikwa kwenye mkataba.

Pia kuendeleza kitengo cha majahazi ambacho ni kama kimekufa pale TPA. Wanakuja na mengi ya kisasa ambayo hatunayo muda huu.

DPW wapo mpaka Uingereza na Marekani, unauliza nani mwenye haki ya kufadhiliwa kati ya Tanzania na Dubai?. mkuu punguza masihara.

Huwezi kujenga reli ya SGR yenye kula matrilioni ya pesa halafu uwe na bandari yenye ufanisi ule ule wa kizamani wenye kuwapa mianya wapigaji na wazembe wanaozoea maisha rahisi ya wizi hapo bandarini.

Ni changamoto mpya kuipokea hii kampuni kwa maana ya kwenda sambamba na dunia isiyotusubiri mpaka tuamke vichwani.
 
Hii hoja ingekua na mashiko kama ungeleta fact kua DPW anawekeza kiasi gani kinachomfanya yeye kua mwekezaji wakipekee zaidi ya apo maneno yako yanabaki kua ni mtazamo wako na ayana maana yeyote
Kwenda bungeni Dodoma ili azimio la uwekezaji wake lipitishwe na bunge ni taarifa tosha kabisa ya ukubwa wa kampuni waliyonayo.
 
ni kutafutie trillions ngapi kwani unanilipa ? huwezi kutafuta mwenyewe serikali itategemea kupata shillingi ngapi kila mwaka kwenye hizo bandari ambayo ndio price watanganyika have to pay!....kama hunielewi tulia, usinipotezee muda na kichwa chako kama cha konokokono...
Huu ni uwekezaji na hakuna price yoyote ya kulipwa na yoyote. Huu unaoitwa utanganyika ni siasa zilizofilisika zinazotumiwa na huyo Mwabukusi ambazo zinawapata watu wasiofikiria kwa kina.

Ufanisi na utendaji mzima wa bandari unakwenda kubadilika kwa faida ya hao hao wanaojiita watanganyika.
 
Kama hauna "kipawa" cha uongozi utaujuwaje "uongozi" mpaka uweze kusema wenzako hawawezi?
Mungu wangu mbona swali lako ni la kitoto sana. Uongozi siyo udaktari. Naishi ndani ya Jamhuri na mlipa Kodi mzuri najua pale jamii yangu inapokuwa na uongozi mbovu. Sihitaji kuwa na kipawa cha uongozi kujua hilo.
 
Yaani mwenyekiti wa CCM (ambaye pia ni rais, Samia) amempa baraka rais wa Tanzania (ambaye ndo huyo huyo mwenyekiti wa CCM, Samia) kuendelea na uwekezaji wa hawa DP world pale bandarini.!!!

Yaani kwamba tulitegemea SAMIA amgomee SAMIA kuwakubali hawa DP world..!!!

TANZANIA SIHAMI NG'O..!!
Hapo amepata baraka ya CCM nzima ya kuendeleza bandari. Hao kina Mzee Warioba, Mzee Shivji na Mzee Malecela ni sehemu ya CCM nzima.

Ni majibu kwa mitazamo tofauti ya watu wa ndani ya chama. Kwamba kaanza kwanza na chama chake.
 
Huu ni uwekezaji na hakuna price yoyote ya kulipwa na yoyote. Huu unaoitwa utanganyika ni siasa zilizofilisika zinazotumiwa na huyo Mwabukusi ambazo zinawapata watu wasiofikiria kwa kina.

Ufanisi na utendaji mzima wa bandari unakwenda kubadilika kwa faida ya hao hao wanaojiita watanganyika.
Ni huo ufanisi ambao utaingiza hizo trillions ndio zilimfanya mama akauza bandari zetu kwa muda usio na kikomo,, hii ni price watanganyika have to pay,ni bandari za Tanganyika tu ndizo ziko kwenye hayo makubaliano na sio za zanzibar unajuaje kama watanganyika ndio wanufaika na sio wazanzibar?
 
Hapo amepata baraka ya CCM nzima ya kuendeleza bandari. Hao kina Mzee Warioba, Mzee Shivji na Mzee Malecela ni sehemu ya CCM nzima.

Ni majibu kwa mitazamo tofauti ya watu wa ndani ya chama. Kwamba kaanza kwanza na chama chake.
Kuna mwana CCM wa kumgomea mwenyekiti wake? Atafukuzwa uanachama asubuhi na mapema..!!! Hayo ya kusema amepata majibu ya watu ndani ya chama NI UNAFIKI KAMA UNAFIKI MWINGINE TU..!!!
 
Uelewa tu unakusumbua nenda Israel mwaka jana wao wameiuza kabisa bandari yao Haifa port kwa Adani group kwa bilioni 1.2 USD .unataka kuniambia waisraeli hawawezi kuijenga nchi yao?View attachment 2683361
Kwa nini mnatolea mifano kwa Nchi ambazo unaona wametangaza hata bei haya huku kwetu imeuzwa kwa bei gani na kwa muda gani ukiona mzungu kaingia mkataba anakua kakagua vitu vingi sana sio sawa na mswahili asiejua kusoma na kuandika umasikini upo kwenye damu wanafanya vitu sio kwa ajili ya vizazi vijavyo ni kwa ajili ya wakati wa sasa...
 
ni kutafutie trillions ngapi kwani unanilipa ? huwezi kutafuta mwenyewe serikali itategemea kupata shillingi ngapi kila mwaka kwenye hizo bandari ambayo ndio price watanganyika have to pay!....kama hunielewi tulia, usinipotezee muda na kichwa chako kama cha konokokono...
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] Anita hoja haipigwi rungu
 
Mkuu hao DP wamekubali kuja kuendeleza sekta nzima ya bandari. Kutoa utaalam wa masuala ya uendeshaji kwa chuo cha bandari DMT. Kuongeza uwezo wa wafanyakazi wa bandari pia ni jukumu lililoandikwa kwenye mkataba.

Pia kuendeleza kitengo cha majahazi ambacho ni kama kimekufa pale TPA. Wanakuja na mengi ya kisasa ambayo hatunayo muda huu.

DPW wapo mpaka Uingereza na Marekani, unauliza nani mwenye haki ya kufadhiliwa kati ya Tanzania na Dubai?. mkuu punguza masihara.

Huwezi kujenga reli ya SGR yenye kula matrilioni ya pesa halafu uwe na bandari yenye ufanisi ule ule wa kizamani wenye kuwapa mianya wapigaji na wazembe wanaozoea maisha rahisi ya wizi hapo bandarini.

Ni changamoto mpya kuipokea hii kampuni kwa maana ya kwenda sambamba na dunia isiyotusubiri mpaka tuamke vichwani.
Hoja yangu haihusu bandari kutokuboreshwa, ikizingatiwa uwezo na ufanisi wa SGR.

Pia hoja siyo ukubwa na uwezo wa DPW kuendesha bandari.

Sababu hizo 2 ndio msingi wa utetezi wa uwekezaji wa DPW kupitia mgongo wa nchi yao, Emirate ya Dubai, bila kutilia maanani vifungu batili vya makubaliano (IGA). Yaani tuko wanyonge ("hopeless") kiasi cha kuingia aina hiyo ya makubaliano. Mimi, na wenye mawazo kama mimi, nasema HAPANA.

Kuna njia sahihi za "nipe-nikupe" ("win-win situation") kuboresha bandari zetu, ikizingatiwa nchi ilivyo na utajiri wa rasimali. Nimetoa mapendekezo kadhaa, ambayo unakwepa kuyahoji, km JMT kutafuta mitaji na kutumia makampuni yenye uwezo, ikiwemo DPW, kuboresha bandari zetu kwa masharti yetu wenyewe kuliko kujiona wanyonge wa kujisalimisha kwa makubaliano yenye kudharilisha.

HAPANA kwa hayo makubaliano (IGA). Serikali iandae kongamano, wadau tujadili yaliyomo kwenye IGA.
 
Povu kama lote!
Mtateseka sana mwaka huu ikiwa ndo mtaishia humu nyuma ya keyboard.
If you're really serious tokeni humu mchukue hatua, otherwise nyie ni debe tupu mwajichosha tu
Mawakili wameshafungua kesi ya kikatiba......ni mwanzo mzuri
 
Hamashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) iliyokutana katika kikao chake cha kawaida makao makuu ya chama hicho jijini Dodoma leo Jumapili, Julai 9, 2023, chini ya Uenyekiti wa Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na mambo mengine imejadili mkabata wa makubaliano ya uwekezaji na uendelezaji wa bandari nchini.

Mkataba huo ni baina ya Serikali ya Tanzania kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) na Serikali ya Dubai kupitia Kampuni yake ya Dubai Port World ambao tayari Bunge la Tanzania limeridhia ushirikiano huo.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Sophia Mjema amewaambia waandishi wa habari kuwa, Halmashauri Kuu imepokea na kujadili kwa kina taarifa ya makubaliano ya uwekezaji na uendeshaji wa bandari na kuazimia ifuatavyo; uwekezaji na uendeshaji wa bandari ni kwa manufaa ya uchumi wa nchi.

Uwekezaji huo ni utekelezaji wa vitendo wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020–2025, ibara ya 59, ukurasa wa 92. Serikali iongeze kasi ya kutoa elimu kwa wananchi juu ya uhalisia uliomo katika makubaliano ya uwekezaji na uendeshaji huo wa bandari,” amesema Mjema.

=====
Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC) imepokea na kujadili kwa kina taarifa ya makubaliano ya uwekezaji na uendeshaji wa bandari baina ya Serikali ya Tanzania na ya Dubai wakibariki mchakato huo.

Katika kikao chake kilichoketi makao makuu ya CCM, jijini Dodoma leo Jumapili Julai 9, 2023 chini ya Mwenyekiti wake, Rais Samia Suluhu Hassan, kikao hicho kimesema uwekezaji na uendeshaji wa bandari ni kwa manufaa ya uchumi wa nchi.

Taarifa fupi iliyosomwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema mbele ya waandishi wa habari ilesema uwekezaji huo ni utekelezaji wa vitendo wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/25, Ibara ya 59, ukurasa wa 92.

Hata hivyo, Mjema amesema kikao kimekubaliana kuwa, Serikali iendelee kutoa elimu kwa kwa wananchi katika jambo hilo.

"Serikali iongeze kasi ya kutoa elimu kwa wananchi juu ya uhalisia uliomo katika makubaliano ya uwekezaji na uendeshaji huo wa bandari," amesema Mjema.

Halmashauri hiyo ilifanyika baada ya kutanguliwa na kikao cha Kamati Kuu ambapo pia imezipongeza Serikali zote mbili za Chama Cha Mapinduzi, Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Hussein Ali Mwinyi.

Katika mkutano huo na waandishi, Mjema amesema siyo siku ya kujibu maswali kwani yeye amesoma kile ambacho wamekubaliana na Halmashauri na mambo mengine yasubiri wakati wake.

Pia soma: Dodoma: Bunge lapitisha azimio la kuunga mkono mkataba wa Tanzania na DP World
DOKEZO - Malalamiko ya mkataba wa DP World yapelekwe CCM, Rais Samia hana makosa sababu anatekeleza sera za chama chake
Mwenyekiti wa Kikao alikuwa ni nani?
 
Back
Top Bottom