CDC Africa: Vipimo vya Corona Virus vinavyotumika Tanzania vinafanya kazi vizuri

Neno beberu katika ubora wake au ujinga wake.

Kila mwenye maoni tofauti na Mh.Raisi Magufuli ni beberu?

Hivi na huyo Jack bilionea wa kichina alietoa msada wa test kits za Corona kwa taifa letu amegeuka beberu?

Huyo Bosi wa kimataifa kwa Africa Disease control center nae ni beberu kwa kuwa hakuunga hoja ya Raisi Magufuli?
Ni sifa gani inahitajika hadi binadamu mwenzako umwite beberu?

Miaka ya 60 kulizuka maneno yenye lugha kama hiyo kila kosa la uwajibikaji kwa nchi za kikominist walisingizia nchi za magharibi. Je tunarudi huko?Lakini mbona matendo ya watawala sio ya kijamaa?

Kwa mwendo huu hatumsaidii Raisi au Taifa letu.
 
Tunaambiwa Raila pia "beberu". Kisa amekosowa wakubwa.
 
Wewe ndio huelewi, acha kulazimisha tumuelewe. Rais ana taasisi zote za kuchunguza, kwa hiyo kama shida ni wataalam angejua tu kwa kutumia mashushu wake na kama ni hizo testing kits au machine pia angejua kwa kutumia mashushu haohao.

Sasa unafukuza watu halafu ndio unaunda tume ya kuchunguza, Vyombo vyetu vya usalama/Tiss vinafanya kazi gani??


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili jamaa la Africa CDC bonge la dunderhead!

Unajuaje hakuna manufacturing defect ?

Hata ukinunua gari jipya Japan, zero mileage, halafu ukawapigia simu baada ya wiki mbili kwamba gari lenu bovu, hawawezi kukubishia "hilo gari ni zima!!!!

Wakati wewe consumer ndio unacho chombo mkononi na una experience chombo kibovu!
 
Hata ingekuwa mimi ninge reject pia.
Hivi kweli mtu unaweza kwenda porini kukimbizana na kware ili upate sample ya kuwategeshea lab technicians! Hivi mapapai na mafenesi na kipimo cha RNA ya kirusi cha Corona wapi na wapi. Hii quality assurance na quality control ya wapi?

Yaani wenzetu wako busy kupambana na ugonjwa kwa kuchukua decisive measures. Sisi tunapima mbuzi, kondoo na mafenesi.
 
Mkuu tofautisha kati ya kusimamishwa na kufukuzwa,kiufupi hao wataalamu wamesimamishwa ili kupisha uchunguzi wakionekana hawana hatia watarudishwa kazini,

Taratibu za kazi zinataka ikiwa mtu anachunguzwa kuna ulazima wa yeye kukaa pembeni ili asivuruge zoezi zima la uchunguzi
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo Rais wetu haoni shida ofisi kupotezewa heshima?

Yeye angeyaacha haya mambo kwa wataalam wanasayansi. Yeye siyo mwanasayansi. Kama ana mashaka yoyote, alistahili kueleza mashaka yake kwa wanasayansi. Wanasayansi ndiyo wangeifanya kazi ya quality control and analysis. Kosa kubwa ni pale Rais anapofikiria kuwa TISS wanaweza kumpa majibu ya uhakika. TISS wengi tunawafahamu, siyo wanasayansi. Wengine hata hawastahili kuwepo huko TISS. Wameigeuza kazi ya Intelligence kuwa sawa na umbea/majungu.

Rais Magufuli amesoma masomo ya Sayansi lakini hajawahi kuwa mwanasayansi.

Tangu amalize PhD yake, hajawahi kuingia maabara kufanya study yoyote ya Sayansi, hajawahi kushiriki conferences zozote za kisayansi ambazo huelezea maendeleo katika fani mbalimbali za Sayansi, hajawahi kushiriki kufanya research zozote za Sayansi.

Kimsingi, yeye ni mwanasiasa. Muda wake mwingi wa maisha yake umeutumia kwenye siasa. Ni mwansiasa kuzidi hata waliosomea masomo ya siasa ambao hawajawahi kufanya siasa.

Ni kosa kubwa kufikiria kuwa ukisomea masomo tu ya sayansi, basi wewe ni mwanasayansi au ukisomea tu masomo ya sheria basi umekuwa mwanasheria, japo unakuwa na advantage ndogo ya uelewa yakiwa yanaongelewa mambo ya fani ambayo masomo ya fani hiyo ulipata kuyasoma.

Rais ni mwanasiasa. Anashinda anaongea siasa, anawaza siasa, analala akiota siasa. Huyu ni mwanasiasa. Asisahau kuwa kuna watu ni wanasayansi, kuna watu ni wataalam wa maabara. Wanashinda kwenye maabara, mazungumzo yao karibia yote yanahusu mambo ya maabara, semina na conferences zote wanazohudhuria, zinahusu maabara, makala nyingi wanazosoma zinahusu maabara, hawa ni wataalam wa maabara.

Vifaa vya maabara havinunuliwi kama mashati. Mtengenezaji wa vifaa vya maabara ili vifaa vyake viweze kufanya kazi iliyokusudiwa, hufanyiwa majaribio, na huidhinishwa na WHO. Kama kweli kuna hitilafu ya uwezo wa vifaa vinavyotumika maabara yetu ya Taifa, wa kwanza tunaotakiwa kuwashutumu ni WHO ambao wameruhusu vifaa hivyo vitumike. Wengine wanachanganya kati ya vifaa vya maabara kwaajili ya kupima Covid 19 na quick test kits za Covid 19. Kuja baadhi ya nchi wamelalamikia quick test kits LAKINI siyo vipimo vya maabara kama hiki tunachokilalamikia sisi. Sasa wewe kulalamikia kitu ambacho hakijaonesha hitilafu sehemu nyingine yoyote, unastahili kufanya scientific tests hasa, na hizi za kuoima mafenesi na kwale wakati mtengenezaji hajaeleza kama kifaa hicho kinaweza kupima hivyo vitu.

Huwezi kwenda kuilaumu WHO kwa namna alivyofanya Rais wetu. Kulistahili kufanyika detailed scientific studies kuweza kuzidisqualify idara za WHO zilizoidhinisha kutumika kwa vifaa hivi.

The whole approach to this matter has been disgracefully wrong. Mwisho wa yote ni aibu kwa Rais wetu na kwa Taifa kwa ujumla.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya. Bia yako na wenzako. Kazi kwenu. Unaona hili beberu lilivyojaza? Try to confront it if you dare!
 
Huyo atapingaje matokeo ya experiment bila yeye kufanya experiment?
Hata Europe nchi kibao zimeshagundua hizo test kits kuwa nyingi ni feki.
Magu yuko sahihi kwenye hili
 
Nadhani hujui kanuni za QAQC za scientific studies.

Kama walitaka kujua quality ya results, walichotakiwa kufanya ni kuchukua samples za binadamu kwa namna anavyoelekeza mtengenezaji wa kifaa na kisha kuzipeleka kwenye maabara 5. Na kisha kulinganisha majibu. Siyo kuchukua samples za mafenesi, mara sijui kuku na mbuzi! Ukifanya hivyo itaonekana hujui unachokifanya, labda kama mtengenezaji amekuambia kuwa kifaa hicho kinaweza kupima matunda na wanyama wa kufugwa na wa porini.

Na kama atakuwa amesema hivyo (japo najua siyo), atakuwa pia amekuelekeza namna ya kuchukua hizo samples, treatment yake, na reagents utakazotumia.

Kuna kanuni zinazoelekeza namna ya kuchukua samples, na kwa Covid 19, ni lazima iwe ni kwenye chumba chenye ubaridi na negative pressure. Sasa hao mbuzi na mafenesi, sijui walichukuliwa samples kwenye mazingira gani, na sijui kama Rais aliwapelekea reagents za kutumia kwenye hizo samples kwa kadiri ya maelekezo ya mtengenezaji (maana huwezi kutumia reagents zinazotumika kupimia binadamu) wa mashine ya kupimia!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo dokta angeunda team pamoja na ya Magufuli wacheck pamoja. Sasa yeye anajua je machine ya Tz inafanya kazi vizuri bila kuja kuwa na task forces ya pamoja?
 
Return Of Undertaker,

He is rubbish headed, Thanks Ndugu Rais Magufuli, our journey for the greatest tomorrow of ours shall encounter hundreds of battles.
 
Wewe ndio wataka kuyumbisha. Yeye alijisfu kwa uvumbuzi. Wakati alifanya maigizo ili kuhalalisha madai yake ya kudharau kiwango cha maambukizi.
 

Lazima watetee corruption yao ya kuingiza hivyo vifaa katika Afrika. Subiri uone huyo Ma atakavyokurupushwa na Chinese Community Party kwakuwa wamemgundua pia anatoa misaada kwa uelekeo wa kujinufaisha kisasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…