#COVID19 CHADEMA: Chanjo ya COVID-19 iwe ya lazima

#COVID19 CHADEMA: Chanjo ya COVID-19 iwe ya lazima

Nia nzuri ipi. Msimfanye mkubwa wenu kuwa hakosei. Taja Nchi gani chanjo hizi Ni lazima. Hakuna chanjo iliyochukua miaka 2. it’s a risky. Mimi nilichomwa toka mwezi wa nne kwa hiari. Na wengi tu ulaya huku hawataki. Afu Sijaona huku ulaya mwana upinzani anatoa hotuba za namna Hii. Mama mwema sana.
Umesoma haraka comment yangu
 
naona unazidi kuchanganyikiwa baada ya vurugu za katiba mpya kukwama.

chanjwa wewe na familia yako inatosha achana na sisi
 
Naunga mkono hoja ya Mbowe, chanjo ya Corona iwe ya lazima, mnaosema hiari bado Corona haijawatembelea ndio maana.

Mkuu mwanzo wa ngoma ni lele lakini hii chanjo tunakokwenda ni wazi kuwa itakuwa ni lazima na serikali inalijua hilo.

Hapa chini niliandika kwao Salary Slip na technically (waliokuwa na reservations zao) heshima kwao sana:

IMG_20210719_184727_684.jpg


Cc: Vessel
 
Acheni uongo wakati mwingine unaogeuzwa kisiasa,hivi mgonjwa wa kipindupindu useme anahiari ya kupatatiba au akatae,nini kitatokea.
Hujui kitu kuhusu medical ethics. Unalinganishaje Kipindupindu na COVID-19? Unajua Mortality rate ya Kipindupindu wewe? Hata Polio, Chanjo yake haikua lazima na haikupigiwa debe na wanasiasa. Acheni wataalam wafanye mambo yao kwa Uhuru na ninyi wanasiasa mfanye yanayowahusu kwa Uhuru. Kama mtu hawezi lazimishwa kuongezewa damu, sembuse Chanjo?
 
Mkuu mwanzo wa ngoma ni lele lakini hii chanjo tunakokwenda ni wazi kuwa itakuwa ni lazima na serikali inalijua hilo.

Hapa chini niliandika kwao Salary Slip na technically (waliokuwa na reservations zao) heshima kwao sana:

View attachment 1859891

Cc: Vessel
Kwangu kigezo cha chanjo ina madhara hakina maana, ni bora uchanjwe upate kinga hata kama itakuwa na madhara peke yako (japo sio guarantee kudhurika kwa chanjo), kuliko ukae bila kuchanjwa halafu uje kuwaambukiza wengi zaidi na usababishe vifo vingi zaidi.
 
Wanasema mwanzo wa ngoma ni lele:
Kwangu kigezo cha chanjo ina madhara hakina maana, ni bora uchanjwe upate kinga hata kama itakuwa na madhara peke yako (japo sio guarantee kudhurika kwa chanjo), kuliko ukae bila kuchanjwa halafu uje kuwaambukiza wengi zaidi na usababishe vifo vingi zaidi.

That is obvious. But remember, common sense is not common to everybody.
 
Acheni uongo wakati mwingine unaogeuzwa kisiasa,hivi mgonjwa wa kipindupindu useme anahiari ya kupatatiba au akatae,nini kitatokea.
Unapofananisha vitu, fananisha vinavyolingana.

Mgonjwa wa kipindupindu ni mtu ambaye ana ugonjwa tayari.

Chanjo inatolewa kwa mtu ambaye hana ugonjwa, ili kumkinga.

Kitaalamu, kitabibu, kwa kufuata maadili ya kitabibu, kabla ya kuchanjwa unatakiwa ukubali, unapewa fomu ya kusaini kukubali kuchanjwa.Ionekane wazi kwamba hujalazimishwa.

Haya ni maadili ya kitabibu yanayoeleweka dunia nzima.

Ni maadili ya kitabibu na sehemu ya haki za kibinadamu.

Sasa unataka Tanzania iachane na mikataba ya kimataifa inayotambulika na Umoja wa Mataifa inayokataza kulazimisha chanjo?

Unafahamu madhara ya kulazimisha chanjo, hata kama hii chanjo ni kitu kizuri na kinapunguza vifo?
 
Hapo ndio CHADEMA wanapofeli , sasa hivi vilio vya wananchi ni tozo za simu wao wameng'ang'ania chanjo ya corona
 
Tuangalie wenzetu waliotutangulia katika demokrasia wanasemaje, naangalia demokrasia kwa sababu CHADEMA ni Chama Cha Demokrasia na Maendeleo. Demokrasia ipo katika jina la chama.

Mimi nakaa Marekani kuna demokrasia mpaka inakuwa fujo.

Katika majimbo yote 50 ya Marekani hakuna jimbo linalolazimisha chanjo.Yani wanaweza kukubana ukitaka kufanya kazi hii ni lazima upigwe chanjo, ukitaka kusoma shule hapa ni lazima upigwe chanjo. Hivi vitu vilikuwepo kabla ya Covid.Mimi nilivyosoma chuo hapa ilikuwa huwezi kuanza chuo kabla ya kuonesha ushahidi wa chanjo ya MMR (Measles,Mumps and Rubella). Lakini hakuna sehemu serikali ya Federal au State wanaposema ni lazima watu wote wapigwe chanjo.

Na siku serikali itakapolazimisha chanjo ndipo baadhi ya watu watu watachukua bunduki zao kuingia mtaani kuandamana.

Mimi napenda chanjo, nimechanja chanjo zote mbili za Pfizer, naona watu wanaokataa chanjo kuwa ni tatizo kubwa sana, kwa sababu wao ndio wanaosababisha mlipuko wa ugonjwa uendelee. Sasa hivi Marekani watu wanaolazwa mahospitalini kwa Covid na wanaokufa karibu wote ni wale waliokataa chanjo. 9 Covid deaths out of 10 in the US are for people who are unvaccinated.

See here
Lakini sitaki waingiliwe katika haki yao ya kukataa chanjo.

In fact hiyo inaweza kuwa a special case ya Darwinian evolution kuua watu wajinga na kuacha dunia iendelee na watu wenye maarifa.

Sasa mimi siku zote nimekuwa natetea haki binafsi za watu, kama mtu kachoka maisha anataka kufa kifo cha "suicide by Covid" mimi nina haki gani ya kumkatalia?

NPR wameripoti kwamba sasa hivi Marekani vifo vya Covid vinaongezeka, na 90% ya wanaokufa ni watu waliokataa chanjo.

Sasa mtu akitaka kufa mwenyewe mimi ni nani nimkatalie?

Mimi nafikiri hoja kuu hapa ni suala la "ulazima" ama "lazima". Hapa ndipo wengi wanapokuwa na wasiwasi napo hasa kuhusu utekelezaji wa huo "ulazima". Isitoshe, wengi bado wana hofu [tena kubwa sana] juu ya usalama wa chanjo.

Mpaka sasa kuna nchi ambazo tayari zimekwisha weka ulazima wa chanjo kwa raia wake kutokana na mwenendo wa ugonjwa na jinsi maambukizi yanavyozidi kuongezeka. Marekani pamoja na nchi kadhaa za Ulaya tayari zimeweka utaratibu kwa baadhi ya watu kuchanjwa kwa lazima.

Hizi waves zinapozidi kuongezeka na kuendelea huku watu wakiendelea kugomea chanjo athari zitakwenda mpaka kwa wale waliokwisha chanjwa. Na hili limekwisha anza kuonekana.

Kama ni suala la haki za binadamu, sidhani kama kuna haki kwa serikali kuwaacha watu wafe tu ama wajiue (suicide by Covid) kisa wamejichagulia wenyewe. Wala sidhani kama kuna nchi ya kidemokrasia inayoweza kupuuza matendo ya namna hiyo ya watu kujaribu kujidhuru ama kijiua kwa makusudi au kwa utashi wao wenyewe.
 
Acheni uongo wakati mwingine unaogeuzwa kisiasa,hivi mgonjwa wa kipindupindu useme anahiari ya kupatatiba au akatae,nini kitatokea.

Mkuu huna haja ya kupoteza nguvu nyingi kubishana na watu ambao aghalabu uelewa wao ndiyo hivyo tena.

Wanasema mwanzo wa ngoma ni lele.

Hata serikali inajua kuwa hii chanjo baadaye itakuwa ni lazima. Serikali wanapanga kuyavuka madaraja muda utakapofika.

Leo wanasema chanjo kutoka Desemba. Yanini waanze marumbano sasa?

Si waona hata barakoa ilivyokuwa? Mwanzo hiari, kisha huingii kwenye ofisi, hospitali, bus, nk bila barakoa.

Hata hivyo nadhani:

IMG_20210719_185857_625.jpg
 
Mimi nafikiri hoja kuu hapa ni suala la "ulazima" ama "lazima". Hapa ndipo wengi wanapokuwa na wasiwasi napo hasa kuhusu utekelezaji wa huo "ulazima". Isitoshe, wengi bado wana hofu [tena kubwa sana] juu ya usalama wa chanjo...
Marekani imeweka ulazima wa kuchanja kwa nani?

Unaelewa kwamba maadili ya kitabibu yanakataza mtu kulazimishwa kuchanja chanjo?
 
Kwenye hili la chanjo kulazimisha ndio ninapowaona Chadema ni watu wa hovyo. Unalazimishaje swala la afya yangu na familia yangu? Kufanyiwa upasuaji wenyewe lazima usainishwe fomu ndipo ufanyiwe kama sio wewe ni ndugu yako wa karibu. Wanaacha kuongelea mambo ya maana wanaongea pumba.
 
Marekani imeweka ulazima wa kuchanja kwa nani?
Kwa Marekani, nazungumzia vaccine mandates katika taasisi na kampuni binafsi.

Isitoshe, chanjo nyingi bado hazina ama hazijapata full approval ya FDA. Zinatumika kama emergency tu. Utaratibu wa vaccine mandates unaweza kuongezeka zaidi hapo baadaye pale chanjo zitakapopata full approval.
 
Kwa Marekani, nazungumzia vaccine mandates katika taasisi na kampuni binafsi.

Isitoshe, chanjo nyingi bado hazina ama hazijapata full approval ya FDA. Zinatumika kama emergency tu. Utaratibu wa vaccine mandates unaweza kuongezeka zaidi hapo baadaye pale chanjo zitakapopata full approval.
Hiyo mandate unayoiongelea Marekani si ya serikali federal au state, ni ya waajiri, shule etc, ambayo nishaizungumzia hapo juu.

Hiyo ni tofauti na anayosema Mbowe ya serikali kulazimisha wananchi.

Nakwambia hivi, kanuni za maadili za kitabibu zinakataza chanjo kulazimishwa.Ndiyo maana kabla ya kupigwa chanjo unapewa consent form usaini/ usome na kuelewa.

Sasa Mbowe anavyotaka serikali ilazimishe chanjo anataka kuondoa consent ?
 
Hii nchi inabidi wananchi tuingie msituni ili hawa wanaisiasa uchwara akili zao zikae sawa

Tumechoka hizi drama.
 
Back
Top Bottom