CHADEMA fursa iliyopo wazi kwa sasa ni kuwatumia wafuasi wa hayati Magufuli kujiimarisha zaidi kwa ushindi wa 2025 huu ndio mtaji wetu mkubwa kisiasa

CHADEMA fursa iliyopo wazi kwa sasa ni kuwatumia wafuasi wa hayati Magufuli kujiimarisha zaidi kwa ushindi wa 2025 huu ndio mtaji wetu mkubwa kisiasa

Magufuli alikuwa na wafuasi wengi sana. Mama ntilie, machinga, wakulima na watu wa hali ya chini. Yeye aliwaita wanyonge. Hawa ndio mtaji wetu kwa sasa. Tuwatafute na kuwavuta Chadema maana CCM ya sasa imewakataa na imerudi kwa mafisadi.

Tuwapange vizuri na ikifika mwaka 2025 huu ndio mtaji mkubwa kwa ushindi wa kukamata dola.

Nimetoa ushauri naomba uzingatiwe.
Hii nakuunga mkono. Siasa haina adui wa kudumu. Cha muhimu malengo yatimie
 
Chadema ni adui wa magufuli sisi hatuwezi kuwakubari tunangoja chama kipya ,hapo chadema na act cha zitto watashangaa kuwa jpm ana nguvu kubwa baada ya chama hicho kuwa na nguvu kuliko vyama vyote tz,magufuli anakubalika kwa asilimia 90% ya watz 10% ndiyo wanagawana wahuni wa ccm na upinzani

Angekuwa anakubalika asingeiba kura 2020. 2015 alipata asilimia 56 ya kura zote na hapo wizi uliofanyika. Hiyo asilimia 90 alipata wapi?. Msilazimishe Watu wamuabudu huyo kiumbe mwenye roho mbaya. Bora ameondoka alikuwa anataka kuzalisha Taifa la mazezeta yanayopelekwa Kama mangombe.
 
Chadema hawahawa aki na Lema? Mwenyekiti ameuza mechi Kwa mama, sukuma gang ni kundi linalojitegemea ila liko kimya hadi 2024.
 
Kama na wewe ni mmoja wapo wa walio husika kumuua basi jiwekee ulinzi wa kutosha kama wenzako walio husika wanavyo fanya ,mwenzako mkwele anaishi kama digidigi na madoctor wake

Acha kuidhalilisha security ya Tanzania. Yani kwa ulinzi aliokuwa anapewa ndio aje auawe na Kikwete. Yani kikwete afanye mpango wa kumuua amri jeshi mkuu, wewe raia ujie halafu wakuu wa ulinzi wasijue.

Yule karma ndio imemuondoa kwa ujinga alioufanya kwenye uchaguzi wa 2020. Halafu ukiua kwa upanga utakufa kwa upanga.
 
Chadema hawahawa aki na Lema? Mwenyekiti ameuza mechi Kwa mama, sukuma gang ni kundi linalojitegemea ila liko kimya hadi 2024.

Mbona mnaifuatilia Sana chadema? Yani kura muipe CCM halafu lawama mpeleke chadema. Halafu hao sukuma gang walikuwa wapi kinana akipata asilimia 100 ya kura?. Hakuna Cha sukuma gang Wala nini.
 
Bwashee chadema yenyewe unayotaka ituvute kwenda kwayo ni ipi, hii hii ambayo mgombea wao ni tundu lisu?
Kama ni hiyo basi ushauri wako hautafanya kazi. Hatuwezi kuongozwa na mtu ambaye hazimtoshi #dishlimetilt

Unapata mateso baada ya kushindwa kumuua. Yani mumpige mtu risasi halafu mje kulalamika hazimtoshi. Uzuri aliyeagiza Tundu Lissu apigwe risasi kaondoka yeye na kumuacha Lissu.
 
Yaani ....

Makonda, mpina, Bashiru.... Ndiyo watumike kuisaidia chadema??. Ni mara 1000 covid kama mzee mdee, Bulaya wakarudishwa kundi kuliko upuuzi wa hao.
 
Viongozi wengi CHADEMA wenye maono wamestuka hawamtukani tena. Unajua idadi ya kura za machinga Nchi nzima walioharibiwa biashara zao ni wangapi? Wamuona ni SHUJAA wao.

Mnajaribu kutishia Watu kana Magufuli alikuwa mtu mwema Sana, kama vile tulikuwa hatuishi naye. Hakuna kiongozi chadema atakaye mkubali Magufuli aliyezuia chadema wasifanye siasa kwa miaka sita na ushee.
 
Magu alichukiwa na C.C.M na CHADEMA wapiga deal. lakini alipendwa na WANANCHI Walio wengi wenye vipato duni wasio na vyama.

Acheni uongo, mtu alyependwa CCM Ni jakaya 2005. Kila mtu alimkubali, sio huyo muiba kura za Watu 2020. Kupendwa hakulazimishwi ni hiari. Mstulamishe kumkubali mtu ambaye yeye mwenyewe Hana upendo.
 
Magufuli alikuwa na wafuasi wengi sana. Mama ntilie, machinga, wakulima na watu wa hali ya chini. Yeye aliwaita wanyonge. Hawa ndio mtaji wetu kwa sasa. Tuwatafute na kuwavuta Chadema maana CCM ya sasa imewakataa na imerudi kwa mafisadi.

Tuwapange vizuri na ikifika mwaka 2025 huu ndio mtaji mkubwa kwa ushindi wa kukamata dola.

Nimetoa ushauri naomba uzingatiwe.
Kwa tume ipi brother itakayo watangaza?
 
CHADEMA ijifunze kukubali MAZURI ya viongozi kama yananufaisha wananchi. Waache kupinga kila kitu mfano ktk Sakata la makinikia Tundu alitanguliza maslah yake mbele kama mwanasheria kutetea wezi ,CHADEMA ikanyamaza. Wananchi tulikosa uungwaji mkono Kutoka vyama vya upinzani kuhusu suala Hilo. Sijui kama mtasamehewa.

Mnaitaka chadema ya Nini? Bungeni mmejaza CCM na kwenye halmashauri mmejaza CCM. Kwa nini msiwapigie kelele hao.

Achaneni na chadema wanafiki nyie. Mtu kutoa ushauri kwamba tunaweza kushtakiwa twende kwa makini ni vibaya?.
 
Mnaitaka chadema ya Nini? Bungeni mmejaza CCM na kwenye halmashauri mmejaza CCM. Kwa nini msiwapigie kelele hao.

Achaneni na chadema wanafiki nyie. Mtu kutoa ushauri kwamba tunaweza kushtakiwa twende kwa makini ni vibaya?.
Hoja Kwa hoja. Tunataka KATIBA mpya iongoze hata sera za vyama pinzani, tuwe na maono ya kitaifa. Lisu alisema mashoga wapewe HAKI zao🙂, je huo ni msimamo wa CHADEMA? Watanzania watakueleweni na kuwaamini ktk mambo hayo? Alipinga chanjo Kwa nguvu lakini katk kampeni hakuvaa barakoa! Ktk meng Bado kinapwaya. Tunataka vyama vya siasa imara. Mimi Sina chama. Nadeclare interest.
 
Peleka ungiri mbali ww sukuma gang, dhalimu hakuwa na ushawishi wowote zaidi ya ulevi wa madaraka. Angekuwa na hao watu asingenajisi uchaguzi. Ulivyo na gundu hata huko ccm hawakutaki.
Wewe utakuwa vyeti feki uliyetumbuliwa hadi leo huamini hakuna ajira kwa wenye vyeti feki
 
Magufuli alikuwa na wafuasi wengi sana. Mama ntilie, machinga, wakulima na watu wa hali ya chini. Yeye aliwaita wanyonge. Hawa ndio mtaji wetu kwa sasa. Tuwatafute na kuwavuta Chadema maana CCM ya sasa imewakataa na imerudi kwa mafisadi.

Tuwapange vizuri na ikifika mwaka 2025 huu ndio mtaji mkubwa kwa ushindi wa kukamata dola.

Nimetoa ushauri naomba uzingatiwe.
Sukuma gang usiyechoka.
 
Magu alichukiwa na C.C.M na CHADEMA wapiga deal. lakini alipendwa na WANANCHI Walio wengi wenye vipato duni wasio na vyama.
Wananchi tulio wengi tusio na vyama ndiyo tulimchukia zaidi.
 
Back
Top Bottom