CHADEMA: Hatutaingilia Mahakama kuhusu kesi ya Wabunge 19 kupinga kuvuliwa uanachama

CHADEMA: Hatutaingilia Mahakama kuhusu kesi ya Wabunge 19 kupinga kuvuliwa uanachama

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinatarajia kutoa tamko leo Mei 17, 2022, ambapo waandishi wa habari wamekaribishwa kuchukua taarifa ambayo inatarajiwa kuzungumza, lakini kubwa wengi wanaamini itakuwa inahusu sakata la kina Halima Mdee na wenzake 18.

====

"Wanaojaribu kufanya propaganda huko (Sakata la kina Mdee), suala hili limekwenda mahakamani, tuko tayari na mahakamani wametupeleka eneo ambalo kwetu ni kanda ya faraja, ni eneo tunalomudu. Sidhani kama kuna kesi ambayo Chadema ilishindwa mahakaamni, rekodi bazipo," - John Mrema.


"Fomu za kudhaminiwa kwa hawa wabunge 19, zilitoka wapi na zilikuwa za chama gani? Maana fomu za kudhaminiwa za CHADEMA hadi leo zipo. Katibu Mkuu aliyepeleka majina alikuwa ni wa chama gani kwa kuwa Katibu Mkuu John Mnyika hakuwahi kupeleka majina Tume ya Uchaguzi," - Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara


"Sasa tunakwenda kuwahoji (kina Halima Mdee), nani alisaini barua zao? Nchi hii ingekuwa inafuata sheria, wangekuwa na kesi ya jinai ya kughushi nyaraka na kujipatia fedha za walipa kodi kinyune cha sheria," - John Mrema.


"Ili mtu yeyote awe mbunge wa CHADEMA ni lazima ateuliwa ha kamati kuu ya CHADEMA kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA na mamlaka ambao kamati kuu imepewa," - Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara.


"Walipoitwa (Wabunge 19) kujieleza kamati kuu walisema wanahofia usalama wao na wakaomba wapangiwe siku nyingine. Katibu Mkuu John Mnyika aliwajibu kuwa wenye mamlaka hayo ni Kamati Kuu, hawakutokea. Hivi Mahakamani mshtakiwa asipotokea shauri haliendelei kusikilizwa?" - Benson Kigaila

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Benson Kigaila amesema Chama hicho hakitaingilia taratibu zinazoendelea mahakamani kuhusu wabunge 19 waliofutiwa uanachama, huku akisisitiza kuwa hawakuwahi kumteua mtu kuwa mbunge wa viti maalum na hawautambui uchaguzi wa mwaka 2020 wala matunda yoyote ya uchaguzi huo
Hii ni dharau kwa kodi za wananchi na siyo kwa CHADEMA
 
Mkuu uandishi huu wa kipumbavu sio mzuri, unalifanya jukwaa hili lionekane ni kijiwe, CDM wameshatolea tamko kuhusu hii issue mara nyingi tu, HAWACHUKUI RUZUKU, looo hii dot.com mnasumbua sana kwa ufikiri wenu butu
Hao ni madalali wa CCM
 
sasa chadema wasivyo na viongozi wenye akili unasema hamtaingilia mahakama wakati tayari unazungumzia suala lililoko mahakamani chadema hambna viongozi kuna waganga njaa
Hiyo ni heading tu mmepewa, the rest mtakutana na kina Kibatala ofisini kwao japo jana mlitaka kuwakimbia lakini wapi jamaa wakaibuka tu.
 
Acha upumbavu wewe na ndo shida ya kuongozwa na mtu alofeli Kidato cha Sita huyo Mbowe wenu, aliwahi kulikataa gari la Kiongozi wa Upinzani Bungeni lakini akalichukua kinyemela sembuse Ruzuku? Ruzuku za Wabunge 19 CHADEMA wanazichukua na hawajawahi kuzikataa.
Elimu si kigezo cha kuwa kiongozi bora,ndio maana nakuambia acha kuandika upumbavu, President Mugabe alisoma sana ila ameiacha nchi yake masikini sana na almost 20%ya raia wake wakiwa wakimbizi wa kiuchumi,icon pekee Africa, Madiba hakusoma sana kielimu (LLB)but aliiongoza SA in a very trying time, CDM hawakuchukua ruzuku na hii ni fact
 
UTAKUWA HUJUI VIZURI CHADEMA YAANI HIZO DOCUMENT WANGEKUWA WAMEFOJI NA CDM WANAVYOPENDA KESI WANGEKUWA WAMESHAENDA MUDA MREFU KUSHITAKI NA HUJIULIZI KWANINI WLAIKUWAHWAEND MAHAKAMANI KUWASHITAKI KINA MDEE SASA WANAUMBUKA
Ndugu yangu,
nadhani weye ndio sio tu huijui vizuri CHADEMA bali pia huwajui huwajui vyema WAHUNI wanaoshindana kutafuta na kutengeneza mianya ya kuimaliza CHADEMA. Kwa bahati mbaya nawe umejaa kwenye mtego huo.
Hata hivyo kesi hii waliyofungua covid 19 itasaidia SANA kuwafungua wengi macho kuwa HUU ni mwendelezo uleule wa juhudi zilezile za wahuni, tofauti yaweza kuwa mawakala wameongezeka. KATIBA MPYA ndio tiba.

Ndo tushafika patamu, tu karibu na utamu.
Pa ukweli pana tamu, kwa wajuao utamu.
Kwa wa hila si patamu, bali chungu iso tamu.
Siku wakijua tamu, watakuta ziso tamu.
 
Mkuu uandishi huu wa kipumbavu sio mzuri, unalifanya jukwaa hili lionekane ni kijiwe, CDM wameshatolea tamko kuhusu hii issue mara nyingi tu, HAWACHUKUI RUZUKU, looo hii dot.com mnasumbua sana kwa ufikiri wenu butu
Bora umuelimishe maana Ni shida tupu!
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinatarajia kutoa tamko leo Mei 17, 2022, ambapo waandishi wa habari wamekaribishwa kuchukua taarifa ambayo inatarajiwa kuzungumza, lakini kubwa wengi wanaamini itakuwa inahusu sakata la kina Halima Mdee na wenzake 18.

====

"Wanaojaribu kufanya propaganda huko (Sakata la kina Mdee), suala hili limekwenda mahakamani, tuko tayari na mahakamani wametupeleka eneo ambalo kwetu ni kanda ya faraja, ni eneo tunalomudu. Sidhani kama kuna kesi ambayo Chadema ilishindwa mahakaamni, rekodi bazipo," - John Mrema.


"Fomu za kudhaminiwa kwa hawa wabunge 19, zilitoka wapi na zilikuwa za chama gani? Maana fomu za kudhaminiwa za CHADEMA hadi leo zipo. Katibu Mkuu aliyepeleka majina alikuwa ni wa chama gani kwa kuwa Katibu Mkuu John Mnyika hakuwahi kupeleka majina Tume ya Uchaguzi," - Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara


"Sasa tunakwenda kuwahoji (kina Halima Mdee), nani alisaini barua zao? Nchi hii ingekuwa inafuata sheria, wangekuwa na kesi ya jinai ya kughushi nyaraka na kujipatia fedha za walipa kodi kinyune cha sheria," - John Mrema.


"Ili mtu yeyote awe mbunge wa CHADEMA ni lazima ateuliwa ha kamati kuu ya CHADEMA kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA na mamlaka ambao kamati kuu imepewa," - Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara.


"Walipoitwa (Wabunge 19) kujieleza kamati kuu walisema wanahofia usalama wao na wakaomba wapangiwe siku nyingine. Katibu Mkuu John Mnyika aliwajibu kuwa wenye mamlaka hayo ni Kamati Kuu, hawakutokea. Hivi Mahakamani mshtakiwa asipotokea shauri haliendelei kusikilizwa?" - Benson Kigaila

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Benson Kigaila amesema Chama hicho hakitaingilia taratibu zinazoendelea mahakamani kuhusu wabunge 19 waliofutiwa uanachama, huku akisisitiza kuwa hawakuwahi kumteua mtu kuwa mbunge wa viti maalum na hawautambui uchaguzi wa mwaka 2020 wala matunda yoyote ya uchaguzi huo
Ukimkuta Kobe juu ya mnazi ujue Luna aliyempandisha.
CHADEMA walieleza jambo hili Mara zote kwa ufasaha usioacha maswali lakini kina Mdee+wenzake na watetezi wao CCM,Bunge,NEC,Serikali na Sasa Mahakama tukufu hawaelewi chochote pamoja na maelezo fasaha.Spika anajifanya hamnzo kwa kudai anasubiri uamuzi Wa Mahakama kabla hats shauri halijasikilizwa/kuamuliwa.Hii ni sawa na kusema Spika amei per-empty mahakama halafu nayo ikafuatisha hivyo hivyo.
Katiba hii mbovu wanayoitetea hawaiheshim lakini bado wapo kwenye nyadhifa zao kwa sababu katiba mbovu inawalinda na Watanzania wapo kwenye silent mood,hawalalamikii hilo na hawajitetei wala hawailindi Katiba ya 1977,hawashinikizi kuipata mpya wala hawawajibishi viongozi waliojibadilisha kuwa miungu watu na ni kama tumepigwa ganzi ya ubongo vile.
Tunahitaji nchi yetu ya Tanganyika maana huku Tanzania pametushinda.Bora turudi nyumbani hata kama ni kubaya,tutajenga upya.
 
Wasisusie mwaliko wa Ikulu tu. Sakata la kina Mdee tayari lipo Mahakamani hairuhusiwi kulijadili hadi kesi iishe hapo December 2024
Nani aliyekudanganya kuwa swala likiwa mahakamani halijadiliwi? Mbona kesi ya Kingai na group lake tuliijadili!?

Inategemea tu unajadili vipi.
 
Naibu katibu mkuu wa Chadema mh Benson Kigaila amesema chama chake hakitapeleka NEC majina ya Wabunge 19 wa viti maalumu kwa sababu hawautambui uchaguzi mkuu wa 2020

Source: ITV

Sasa Mbowe huwa anaalikwa na nani Ikulu?
 
Wapuuzi Sasa kelele za nn kwa WANAWAKE 19 so wawache tu hatakama hawatakuwa na chama , wamekuwa joka la mdimu

USSR
 
Hawa waliopo alipeleka nani? Ni vipi suala hilo lisipatiwe ufumbuzi, hata kesi ya kutetea uanachama wao isingekuwepo!
 
Naibu katibu mkuu wa Chadema mh Benson Kigaila amesema chama chake hakitapeleka NEC majina ya Wabunge 19 wa viti maalumu kwa sababu hawautambui uchaguzi mkuu wa 2020

Source: ITV

Sasa Mbowe huwa anaalikwa na nani Ikulu?
Eeh waache kwani nani anawalazimisha? Kwani wasipoteua itakwamisha Serikali au kuleta njaa kwa watu?
 
Back
Top Bottom