Tindo
JF-Expert Member
- Sep 28, 2011
- 63,730
- 111,542
Habari za leo ndugu zangu wa chama cha CHADEMA. Leo nataka niwaibie siri ila siwalazimishi kuifuata ni juu yenu.
Ni hivi,
"CHADEMA mkimwomba msamaha Magufuli na kuamua kufuata sera na maono yake, 2025 mnachukua nchi kilaini sana".
Nimeyasema haya kwasababu alitaka mjenge naye uchumi lakini mlianza usumbufu. Mkaanza kumsumbua, aliteua hadi watu kutoka chama chenu lakini bado mliendelea kuwa wasumbufu.
Hamkupenda kushirikiana naye ni kwasababu hamkumkubali. Sasa wakati wa kumkubali ndio huu, kuomba msamaha na kufuata sera na nyayo zake. Na sababu za kutomkubali na usumbufu wote mlioanza kumletea chanzo chake ilikua ni sanduku la kula. Hamkuamini ushindi wake 2015.
Basi hamna budi kujitakasa na kumkubali sasa, 2025 ndipo mtaweza kushinda. Nimesema haya kwasababu watanzania kuna kitu wanakiamini. Hicho ndicho mwatakiwa kukifuata.
Mkifanya hivyo hamtahitaji hata kupiga kampeni wala kuitisha mikutano na wananchi au waandishi wa habari. Mtajikuta mnakubalika tu.
Kama hamniamini jaribuni hata saivi mtume tu kavideo Facebook au Instagram, alafu mje kusimulia hapa jamii forum.
Yaani Cdm wamuombe msamaha mtu aliyekuwa dhalimu na jizi la kura? Kama hizo sera zake zilikuwa zinakubalika, kwanini alinajishi chaguzi za nchi ili akae madarakani kwa shuruti? Subiri kuna chama kinaanzishwa na CCM kwa uratibu wa Tiss, wape hizo sera za Magufuli wakachukue nchi.