Katiba mpya ni kuelekea 2030
huko huku kuelekea.
Watanganyika wasikubali huu mfumo wa Chama Kimoja na chama kushika hatamu . Huu mfumo wa Chama dola uliwasumbua sana maadui wa nje wakiwemo wale Waliopinduliwa kule Zanzibarna na kurudi kwao Oman na wengine kukimbilia Ulaya.
Baada ya Azimio la Zanzibar hakuna tena chama kushika hatamu bali mwenekiti wa Chamab kushika Hatamu kwa Rushwa na misaada kutoka huko huko kwa Wakoloni tuliowapokonya nchi kwa damu za kina mkwawa. lililoazimia kurudisha Usultani na kuwakabidhi nchi ya Tanganyika na kuanzia kwa kuwauzia Eneo la Loliondo na wanyama waliopo kwa karne nzima na sasa kasi ya kumaliza kila kitu kwa kuwapa watu wenye ELIMU NA UWEZO KAMA SISI. Wananunua Teknolojia kama sisi . Wananunua ndege kama sisi ,wananunua magari na Computer kama sisi ,wananunua madawa kama sisi. Walichotushinda ni kitu kimoja wanawanunua Watawala na kuwapa pesa za kuhongo kwenye uchaguzi.
Kwa nini tutumie pesa na kodi za wananchi kuingia kwenye uchaguzi uliokwisha kununua washindi na hakuna kura zitakazo hesabiwa na kutoa ushindi kwa aliyechaguliwa ?
Kwa nini tuendelee kupoteza maisha ya watu watakaojitokeza kupinga dhulma wakati walitakiwa wapinge uchaguzi kufanyika chini ya Tume ya Iliyopatikana kutokana na katiba iliyogeuzwa kuwashughulikia wapinzani wa kisiasa badala ya mabeberu na wanyonyaji wankiuchumi toka nje?
CCM ni chama cha wakulima na wafanyakazi lakini sasa kimegeuka kuwa chama cha mafisadi na machawa kwa manufaa ya wageni .
Kongo ilianza hivi hivi kuwafutahia marajiri toka ufaransa ,ubelgiji na marekani walipokuwa wanamwaga mapesa kwa Mabuto na serikali yake kuwa ya kula bata Ufaransa na kwenye mahoteli makubwa huku machawa wake wakiwa wanajiona wapo peponi . Mabeberu wakaigawa nchi kwa kutumia pesa zao.
Leo tunaiona safari ya Kuelekea kule kule Kongo ikifanywa na hawa watawala halafu hatushtuki kutokana na misaada na maslahi ya wachache na machawa wakila bata huko Dubai na marafiki zao wa nje. Wageni wanazidi kujiimarisha kiuchumi kwa kudhibiti vyanzo vikubwa vya mapato kama Bandari , Viwanja vya ndege,misitu ,ardhi ,madini ,wanyama n.k. Wanajiingiza kwa misaada ya kuwaimarisha mqwakala wao kwenye siasa na dini pia ili watanganyika enye kuona mbali watakapo wakataa waingize itikadi za kidini kuwa wanakatalowa kwa sababu ni wa dini fulani .
Kuna siri kubwa sana zinazofanywa na wafanyabiashara wa kubwa wa kimataifa bila kujali haki na ustawi wa watu maskini katika nchi zao za asili.
Ndio maama hawa mawakala wao wanakusanya mali nyingi sana kwa muda mfupi na kujiweka kwenye kiwango cha mattajiri wa dunia kwa haraka.
Tukiwa na katiba hii ya kimungu hata akishinda Tundu Lisu ambaye kiuhakika atamshinda kwa mbali sana Mgombea wa CCM endapo wataamua kulinda kura kwa jasho na damu ,jambo ambalo hatulitaki na ndio maana tunasema uchaguzi usifanyike bila katiba mpya ,bado akiingia madarakani atanogewa na madaraka makubwa na fursa za kujineemeha na marafiki zake na ndugu zake na pia kuwakaribisha Waneligiji waliomsaidia kuokoa maisha yake . Bado tutarudi kule kule kwenye utawala wa kihuni wa CCM wa kuuza nchi kwa Wageni.