Niaje niaje?
Moja Kwa moja kwenye mada kuu, napenda kuwapongeza WATANZANIA wenzangu Kwa kuwa wazalendo kabisa. Bila shaka ninyi ni mashujaa na wa kweli kabisa katika maisha ya kawaida ndio, lazima tuseme ukweli panapohitajika uwezi kupata ubunge ukalipwa posho zako ukasahau walio kupigania uupate, hii ni dharau. Kira siku ni kujipost tu uko mtandaoni mkijidai na kujitapa kama ninyi ni matajiri wakubwa mnashinda kuvaa gold kwenda kwenye mahotel makubwa na familia mkijiona Bora kabisa ndio.
Una magari sita sijui matano yote umeweka majina yako kwenye kwenye plate number ambayo unalipia Kira moja karibu milioni kumi Kwa mwaka wakati aliye kupambania ubaki kwenye madaraka bima ya afya ya elfu arobaini tu hana, na uko comfortable kabisa kujimwambafai kwa visuti vyako vya sinza kijiweni na vimoka vyako vya kariakoo sokoni.
ASANTE WAJUMBE KWA KUTOWAPIGIA HAWA MABAZAZI WAKUBWA, unajifanya unatupigania huku watoto wako wanasoma international schools Sisi wetu wanasoma changanyikeni haafu unasema tuko sawa wewe ni TAAHAHIRA MKUBWA.
SASA KWA TAARIFA YAKO HATUANDAMANI TUNAUNGA JUHUDI LIWALO NA LIWE. WEWE UKIONA HAPA PAGUMU HAMA NCHI MWANASESERE WEWE.
Nawasilisha