Nsanzagee
JF-Expert Member
- Jun 28, 2023
- 2,209
- 4,769
- Thread starter
- #61
Unajua mkuu, wewe unakuwaga na hoja na huwa ninakukubali sana!Simu ilizingua.
Nasema hivii.
CCM hata ya Magufuli ilishindwa, ndiyo maana haijaleta mabadiliko ya kimfumo.
Sasa kwa nini tunalinganisha CCM iliyoshindwa na CCM iliyoshindwa badala ya kuweka standards za uongozi mzuri na kutaka tuzipate kutoka kwa yeyote?
Kwa nini tunashindwa kufikiri kidhahania na kusema uongozi mzuri ni ule utakaotupa hiki, na hiki na hiki, hata kama hakipo?
Kwa nini tunaona ili kulinganisha uongozi, inatubidi tulinganishe uongozi mmoja ulioshindwa na mwingine ulioshindwa?
Kwa nini tunalinganisha failure na failure badala ya kuweka viwango vizuri, hata kama hatujavifikia, halafu tulinganishe uongozi wetu ulioshindwa na uongozi wa viwango vinavyotakiwa, hata kama hatujavifikia bado?
Hasa unapoongelea mifumo! Hilo nakuunga mkono, kwenye hilo, naliona kosa kubwa la JPM la kutokuweka kuw mfumo ambao kila kiongozi atakayekuja, aongozwe na mfumo na siyo yeye kuiendesha mifumo atakavyo
Tunataka mfumo wa kufuatwa na kila kiongozi ajaye na siyo mtu kuwa yeye ndio mfumo