Tetesi: CHADEMA ‘Nusu Mkate’ wote wanahamia CCM February 5 akiwemo Wenje, Sugu na Boni Yai

Kulazimishwa vikiambatana na vitisho kuelekea fursa, unakumbuka issue ya Nusrant Hanje kutolewa gerezani akiwa na kesi mahakamani hadi kuapishwa kuwa Mbunge?.
Bro wewe pengine hujui mwanasiasa msaka fursa yupoje. Niambia wake wake wa kigaila kina kunti majala, matiko, bulaya walitishwa na nani? Au niambie ally bananga mmoja wa kampeni meneja wa lissu 2020, alitishwa na Nani kwenda ccm? Mwanasiasa msaka fursa anaisaka fursa kwenye angle nyingi, msigwa katishwa na nani? Ndio maana nakuambia hizo sio sababu za mwanasiasa kuhama
 
Tusubiri tuone mkuu
 
Tusubiri tuone mkuu
Hata asipohama hiyo tarehe 5, but hawezi kubaki chadema muda mrefu. Hakuna namna yoyote sugu anaweza tena kuaminiwa na chadema iliyopo sasa

Lema with confidence alisema uchaguzi wa nyasa ambao sugu alishinda ulikua mbovu kuliko hata wa Tamisemi. Tusiukimbie ukweli sugu alichofanya kwenye uchaguzi wa nyasa ilikua kitu Cha ajabu. Unahisi kwa nini lissu na lema hawakulalamika sana uchaguzi wa wenje Kanda ya Victoria?
 
Wengi walivofurahia ushindi wa Lisu sio Kwa sababu Lisu yupo vizuri apana watu walitaka waone makanjanja kama hawa, watu wanaohadaaa wananchi Kwa siasa uchwara, watu wanaofanya uwinga wa kisiasa na wengine wote waliopo kwenye vyama Kwa hila flani
Mkibosho umenena vema.
 
Sina data kamili lakini nguvu ya Sugu ilikuwa inatoka HQ kwa kina Mrema na genge lake ambao leo hawana nguvu tena
 
Mbowe akikaa akatulia atagundua timu ake ilikuwa ya hovyo sn
Tatizo kubwa la mbowe kwa timu yake ni kuwapa maslahi, ni kitu kizuri lakini mtu unayempa maslahi sana ni rahisi kuwa compromised kwingine. Mbowe alikua anampa boni magari, alikua anampa mallya magari, hivi watu wa hivyo waliokua wanapata mtelezo wataishi vipi tena kwenye hiyo taasisi? Si ajabu walilia sana kama boniyai alivyosema
 
Nashukuru kuweka kumbuka sawa, lakini hoja ya Uchaga ilikita mizizi Chadema labda kwakuwa Mwenyekiti aliyemaliza muda wake alikaa miaka mingi madarakani
Hoja hiyo imekufa hoja wanayoifanyia kazi kwa sasa ni kuwagombanisha Wakatoliki na Walutheri na madhehebu mengine.
 
Wakubali matokeo, ni sawa na mtu kufiwa na mzazi wako utaumia lakini mwisho utazoea
 
Sugu hawezi kuwa mjinga kiasi hicho, pesa anayoingiza kwa mwezi ni zaidi ya 20M kwenye biashara kuliko akahangaike na salary ya 4.6M atakuwa ni mwenda wazimu haswa.
Sugu hamshindi Msando Kwa chochote Lakini Wakili Msomi Msando ni DC
 
Sina data kamili lakini nguvu ya Sugu ilikuwa inatoka HQ kwa kina Mrema na genge lake ambao leo hawana nguvu tena
Wala sio suala la data, kilichofanyika kilikua hadharani, rushwa ilitolewa sana. Mbowe aliwekwa vikao zaidi ya mara moja kuingilia Kati kinachotokea nyasa, akashupaza shingo
 
Je na vipi ukapata kujua ccm mboga saba wote nao watahamia kwa jirani katika muda muafaka,hapo vipi?
 
Sugu hamshindi Msando Kwa chochote Lakini Wakili Msomi Msando ni DC
Msando namfahamu vizuri sn hana mali kama unavyodhani kumshida mtu ambaye amekuwa mbunge kwa miaka 10 + biashara, mbunge akiwa siyo mla rushwa for 5 years hakosi 2B, kwanza anapewa mkopo na hazina 1B nusu anakatwa na nusu analipiwa na bunge, mbunge likivunjwa hakosi 300M, bado vikao, safari, GSM huwezi kumpa hata kuwa Gavana lakini ubunge atakubali sababu ndiyo kuna hela zipo nje nje
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…