Uchaguzi 2020 CHADEMA: Tunamuunga mkono Maalim Seif kwa Urais Zanzibar. Lissu hataendelea na kampeni, atapangiwa majukumu mengine

Uchaguzi 2020 CHADEMA: Tunamuunga mkono Maalim Seif kwa Urais Zanzibar. Lissu hataendelea na kampeni, atapangiwa majukumu mengine

Vyama vilivyokataa Lissu aendelee na kampeni navyo vimeambiwa vinapokea maagizo ina maana CCM wana nguvu
 
Mbowe ni Mtanzania...siyo kibaraka wa mabeberu Kama Lissu...anatanguliza Tanzania Kwanza...Lissu anamtanguliza Amsterdam na mabeberu wengine...
Mbowe ni Mzalendo, hayuko tayari kuona damu za watanzania zinamwagika sababu ya kulazimisha kuingia Ikulu. Historia ya Tanzania itamkumbuka daima. Sio wale jamaa na Lisu wao wanaotamba kuingiza nchi kwenye machafuko wabebe madini na rasilimali za Tanzania.
Queen Esther
 
Unafikiri hawajui matendo yenu??? Unafikiri hawajui kuwa mnaua ili kutengeneza balance badae??? Unafikiri hawajui kuwa kila kesi inayotokea saivi mnawapa Chadema ili kubalance tuhuma???!

Subirini tu😂😂😂😂✌
Umeweka upuuzi hapa....hivi kiwango chako Cha elimu kikoje?! It is no wonder unashabikia mauaji...yaani CCM hii iue watu eti ili kubalance mauaji..what a stupid comment?! Yaani mmeishiwa hoja...yaani mmekaa kusubiria mabeberu eti wachukue hatua...ndiyo maana nyie wenyewe mnachoma ofisi za chama chenu ionekane kuwa ni CCM au serikali..very stupid indeed...yaani mmewaua wale vijana kikatili Sana...na damu yao itawaandama kokote muendako...Kama kweli wewe ni jasiri jitambulishe hapa ufahamike ...
 
Hivi unadhani anachosema huyo jamaa hakifahamiki na hizo ngazi za juu? Hizo ngazi za juu wanajua sana na wao ni sehemu ya hayo maagizo ili wapate hela.


Sidhani mkuu ila naamini kuna baadhi ya watendaji wana 'take advantage ' kupitia mpango wa kukomesha uvuvi haramu
 
*CHADEMA PUMZI IMEKATA*

Baada ya akusikiliza kwa makini hituba ya Mbowe yangu ni haya yafuatayo:-

1. Mhe. Mbowe unaposema chama chenye ushindani na CCM ni Chadema peke yake huoni unadhalilisha vyama vingine vya upinzani?. Hata Chadema ilianza mdogo mdogo leo ipo hapo ilipofikia. MBONA UNAUA DEMOKRASIA YA VYAMA VINGI?

2. Mhe. Mbowe unaposema kura za vyama vitatu tu kati ya vyama karibu 17 ndio vimepinga kusimamishwa kwa Lissu huoni hiyo ni DEMOKRASIA??? Mbona unaikosoa tena!

3. Mhe. Mbowe! Kwanini mmeamua kuungana baada ya kuona maji yapo shingoni? Mhe. Membe alisisitiza sana muungane mkamgomea! Leo uchaguzi umebaki siku 24 na mmeambiwa maandalizi yamekwisha ndio mnaungana?! Huko ni kutafuta nongwaaaa baada ya kuona mmeshindwa!! Waliokiunga CCM mkono walifanya hivyo kabla kipenga hakijapulizwa. Sasa kipenga kimepulizwa imebaki kama robo kazi iishe mnataka kuungana!! Mwogopeni Mungu wajameni!!

4. Hatujaona mahali mnakemea wana CCM wanaouliwa na kujeruhiwa na wafuasi wenu. Mkt wa CCM Taifa Dr. Magufuli aliwatangazia wanachama wake kisasi ni cha Mungu!! Akaonya wasilipize kisasi!! Huo ni uungwana wa hali ya juu.

5. Ratiba za kampeni kila chama kilipeleka chenyewe kwenye Tume. Leo unalalamikia ratiba uliyotengeneza mwenyewe!! Mambo ya ajabu kabisa na ni kuleta vurugu kwenye nchi!! Mlipoanza mashindano mlikutanishwa wote na mkasaini, leo unasema huyu atolewe! DEMOKRASIA gani hiyo! Hivyo vyama navyo vina fursa na vitakua kama Chadema. Kumbuka kulikuwa na chama chenye nguvu kabla ya Chadema na hawakusema Chadema inaunga mkono CCM.

6. Kila chama kiliwasilisha Tume majina ya watakaopiga kampeni. CCM iliwasilisha majina na Waziri Mkuu ni Mjumbe wa Kamati kuu na jina lilipendekezwa na anapiga kampeni. Sasa nini kinakusumbua?? Mbona Chadema mmetengeneza orodha yenu na hakuna anayewauliza?

Mwisho niseme tu! Tayari mmeona uwezekano wa kushinda ni sawa na ngamia kuingia kwenye tundu la sindano mmeanza kutoka kwenye hoja mpo kwenye viroja! Mnahubiri kusimamia sheria leo mnataka Tume ipindishe sheria. Mlimuacha Lisu aropoke badala ya kunadi sera sasa jahazi linazama!! Bora mngemsikiliza mzee wangu Mhe. Membe!! JITAFAKARINI!! WATANZANIA HAWATAKI VURUGU!!! SANDUKU LA KURA LIACHWE LITAAMUA!!! DEMOKRASIA IACHWE ICHUKUE MKONDO WAKE!!!!
 
Safi sana waheshimiwa kwa kukwepa huu mtego, tusiruhusu TUME kupata kisingizio cha kufanya hujuma zaidi kwa mgombea wetu. Mwenyezi Mungu atatenda muujiza na hujuma zao hazitsaidia. Kule kwao maji yapo shingoni, Mheshimiwa TAL kaza buti, wale wameshalegea, WATAACHIA mapemaa!
 
Kuna msuguano mkubwa sana kati ya Lisu na Mbowe. Mbowe akimtuhumu Lissu kuwa amepewa pesa na watanzania wanaoishi nje ya nchi pia na Mabeberu yeye akiziminya na hakuzitoa ili zitumike katika kampeni. Nae Tundu akimtuhumu Mbowe kuwa pesa za michango ya wabunge za kila mwezi Mbowe hazitoi ili zitumike katika kampeni.

Mvutano huo ndiyo unaopelekea utofauti wa majibu ya Mbowe na Lissu. Hata kampeni wamemsusia nae Tundu alisusa kwenda katika jimbo la Mbowe (Hai).

UKIMWANDIKA KWA MABAYA TUNDU UNAFUNGIWA JF
Heee! Hii JF ya Mzalendo wa kweli Max Demelo!! Heeee!! kweli!! Ngoja tuone!! Mbona Magufuli anatukanwa humu sana tuu na watu hawafungiwi? Ngoja tukodoe macho!!
 
..wakati bado haujafika.

..wananchi wakichoshwa, cdm, act,ccm,... wote watawekwa pembeni.

..tatizo ni kwamba ccm hawaioni HATARI hiyo.
Demokrasia imekwama sio tu kwa chama tawala bali na vile vyama viranja vya upinzani.
Tukisubiri kuletewa demokrasia na hawa wachezaji butu tutachelewa kuchukuwa kombe.
Turudi kwanza kwenye drawing board ya demokrasia na katiba.
Tukimaliza hilo ndio tufanye Uchaguzi mkuu.
Vyama vya siasa kwa sasa sio muarobaini wa uchaguzi huru na haki ni maigizo tu.
CCM nayo ni kubwa mno kujisafisha na hilo ni tatizo kubwa kwani yeye kageuka kama bidhaa za Azam yupo kila pahala.
Mchango wa mgombea binafsi ni muhimu kwa kuwaengua vyama maslahi.
HIzo nyege za wapinzani kujitundika kwenye uchaguzi mkuu kila miaka mitano huku wakijua wanaabulia patupu, bila tume huru ni fedheha kwa umma wa Tanzania.
 
Safi sana waheshimiwa kwa kukwepa huu mtego, tusiruhusu TUME kupata kisingizio cha kufanya hujuma zaidi kwa mgombea wetu. Mwenyezi Mungu atatenda muujiza na hujuma zao hazitsaidia. Kule kwao maji yapo shingoni, Mheshimiwa TAL kaza buti, wale wameshalegea, WATAACHIA mapemaa!
Tuambie mgombea wenu kwanini kila siku anaongea uongo na hamumkemei? Atoe ushahidi Wakurugenzi kuitwa Ikulu! Mbona hiyo hoja haijibiwi?
 
Alivyotepeta kwa tume ndo atakavyotepeta baada ya uchaguzi,la muhimu ni kutii sheria bila shuruti.
Lissu akiambiwa awehanasikia na anaelewa hawezi kushindana na dola.
 
Kuiitii hii amri batili na ya kifedhuli ya NEC CCM ni ujinga na ni sawa na kukubali mapigo yajayo
 
"Jifanye mjinga siku ipite," "funika kombe mwanaharamu apite"ni uamuzi wa hekima na mwiba mkali kwa ccm.
Mda huu chadema wautumie kuujulisha Ulimwengu wote taasisi zote za haki za binadamu na pia wasake ujuzi Malawi Zambia kenya congo Ghana Gambia wajue mbinu walizotumia kuondoa shetani Nchi mwao wazitumie kuondoa ushetani wa CCM
 
Umeweka upuuzi hapa....hivi kiwango chako Cha elimu kikoje?! It is no wonder unashabikia mauaji...yaani CCM hii iue watu eti ili kubalance mauaji..what a stupid comment?! Yaani mmeishiwa hoja...yaani mmekaa kusubiria mabeberu eti wachukue hatua...ndiyo maana nyie wenyewe mnachoma ofisi za chama chenu ionekane kuwa ni CCM au serikali..very stupid indeed...yaani mmewaua wale vijana kikatili Sana...na damu yao itawaandama kokote muendako...Kama kweli wewe ni jasiri jitambulishe hapa ufahamike ...
Bila mabeberu kuchukua hatua hii nchi itafika hatua kama Iddi Amini alivyokuwa Uganda. Ni bora mabebeberu wachukue hatua sasa maana tumechoka watu kuuawawa na kuteswa kwenye nchi yao
 
Haki haipatikani bali kwa ncha ya upanga.
Mkurugenziccm wa Tumeccm na polepole huwa hawatambui kuna maisha baada ya uchaguzi hawajui kuwa endapo malaika atazuia mbinu zao za hovyo hatimae chadema kuingia ikulu watakuwa na vya kujibu baadae, hawajitafakari kabla ya kutenda ushetani wao
 
Wakati mwingine ukishupaza shingo sana huwa linavunjika

NEC na kamati yao ile wanatafuta sababu ya kutoa adhabu kali zaidi na CHADEMA watafanya makosa makubwa kuingia huko mkenge. Ndio maana imebidi busara itawale zaidi na jazba ikae kando
Chadema mmekamatika, ninyi hamnaga busara kama mnajua mko sahihi. Mgombea anasema lake, mwenye chama anasema lake upuuzi mtupu. Hamjajipanga kushinda, na mjiandae kujiunga na wenzenu TLP.
 
Kwa mujibu wa Tumaini Makene:

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe. Freeman A. Mbowe leo Jumapili, Septemba 4, 2020, saa 7 mchana atatoa tamko, kupitia Mkutano wa Waandishi wa Habari, kuhusu maazimio ya Kikao Maalum cha Kamati Kuu ya Chama kilichoketi jana na kumalizika usiku jijini Dar es Salaam.

Asanteni.
========

7:45 mchana: Mambo yanawekwa sawa tayari kwa mkutano wa waandishi wa habari

7:53 mchana: Viongozi wakuu wa CHADEMA wamefika na mkutano kuanza


Mbowe: Ninapenda kuwaeleza watanzania kupitia ninyi waandishi wa habari mambo kadha wa kadha yaliyojiri katika kikao chetu cha kamati kuu ya chama kilifanyika katika ukumbi wa Bahari beach hotel siku ya jana kuanzia asubuhi hadi usiku wa manane.

Kikao kilikuwa na agenda mahsusi moja ambayo ni kujadili mwenendo wa uchaguzi mkuu Urais, wabunge, Rais wa Zanzibar, wawakilishi pamoja na madiwani wote kwa upande wa Tanzania Bara na visiwani.

Kamati kuu imeridhika na mwenendo wa misafara ya kampeni ya mgombea wetu wa Urais na mgombea mwenza ukiondoa matukio machache ya kidhalimu yaliyofanyika katika maeneo ya Nyamongo kwa upande wa mgombea wetu wa Rais na tukio la msafara wa mgombea mwenza kupigwa mabomu katika mji wa Ifakara.

Pili kamati kuu imeitafsiri sana na kuitathmini tume ya Taifa ya uchaguzi na baadhi ya maamuzi yake na mwenendo wake. Kamati kuu imesikitishwa na kitendo cha tume ya Taifa ya uchaguzi kuengua wagombea 36 wa ubunge, 35 wakitoka Tanzania Bara na mmoja kutoka visiwani na kuengua wagombea udiwani wetu 577.

Tunatambua kwamba uchaguzi wote husimamiwa na sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa, vilevile tunatambua sababu mbalimbali zilizotolewa na tame hazina mashiko ya kisheria, hazina mashiko ya kimantiki, zinavunja mfumo wote wa kidemokrasia katika nchi.

Kwamba wagombea wote wa CCM hakuna hata mmoja aliweza kuenguliwa hata wale ambao sisi tulikata rufaa dhidi yao kwa makosa ya msingi na wazi.

Kamati kuu imejiridhisha tume hii ya uchaguzi ni chombo na kinacholindwa makusudi kulinda chama cha Mapinduzi na serikali yake.

Tume imetoa adhabu mbalimbali zisizo za msingi, zisizo za kidemokrasia bila kutia maanani kipindi cha uchaguzi ni kipindi kifupi sana.

Kipindi cha kampeni, kwa mfano mgombea wa CHADEMA wa kiti cha ubunge cha Ubungo, baada ya mchakato kuanza alikatiwa rufaa kwa hiyo hakuruhusiwa kufanya kampeni kwa wiki mbili na nusu kwa sababu ilikuwa haijatoa rufaa yake, baada ya wiki moja, chama cha mapinduzi kikakata rufaa na tume tena ikamsimamisha kwa wiki nyingine moja, unamchelewasha kwa wiki tatu.

Mgombea wetu wa ubunge Same Magharibi alifungiwa kwa wiki mbili, hatujasikia mgombea wa chama cha mapinduzi akisimamishwa pamoja na uharamia mwingi.

Tume imeendelea kuchelewesha majibu katika majimbo kadhaa, jimbo la Iramba Magharibi lenye mgombea Jesca Kishoa, dada makini kabisa, madiwani wake wote wameenguliwa katika uchaguzi kwa sababu ambazo hazina msingi kabisa.

Tume hii inachochea misingi ya kuleta machafuko katika Taifa kwa sababu siku zote tunasema, uvumilivu una mwisho. Kwa hiyo kuna wagombea wetu hawajapata majibu wakati asilimia 50 ya muda wa kampeni umeshapita.

Tumepeleka malalamiko kadhaa ya makosa ya msingi yanayofanywa na wagombea wa chama cha mapinduzi kwa tume tukilalamikia masuala ambayo yanakatazwa kisheria.

Kwa mfano, katika kampeni watumishi wa serikali ikiwemo Rais, waziri mkuu, mawaziri au watendaji wowote hawaruhusiwi kutumia ushawishi wa miradi au kutoa maelekezo ya ujenzi wa miradi mbalimbali katika kampeni.

Tunaona Rais anaagiza bila woga, waziri mkuu anaagiza bila woga. Tumelalamika tume ya Taifa ya uchaguzi lakini Tume haichukui hatua yeyote.

Tumemuona Rais mali za serikali, magari ya serikali yaliyobadilishwa rangi na kuwa rangi ya kijani na kuwekwa namba za chama cha mapinduzi, yale yote ni magari ya Ikulu. CCM hawajaagiza gari hata moja, yale ni magari ya Ikulu na kama CCM wanapinga watoke hadharani na document hizi hapa.

Tumeona msafara wa Rais una magari zaidi ya 80, magari zaidi ya 50 ni ya serikali au watendaji wa serikali. Hii ni unfairness kwa sababu unampa Rais msuli wa serikali inayoendeshwa kwa kodi za wananchi wote.

Walimu wanalazimishwa kwenda kwenye mikutano ya chama cha mapinduzi, hatuna tatizo CCM wakiwaalika wasanii, ile ni initiative yao lakini waalimu wa nchi yetu ni watumishi wa Umma, wanafunzi ni watoto wa watanzania mbalimbali wakiwemo wa chama cha mapinduzi, vyama vya upinzani.

Tumeona vyombo vya habari vya umma kama TBC vinamtangaza Magufuli asubuhi mpaka asubuhi, magazeti ya umma. Mamlaka nnyingi za kiserikali, TCRA ikifanya kazi kubwa ya kujaribu kudhibiti matumizi ya mitandao na kunyima uhuru wa watu kupokea habari.

USHIRIKIANO WA VYAMA
Tumesikia viongozi kadhaa wakizungumza dhana ya ushirikiano wa vyama na tumemsikia msajili wa vyama vya siasa akitokeza hadharani akisema nyinyi hamruhusiwi kuunga mkono chama kingine, muda umeshapita, haya ni mambo ya kusikitisha sana.

Hauwezi ukanitungia mimi sheria ya kujenga mahusiano na rafiki ama kujenga uadui na mtu, hayo ni mahusiano ya watu na watu.

Wamekuwa wakipinga kauli zozote zinazoashiria ushirikiano wa njia yoyote kati ya CHADEMA na ACT lakini wakati huo huo akifumbia macho viongozi wa hivi vyama pandikizi vya upinzani kama TLP au UDP vikitoka na kumuunga mkono Magufuli.

Msajili anatamani kuona nchi hii inatawanyika vipande 40, sisi tunatamani kuona watanzania wanajumuika pamoja kutengeneza force za kisiasa aidha za upinzani au za chama tawala zenye nguvu ya kupingana kwa hoja.

Kamati kuu baada ya kushauriana kwa kina na mgombea wetu Urais wa Zanzibar, tumeona ni sahihi kabisa kwa chama chetu kumuunga mkono Seif Sharif Hamad, mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama cha ACT kwa hio mgombea wetu ameridhia kujitoa yeye mwenyewe kwa mapenzi yake, taratibu zake za kujitoa zitafata.

Kamati kuu imeridhia kuendelea na mazungumzo kuungana mkono kwa baadhi ya kata hata majimbo ambayo tunafikiri tukiweza kumuunga mkono wa chama kingine mwenye nafasi zaidi tunaweza tukapata muwakilishi alie bora zaidi wa eneo hilo.

KUZUIWA MIKUTANO KWA MGOMBEA URAIS
Tume ya taifa ya uchaguzi kumzuia mgombea wetu, nimeshazungumza kuhusu tume kuwa mchezaji na refarii. Awali mheshimiwa Lissu alisema ataendelea na mikutano yake ya kampeni ambayo kimsingi ni haki yake lakini akasema uamuzi wa mwisho anaiachia kamati kuu ya chama chetu. Tumekubaliana tufanye yafuatayo

Kwa sababu tunatambua nia na dhamira mbaya ya tume ya uchaguzi, kwa sababu tunatambua sababu mbalimbali zisizo na maniki sana zinazotafutwa kujaribu kumkwara zaidi mgombea Urais, tumeamua kutowapa fursa hawa tume ya Taifa ya uchaguzi.

Hata kabla sijaeleza maamuzi yetu, naomba nieleze ni nini kilifanyika, tumepokea hukumu kutoka tume ya Taifa ya uchaguzi, katika kujitetea kwake, tume ya Taifa ya uchaguzi pamoja na mambo mengine kadhaa ijaribu kujenga dhana kwamba adhabu iliyotolewa haikutolewa na tume, imetolewa na vyama vingine vilivyoshiriki uchaguzi huu.

Fair enough lakini mwenyekiti wa kikao na katibu wake ni watendaji wakuu wa tume kwa maana hiyo wanarusha lawama kwamba hawakuamua wao, waliopiga kura ni vyama vyenyewe vya siasa.

Tuna vyama 15 vilivyoshiriki kikao hicho(Anavitaja) na katika kura 15 zilizopigwa, kura tatu zilikataa kumfungia mheshimiwa Lissu mikutano yake lakini kura 12 ya hivi vyama vilivyopiga kura eti ya kumuengua mheshimiwa Lissu asiendelee na kampeni.

Huu tunajua ni uamuzi wa chama cha Mapinduzi kwa kuvitumia hivi vyama, sisi kama CHADEMA tunapinga hukumu hii.

Tumemshauri mgombea wetu asiendelee na mikutano kwa hiyo mheshimiwa Lissu hataendelea na mikutano ya kampeni kwa kipindi hiki ambacho tume imezuia mikutano yake.

Tundu Lissu sio tu ni mgombea Urais wa chama chetu, huyu ni makamu mwenyekiti wa chama na chama hiki kina kazi kubwa za kufanya, za kisiasa na za kijamii kwa hiyo Tundu Lissu hatakosa kazi ya kufanyakwa kipindi cha siku saba.

Chama kitampangia program mahsusi kama makamu mwenyekiti wa chama kufanya majukumu ya kijamii na kisiasa katika maeneo ambayo chama kitapanga.
Ni uamuzi wa busara sana. Walichokua wanakitafuta mabwana wale hawajakipata na hawatakipata
 
Wametangaza kushirikiana.

Namuona mahera na lafudhi yake akikandamiza maneno kupinga urafiki wa chadema na ACT-WAZALENDO na akihekelea urafiki wa UDP, TLP na CCM
 
Back
Top Bottom