Chagua mwanamke mwaminifu usije ukaumia kwa kufanya kosa kama wanaume wengine

Chagua mwanamke mwaminifu usije ukaumia kwa kufanya kosa kama wanaume wengine

Infinite_Kiumeni

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2023
Posts
382
Reaction score
687
Ili kujenga mahusiano mazuri kwanza hakikisha wewe ni mwaminifu. Ukitaka kuwa na mahusiano mazuri hakikisha uliyenaye ni mwaminifu. Kwetu wanaume kitu cha kwanza muhimu ni mwanamke mwaminifu.

Uaminifu unajumuisha; kusema ukweli, kuwa na mtu mmoja (kuto saliti), kumuamini mwenzako, kuhifadhi siri za ndani, na kufanya kinachotakiwa kufanywa/ulichosema unakifanya.

Hakikisha kwanza wewe una uwezo wa kuwa mwaminifu, kisha ndio umjaji mwanamke wako. Lakini kama mwanamke uliyenaye hana sifa za kufanya vitu hivyo, inabidi ujiulize tena kama upo na mtu sahihi.

Kosa linalofanywa na wengi ni kuamini kuwa ukiwa naye utaweza kumbadilisha. Sio kweli, hakuna mtu anayeweza kumbadili mwingine. Mtu anabadilika anapotaka mwenyewe. Watu wengine ni wa kumsaidia tu ili abadilike.

Usizame mazima kwa mwanamke. Anza kwa kujuana naye kwanza. Ukiona mambo ambayo huwezi vumilia ni heri uachane na huyo mwanamke mapema. Kabla hujawekeza hisia sana kwake. Ikifikia hatua umeshazama mazima, ni ngumu kuachana naye.

Utajikuta unajipa moyo “Ah, ipo siku atabadilika, nitamfundisha atabadilika,” sio kweli. Mtu akikuonesha jinsi alivyo, mwamini. Hauna haja ya kujidanganya. Usije ukaishia kusalitiwa, kuumia na kuona wanawake wengine wote ni wabaya.

Share Na Wengine Wapate Kujifunza.
 
Kila mtu ni mshauri mapenzi tu
 
Ili kujenga mahusiano mazuri kwanza hakikisha wewe ni mwaminifu. Ukitaka kuwa na mahusiano mazuri hakikisha uliyenaye ni mwaminifu. Kwetu wanaume kitu cha kwanza muhimu ni mwanamke mwaminifu.

Uaminifu unajumuisha; kusema ukweli, kuwa na mtu mmoja (kuto saliti), kumuamini mwenzako, kuhifadhi siri za ndani, na
People change...hata ukimuoa akiwa bikira. anaweza akabadilika mpaka ukashangaa
 
Kwenye mahusiano hakikisha unapata wa kufanana nae tu, mengine mbwembwe.

Mkifanana tabia zenu, mambo yenu, mtaenda sawa.

Sasa mfano unataka upate mtu sio msaliti ila wewe msaliti, au asiyemuongo wakati wewe muongo. Hamfiki mbali. Pata msaliti mwenzio au muongo mwenzio.
 
Hata huyo Mwaminifu ukimpata halafu ukaja kumvuruga anaweza kubadili tabia! [emoji848]
 
People change...hata ukimuoa akiwa bikira. anaweza akabadilika mpaka ukashangaa
Well stated!
Tabia za binadamu hubadilika kulingana na mazingira na wakati - image vikoba leo vinavyowahangaisha wanakikoba
 
Back
Top Bottom