Chakula gani ulikula mara moja na kwa mara ya kwanza hadi leo hutaki tena kukila?

Chakula gani ulikula mara moja na kwa mara ya kwanza hadi leo hutaki tena kukila?

Uko sahihi Daby; chakula kinategemea upikwaji wake. Ukila kwa mara ya kwanza chakula kilichopikwa vibaya, hutakaa ule tena chakula hicho ukijua daima ni kibaya.
Ni Kama Mimi nisivyopenda maboga.... Ingawa watu wanayasifia kweli..... Mimi Mara ya kwanza kula boga lilikua bayaaaaaa
 
Mm ile mboga ya majani inaitwa kisamvu, nilikula nikavimba mwili ,hadi leo nikikuta iko mezani mm lazima ninyanyuke,
Nashauri wabadiri hilo jina
 
1.KAHAWA

kuna jamaa zangu wengi hupenda kweli kahawa,namimi ki ukweli napenda sana ile harufu yake tena nikiona na zile kashata huwa natamani kweli,siku 1 namimi nikasema haiwezekan kila siku nile harufu,Akapta muuza kahawa "nikamuita" kwa kujiamini kama vile member kbsa, akaja nkamwambia "weka kahawa hapa bwana mkubwa" Akanimiminia.

akanipa na kashata zake nikachukua 1,nikatia mdomoni mdomoni "bwana weeee" ilikua chungu hiyooooo haimezeki yani bahati yangu ilivyokua mbaya nilikaa sehemu ambayo hamna hata pakutemea.kote kulikua na tyrese tena nyeupee,asee nilijitahd kunywa ile kahawa ila sikuweza pga hata pafu lingine,muda huo nakunywa kashata yangu mkononi "nishaimaliza mudaaa" ila kakikombe ka kahawa kamejaa full,wenzangu washaongeza round mbili mi npo tu.

nikawa natafuta namna ya kutoka pale nisogee pembeni nikaimwage ie kahawa,ikabd nitege Alarm ya dk 3 nikakaa simu ikaita nikajifanya nimepokea nkainuka nikasogea kwenye mchanga nkamwagilia mbali kahawa lao.
[emoji1][emoji1][emoji1] Kama nakuona
 
Hivi huu ni ushamba ama ni nyodo za kula?
Tikiti maji linakushindaje?
Wakati nipo chekechea ndiyo niliyajua matikiti, niliyakuta nyumbani siku hiyo. Nilikula, hata sikumaliza kipande nikaanza kutapika.

Hali iliendelea mpaka nikapelekwa hospitali. Hakuna aliyefikiria sababu inaweza kua matikiti, so siku nyingine yakaja tena, ikajirudia tena hali ileile na kutapika kwa nguvu. Baada ya kupona hapa ndiyo hata harufu yake imekua inanishinda.

Hivyo ikawa ishajulikana kwamba kwangu mimi matikiti siyawezi.

Hivyo siyo ushamba wala nyodo ni swala la uhai au ugonjwa.

Hata hivyo juisi yake ikichanganywa na matufaa naweza kuinywa.
 
Back
Top Bottom