Kinoamiguu
JF-Expert Member
- Nov 29, 2018
- 11,936
- 15,196
Ukifuatilia sana hauzi hata vocha
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Acha kuleta mifano ya kibwege.....kwaheri maana nikupoteza muda ku-argue na bongo lala asiyejua msingi wa maduka kufungwaBora kuwa na funza kuliko kujaza kamasi na kuchekea wapuuzi wanaoleta siasa kwenye uchumi.
Wahujumu uchumi haipaswi kuwachekea,Kagame au Museveni hawezi chekea huu utaahira.
Wakamatwe waburuzwe kizimbani Kwa uhujumu uchumiAcha kuleta mifano ya kibwege.....kwaheri maana nikupoteza muda ku-argue na bongo lala asiyejua msingi wa maduka kufungwa
Kwani Toka wameanza kunyongwa Wala Rushwa wameisha? Acheni ujinga wa kuhujumu uchumi Kwa siasa nyepesiNdio nimekuambia nenda China halafu ukale rushwa ndio utajua wananyonga au hawanyongi.
Unajua maana ya uhujumu uchumi?Wakamatwe waburuzwe kizimbani Kwa uhujumu uchumi
Eti nini?Sio kweli Kila mtu taarifa zake zipo kuanzia za kibayometric Hadi za physical,huwezi Anza kutanga Tanga kushindana na Serikali kisa unafanya siasa za ujinga.
Bora ujinga huo wa Serikali kuliko fedheha.Wafanyabishara wa Kariakoo wasijifanye spesho sana,Nchi hii inaweza enda bila hao wajinga.
Aggrey Mwanri apewe ukuu wa mkoa wa Darisalamu, hao wafanyabiashara angewachota wote na kuwasukuma ndaniMkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amefika soko la Kariakoo kutokana na Biashara kufungwa kuanzia leo Juni 24, 2024 na kuongea na wafanyabiashara.
Chalamila amesema wafanyabiashara wako wa aina kadhaa ikiwemo walioshiba, kati na wachanga na iwapo wataigana kuna watakaojuta leo, kesho na mwingine baaada ya mwezi mmoja. Chalamila amesema ni kweli wafanyabiashara wanaweza kuwa na changamoto lakini zipo nyingine za kisheria na haiwezaki kuzisuluhisha asubuhi na mapema.
Chalamila amesema duka si sawa na hospitali kwani hospitali zingegoma ingekuwa hatari zaidi na kuomba busara itumike. Mwisho amemaliza na mkwara mzito kwa yeyote atakaempiga mkwara aliyekubali kufungua.
"Aliyekubali kufungua afungue na yule ambae atamletea mkwara mtu yeyote yule aliyekubali kufungua naapa mbele ya Mwenyezi Mungu, hapo ndipo nitakapoonesha shoo nzima. Wewe unakuja unamletea mkwara, mimi nitakuchimba mkwara na hautaamka tena, na hili naomba niwaeleze ndugu zangu wa Kariakoo, utoto ukizidi hatuwezi kufikia hapo"
Pia Chalamila amewashukuru waliofungua maduka na kuwaahidi waliofunga atazilinda biashara zao na hakuna mwizi atakaeiba hata kama itakuwa mwezi. Chalamila amesema biashara sio siasa na leo jioni wataona hasara yake lakini siasa haiwezekani kugundua hasara zake.
Chalamila pia amedai yeye kama mkuu wa mkuu wa mkoa akiumua kwenda kukaa madukani kwao aangalie kiwango kikubwa cha ukwepaji kodi, amehoji kama wataweza kuishi Kariakoo!
Pia, soma=> RC Chalamila: Wafanyabiashara wa Kariakoo wajitafakari, migomo siyo suluhisho
View attachment 3024612
Samiah anakuchekea wewe labda. Kwangu namuona Kama incapable leader.Gharama za Bandari
Ndio maana nasema Samia anawachekea si unaona unavyoongea upumbavu hapa harafu uchumi uko paralysede.
Siasa za kindezi kama hizi piga ndani hao wapuuzi wakimbie Nchi.
...Hao watafutwe wanaochochea mgomo. Kisha washtakiwe Kwa kuhujum
Kasome sheria ya leseni ya biashara, kwanza katika adhabu hakuna kufungiwa biashara Bali fine au kufunguliwa kesi mahakamani. Muwe mnasoma kwanza kabla ya kuropoka.Kasoma masharti ya Leseni yako. Au wewe machinga?
Hizi kamati mara nyingi zinaundwa nyuma ya mikamera majibu ya uchunguzi wa hizo kamati nyuma ya paziaCcm hawana hoja ,kamati ya majaliwa ilienda wapi?
Huu ni msemo usio na maana. Kuna 1) sheria zinazokataza (ni marufuku...), 2) kuna sheria zinazolazimisha (kila mtu ata...), 3) kuna sheria zinazoruhusu (mtu yeyote aweza...). Sasa hiyo ya kutii sheria bila shuruti iko upande gani wakati sheria tayari zina element ya 'coercion' (yaani kufanya jambo lolote au kutofanya kwa jinsi sheria zinavyoelekeza)?Sawa. Fuata Sheria za Tanzania bila shuruti
Ndio , na Waziri kakubali kuwasililiza. Wewe Baki na ukatili wakoHao Viongozi wa mgomo bado wapo wanavinjari uraiani?
Uhujumu uchumi umefanyikaje?.Wakamatwe waburuzwe kizimbani Kwa uhujumu uchumi
Na ndio maana sio mkuu wa mkoa Wala mbunge. Nadhani umeelewa sababu.Aggrey Mwanri apewe ukuu wa mkoa wa Darisalamu, hao wafanyabiashara angewachota wote na kuwasukuma ndani
Anayekula rushwa Ina maana kajitoa mhanga. Wananyongwa mawaziri sembuse wewe. Nani anahujumu uchumi, kufunga duka au mgomo sio uhujumu uchumi. Hakuna kosa Kama Hilo.Kwani Toka wameanza kunyongwa Wala Rushwa waneisha? Acheni ujinga wa kuhujumu uchumi Kwa siasa nyepesi
Mama angewaza kiupana angeanza na kufukuza huyu..... Anaongea kama anaongea na masikini wanaojitafuta.... Tatizo Sana hili...Kwani hao wafanyabiashara wameanza kufanya biashara jana paka aanze kuwaeleza hasara na faida za biashara zao.
Hapa unamchukua mmoja una-deal nae binafsi, unampiga uhujumu!
Akili zitawakaa sawa!