Chalamila: Vibaka wafanywe 'skeleton' za maabara iwe fundisho kwa wengine

Nakazia maneno ya Mhe. Mkuu wa Mkoa. Nina jamaa mbaka leo yuko ICU kisa bisibisi wakitaka pesa alizotoa ATM muda mfupi (usiku). Tena akiwa kwenye gari, wakagonga na boda, jamaa kushuka ikawa issue kumbe walitaka pesa tu.
 
Endeleana wizi wako muda sio mrefu utaingia kwenye 18
 
Hayo yanatokea haimaanishi ndio nawe uue, ingekua hivi hata mtu anaweza kuwa hajaiba akazushiwa uhai ukapokwa. Sheria zingekua madhubuti wananchi wangewaamini polisi... kujichukulia sheria mkononi ni matokeo ya polisi kufeli
Sawa kabisa mkuuu ila sasa wakati tusubiri hao polisi wajenge iman kwetu nao vbaka wanatuteketeza .tufanyajee mkuu ?
 
Huu sasa ni ukiukaji wa haki za binadamu na si vema binadamu kufanyiwa sampling za tiba bila utashi wake. Unamuua kibaka halafu mwili wake unaupeleka maabara kwa ajili ya experiment maabara si vema
Badlika sasa vingenevyo chala keshasema utageuzwa skleton maramoja
 
Unataka ujue kama ni yeye?πŸ₯±
hapana mkuu,... mdogo wangu nae alikoswa koswa na hao washenzi, kwenye tukio kama hilo,....tulipewa taarifa kama hizo kutoka kwa mdogo wetu,...
 
Huyu kuchaa mbona wanaokula kwa urefu wa kamba ana waacha wana kula kiyoyozi kwenye ofisi za wananchi, vibaka nao wanakula kuligana na urefu wa kamba yao.
 
Hayo yanatokea haimaanishi ndio nawe uue, ingekua hivi hata mtu anaweza kuwa hajaiba akazushiwa uhai ukapokwa. Sheria zingekua madhubuti wananchi wangewaamini polisi... kujichukulia sheria mkononi ni matokeo ya polisi kufeli
Na sio polisi hata mahakamani napo ni shida
 
Yupo sahihi,hayo mambo yenu ya haki za binadamu yanatuchelewesha sana,hawa wapuuzi wanarudisha sana watu nyuma......kama hujawahi kufikiwa na hawa huwezi kunielewa na utaona nina roho mbaya,ila ni wapuuzi sana........
 
Huyu kuchaa mbona wanaokula kwa urefu wa kamba ana waacha wana kula kiyoyozi kwenye ofisi za wananchi, vibaka nao wanakula kuligana na urefu wa kamba yao.
Endelea na wizi wako ipo siku utaingia kwenye 18 za raia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…