Changamoto ya kununua magari ya mkononi

Gari mpya ikirudiwa rangi thamani itashuka..!
Gari mpya ikifunguliwa injini thamani itashuka..!
Kwa hiyo ikikwanguliwa na kugongwa unaacha hivyo hivyo ili isishuke thamani? na je kama unataka kubadilisha kitu kwenye engine unaacha ili thamani isishuke?
 
Kwa hiyo ikikwanguliwa na kugongwa unaacha hivyo hivyo ili isishuke thamani? na je kama unataka kubadilisha kitu kwenye engine unaacha ili thamani isishuke?
Sio uache kurekebisha.. Ila thamani ya Gari isiyogongwa>>> Iliyogongwa ikarudiwa rangi>>>iliyogongwa ikaachwa hivyo hivyo..!
Process ya kupaka rangi kiwandani 👇🏾
Kuna garage inarepair rangi kwa namna hiyo!!? Mwendo wa PUTI na msasa.. Wanaspray rangi..

Unopened engine >>>engine iliyofunguliwa ikarekebishwa..!
Fundi anafungua bolt 10..anarudishia 8..mbili anasema hazina kazi..!
Bolts zina specified torque zinapishana.. Fundi anakaza tuu bolt zote sawa..!
 
Mie sio mtaalam sana wa ufundi ila ninatumia tu akili kuwa gari yangu ikichunika chunika au rangi ikipaushwa na jua inapaswa kupigwa rangi ili iweze kurudi katika ubora wake.

Nimekaa Japan na nimeona hizi kampuni za used car zinapaka rangi magari kabla ya kuja huku na mengine yanarekebishwa engine. Nilinunua gari kule na walirekebisha vitu kwenye engine na kupiga rangi kabla hawajaisafirisha
 
Tunaongelea experience ya hapa nyumbani..
Sidhani kama kuna gari ya mkononi inaenda kurekebishiwa Japan..!

Ulipiga rangi gari nzima..!!? Ulilipia Yen ngapi..!!?
 
Beforward wapo vizuri hawana janja janja!
 
Siwezi kununua gari la mkononi kutoka kwa stranger.

"Full AC"

"Full document"

"AC utaomba koti uvae"
 
Nyote mnaongea lugha moja. Japan wanafuata mtiririko uliooneshwa hapo juu wa kurudishia/kupiga rangi tofauti na huku kwetu. Na ndio maana mwonekano wa rangi za magari yanayotoka nje ni tofauti na kwetu hapa baada ya kuwa yamerudishiwa rangi
 
Nyote mnaongea lugha moja. Japan wanafuata mtiririko uliooneshwa hapo juu wa kurudishia/kupiga rangi tofauti na huku kwetu. Na ndio maana mwonekano wa rangi za magari yanayotoka nje ni tofauti na kwetu hapa baada ya kuwa yamerudishiwa rangi
Kweli kaka mwonekano hauwezi kuwa sawa kwa sababu ya teknolojia. Hata Airport yetu ujenzi wake sio level za mbele kwa sababu ya teknolojia na ukosefu wa mafundi bora. Ila hilo lisitufanye kuacha kupiga rangi magari yanapopata mushkeli. Kuna wachuina Bongo wanapiga rangi kama imetoka leo Japan
 
Yalinikuta illa Mungu akanisaidia. Tulihama nyumba yetu mbali na shule na hakuna school bus na wote mi na wife tuna kazi.
Nikanunua gari aina ya Ist kwa muhindi mjini, tena kupitia dalali namjua kwa 11m na ya kwake laki tano, namba Dwf.
Siku nane ikafa engine ilizima ghafla kuwapigia simu walikana wote.
Dereva namjua hana makosa kumbe ilikuwa engine kimeo ilishafunguliwa.
Nikaweka engine mswaki laki 9.
Na gharama zote ikaja kama 1.3m
Ndani ya mwezi wakati ipo safi nikapta mtu nikaiuza kwa 12M.
Sasa ninayo tokea japan imenicost 13.6M
Ipo safi na inasaidia watoto na nyumbani.
Madalali sio watu hata ukimjua pesa kwao ndio Baba na Mama hata laki 2 anakupiga hajali ya baadaye.
Gari za mkononi hapana labda hizi kubwa kupitia makampuni au matajiri wanabadilisha gari tena labda.
 
Pole..
Uzuri wa gari hizi za mkononi ni bei yake..
Inapendeza tungekuwa na utaratibu wa kuweka service history ya gari.. Kabla ya kununua unaomba upewe uone maintenance ya previous owner ilikuwaje..!
 
Changamoto sana, Toyota fielder ilikufa hivi hivj naona, saev hii Nissan Bluebird QR 20 ingawa ni plate no. D ila natamani nipate mtu achukue hata kwa 3m,
mawazo kila siku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…