#COVID19 Chanjo ni Lazima: Hoja ya Mbowe ina Mashiko

#COVID19 Chanjo ni Lazima: Hoja ya Mbowe ina Mashiko

Mkuu siasa unaiona wapi kwenye nukuu hii?

View attachment 1861894

Hata hivyo nisiache kukueleza hatimaye nimekuja kufahamu kuna upotoshaji mkubwa wa makusudi kwenye aliyosema Mbowe:


Nimelazimika kuondoka uzi huo sasa baada ya kumsikiliza msemaji mwenyewe.

Hakika tuna watu waovu sana baina yetu!
Mkuu siasa naiona itaingia pale ambapo chanjo itaanza kutolewa kiulazima, Mbowe kwa maneno yake mwenyewe amesema "chanjo haitakiwi kuwa hiari, huo sio utaratibu wa WHO"...huo ni upotoshaji, chanjo ni hiari, kinachotakiwa ni kutengenezwa mazingira ya kuwafanya raia wengi wawe tayari kupokea hiyo chanjo, tukianza kutafutana tupigwe sindano mwisho wa siku huko vijijini wahudumu wa afya wanaweza kuingia matatizoni kama kuuwawa kwa maana hoja potofu nyingi kuhusiana na hii chanjo zimeshaenea nchi nzima. Ni bora nguvu kubwa itumike kuelimisha jamii, kuishawishi jamii kuona manufaa ya chanjo ya corona...ni kama sera ya uzazi wa mpango, ni muhimu kwa mustakabali wataifa ...lakini kwa taratibu za kiafya haijafanywa kuwa ni lazima kila mtu aifuate, elimu ndio hutolewa zaidi vinginevyo wangekuwa wanawinda watu kuwadunga sindano, kufanya vasectomy ama kuwamezesha vidonge. Kwenye suala la chanjo ninasisitiza iwe ni hiari, tuna uwezekano mkubwa zaidi wa kufanikiwa kupitia njia hiyo kuliko kulazimishana.
 
Hahaha!

Mkuu, ni kweli haufahamu kabisa kwamba kuna mataifa ambayo yana sera ya mandatory vaccination inayofahamika duniani kote?

Ni kwamba haufahamu kabisa kuhusu sera ya afya ya chanjo ya lazima ama unafanya mzaha tu?
Mandatory vaccination ni nini?

Mbowe kasema Watanzania wote walazimishwe chanjo.

Ndiyo hiyo mandatory vaccination unayoongelea?

Nchi gani inalazimisha watu wote wachanjwe?

Unaelewa kwamba hizi chanjo mpaka sasa hazijapata final approval (mfqno chanjo za Marekani hazijqpqtq final approval kutoka CDC) na zinatolewa kwa ememergency approval tu?

Hao Wamarekani wenyewe ambao wametengeneza chanjo zao hawalazimishi watu wao chanjo. Sisi tunaopewa tu chanjo ndiyo tumewazidi ujanja kutaka watu wote wachanjwe?

Wewe unaelewa kwamba si kila mtu ana hali inayofaa kupewa chanjo? Kuna wengine wenye low immunityna ukiwapa chanjo ndiyo unaongeza risk yao kufa? Tanzania wako wangapi hawa? Ukilazimisha wachanjwe halafu wakafa kutokana na chanjo utakuwa umewasaidia?
 
Mimi ni mhanga mtarajiwa wa wazi wa upuuzi unaoendelea hapa. Naweza kugeuka mfu dakika yoyote kwa sababu ya watu hawa. Unaniuliza ya wamarekani? Give me a break!

Wewe ulipo si umeshanjwa?

Ulipo wewe Corona haikuhusu. Ama kweli hawakukosea waswahili waliosema mzigo wa mwenzio kwako ni kanda la sufu(Sufi). Tuko kati ya janga wewe unadhani we are enjoying ourselves?! Tunapambana wenyewe kwani hata kuna hata tulichowaomba?

Iko wapi shida kwenye speech ya Mbowe kwa nchi hii?

Acheni unafiki huku nyie mkiwa salama.

Hatuko wajinga kiasi hicho.

Wewe unayetaka chanjo wasiotaka chanjo wakikulazimisha usipate chanjo utafurahi?

Marekani huwezi kuiepuka wewe mtwana kibweka. Hapa ulipo unatumia mtandao wa Marekani.

Wewe dai chanjo nzuri uchanjwe.

Ukishachanjwa, mostly, hata ukiambukizwa Corona hutaumwa.

Na muachie asiyetaka chanjo hata baada ya kuelimishwa asichanjwe, akipata Corona, alazwe, afe. Kizazi kijacho kipunguze wajinga. Wewe unataka wajinga wazidi wenye maarifa?

Haya mambo mengine ni natural selection tu inapunguza wajinga. Ukitaka kupigana nayo utaleta janga kubwa kuliko Covid.

Mtu ambaye hajali afya yake kiasi cha kukataa chanjo potentially ni janga kubwa kwa dunia na anaweza kuzalisha tatizo kubwa kuliko Covid. Kama anataka kufa, mwache afe. Kwa nininm unataka kulazimisha aishi?

Zaidi ya ukweli kwamba serikali haijatoa chanjo kwa wanaotaka, tatizo liko wapi?

Mtu akikataa chanjo kwa ujinga wake, wakati wewe chanjo imekukinga, wewe kinachokuuma nini?
 
Kwani mna hoja? Kumbe ungali hujaona?


Huu upumbavu wa kuja na vi ID uchwara vipya vya msimu haulipi tena:

View attachment 1861891

Nendeni shule. Mnasumbuliwa na ujinga zaidi.

Rudini mkawaambie mada mkononi imewazidi kimo. Mlichokuwa mmepanga kimeparaganyika!

Habari ndiyo hiyo.
Nonsense!
 
Wewe unayetaka chanjo wasiotaka chanjo wakikulazimisha usipate chanjo utafurahi?

Wewe dai chanjo nzuri uchanjwe.
Hiyo Chanjo nzuri ni ipi?

Ni nani anayeamua kwamba chanjo hii ni nzuri au mbaya?

Wewe ama wanasayansi wa ulaya?
 
Mkuu siasa naiona itaingia pale ambapo chanjo itaanza kutolewa kiulazima, Mbowe kwa maneno yake mwenyewe amesema "chanjo haitakiwi kuwa hiari, huo sio utaratibu wa WHO"...huo ni upotoshaji, chanjo ni hiari, kinachotakiwa ni kutengenezwa mazingira ya kuwafanya raia wengi wawe tayari kupokea hiyo chanjo, tukianza kutafutana tupigwe sindano mwisho wa siku huko vijijini wahudumu wa afya wanaweza kuingia matatizoni kama kuuwawa kwa maana hoja potofu nyingi kuhusiana na hii chanjo zimeshaenea nchi nzima. Ni bora nguvu kubwa itumike kuelimisha jamii, kuishawishi jamii kuona manufaa ya chanjo ya corona...ni kama sera ya uzazi wa mpango, ni muhimu kwa mustakabali wataifa ...lakini kwa taratibu za kiafya haijafanywa kuwa ni lazima kila mtu aifuate, elimu ndio hutolewa zaidi vinginevyo wangekuwa wanawinda watu kuwadunga sindano, kufanya vasectomy ama kuwamezesha vidonge. Kwenye suala la chanjo ninasisitiza iwe ni hiari, tuna uwezekano mkubwa zaidi wa kufanikiwa kupitia njia hiyo kuliko kulazimishana.

Haya nayatoa comment #80 kwenye uzi huu huu:

IMG_20210721_131455_708.jpg


Ni vyema kumsikiliza mheshimiwa Mbowe mwenyewe badala ya kuwasubiri wengine kukulisha matango mwitu:


NB: Heri ule matango pori kuliko matango mwitu.
 
Wanaotaka kuchanjwa wachanjwe....hata hivyo hakuna nguvu ya kuchanja Watu milioni 60.
 
Hivi hii nchi mbona watu hawajitambui? eti chanjo ni lazima! kachanje wewe siyo uwaamulie watu afya zao. Eti mbowe kasema yeye ni daktari? anajua nini kuhusu huo ugonjwa? harafu nyie mlikuwa wapi awamu ya 5? maana awamu hii mna kihere2 kweli! lazima muwe na mipaka ya kusema, serikali iwadhibiti maana mmekuwa wajinga kupitiliza sasa!

IMG_20210721_131455_708.jpg
 
Mandatory vaccination ni nini?

Mbowe kasema Watanzania wote walazimishwe chanjo.

Ndiyo hiyo mandatory vaccination unayoongelea?

Nchi gani inalazimisha watu wote wachanjwe?

Unaelewa kwamba hizi chanjo mpaka sasa hazijapata final approval (mfqno chanjo za Marekani hazijqpqtq final approval kutoka CDC) na zinatolewa kwa ememergency approval tu?

Hao Wamarekani wenyewe ambao wametengeneza chanjo zao hawalazimishi watu wao chanjo. Sisi tunaopewa tu chanjo ndiyo tumewazidi ujanja kutaka watu wote wachanjwe?

Wewe unaelewa kwamba si kila mtu ana hali inayofaa kupewa chanjo? Kuna wengine wenye low immunityna ukiwapa chanjo ndiyo unaongeza risk yao kufa? Tanzania wako wangapi hawa? Ukilazimisha wachanjwe halafu wakafa kutokana na chanjo utakuwa umewasaidia?
Utoaji wa lazima wa chanjo ndio huo unaoitwa mandatory vaccination au pia compulsory vaccination. Ni utaratibu ambao umekuwepo miaka mingi.

Ukisema kuwa ni uongo, utaonekana kuwa wewe ndio muongo sababu hiyo sera inafahamika duniani kote. Ndio maana nikakuuliza kwamba hujui ama unaleta utani tu?

Kama ni suala la utani tu halina shida!

Hata huyo Mbowe kwenye hiyo video uliyoileta hapa amezungumza kuhusu hiyo sera. Kuna sehemu ameitaja kabisa "mandatory". Umefanya jambo zuri sana kuileta hiyo video.

Ukimsikiliza, anasema kuwa nchi za wenzetu chanjo ni lazima, ila wameanzia kutoa kwanza kwa wahudumu wa afya walio mstari wa mbele wa mapambano, wakifuatiwa na makundi maalumu, taasisi na kuendelea.

Hicho ndicho kinachoendelea kwa nchi kama Ufaransa, Uingereza, Italia, Ugiriki, Urusi na hata Marekani hivi sasa.

Marekani hivi sasa kuna vaccine mandates katika ngazi za taasisi na kampuni. Nafikiri, jana tumejadili hili na nikasema kuhusu hilo suala la "final approval" ya chanjo. Nikakuambia kwamba, tusubiri chanjo zipate full approval kutoka FDA. Isitoshe, siku si nyingi hilo litakamilika jambo litakalochochea kuongezeka kwa chanjo za lazima (vaccine mandates).

Suala la chanjo kuwa lazima nchi nzima kwa utaratibu unaofaa linaanzia kwa makundi ambayo yametajwa na Mbowe katika hiyo video. Isitoshe chanjo kuwa lazima haimaanishi kwamba serikali itatumia nguvu ya dola kulazimisha watu watoke kwenye nyumba zao kwenda kuchanjwa. La hasha!

Serikali inatunga sera ya kuhakikisha kwamba:

1) Chanjo zinapatikana kwa urahisi mahali pote nchini.

2) Kunakuwepo na vikwazo laini kwa wale wasiochanjwa kama vile kutoruhusiwa kuingia katika maeneo fulani yenye mikusanyiko ama kufanya kazi katika taasisi mbalimbali n.k.

3) Anayegoma kuchanjwa halazimishwi kwa nguvu ila tu atahitaji kufanya hivyo kama atataka kupata ajira mahali fulani ama kupata huduma fulani ya kiserikali.

Hiyo ndiyo maana ya mandatory vaccination na hii inafanyika katika hali ya dharura ambayo ni moral justifiable kama nilivyosema. Isitoshe, kabla zoezi la chanjo kufikia nchi nzima (population-wide), lazima lianzie kwa makundi fulani yaliyo hatarini zaidi kama alivyosema Mbowe.

Naweza nisikubaliane naye katika masuala kadhaa ila kuhusu hilo suala la chanjo za lazima ni suala halisi na linafanyika kwa utaratibu maalumu unaokubalika kimataifa.

Nimalizie kwa kusema kuwa, ninakushukuru tena kwa hiyo video uliyoileta. Nafikiri imesaidia pakubwa sana kutujibia maswali kadhaa kuhusiana na mjadala huu ambao tumeujadili hapa kwa muda sasa.
 
Hivi mfano chanjo ikawa inaleta complications za kiafya kwa raia , ni nani atawajibika na maisha yao na afya (assume hizo complications ni irreversible)?!

Huwezi lazimisha mtu kuweka makitu kwenye mwili wake na hajui yataleta shida gani.

Mkiendelea kulazimisha hivi siku mtalazimisha watu kushare personal info zao au kuwalazimisha wale vyakula wasivyotumia.....
 
Utoaji wa lazima wa chanjo ndio huo unaoitwa mandatory vaccination au pia compulsory vaccination. Ni utaratibu ambao umekuwepo miaka mingi.

Ukisema kuwa ni uongo, utaonekana kuwa wewe ndio muongo sababu hiyo sera inafahamika duniani kote. Ndio maana nikakuuliza kwamba hujui ama unaleta utani tu?

Kama ni suala la utani tu halina shida!

Hata huyo Mbowe kwenye hiyo video uliyoileta hapa amezungumza kuhusu hiyo sera. Kuna sehemu ameitaja kabisa "mandatory". Umefanya jambo zuri sana kuileta hiyo video.

Ukimsikiliza, anasema kuwa nchi za wenzetu chanjo ni lazima, ila wameanzia kutoa kwanza kwa wahudumu wa afya walio mstari wa mbele wa mapambano, wakifuatiwa na makundi maalumu, taasisi na kuendelea.

Hicho ndicho kinachoendelea kwa nchi kama Ufaransa, Uingereza, Italia, Ugiriki, Urusi na hata Marekani hivi sasa.

Marekani hivi sasa kuna vaccine mandates katika ngazi za taasisi na kampuni. Nafikiri, jana tumejadili hili na nikasema kuhusu hilo suala la "final approval" ya chanjo. Nikakuambia kwamba, tusubiri chanjo zipate full approval kutoka FDA. Isitoshe, siku si nyingi hilo litakamilika jambo litakalochochea kuongezeka kwa chanjo za lazima (vaccine mandates).

Suala la chanjo kuwa lazima nchi nzima kwa utaratibu unaofaa linaanzia kwa makundi ambayo yametajwa na Mbowe katika hiyo video. Isitoshe chanjo kuwa lazima haimaanishi kwamba serikali itatumia nguvu ya dola kulazimisha watu watoke kwenye nyumba zao kwenda kuchanjwa. La hasha!

Serikali inatunga sera ya kuhakikisha kwamba:

1) Chanjo zinapatikana kwa urahisi mahali pote nchini.

2) Kunakuwepo na vikwazo laini kwa wale wasiochanjwa kama vile kutoruhusiwa kuingia katika maeneo fulani yenye mikusanyiko ama kufanya kazi katika taasisi mbalimbali n.k.

3) Anayegoma kuchanjwa halazimishwi kwa nguvu ila tu atahitaji kufanya hivyo kama atataka kupata ajira mahali fulani ama kupata huduma fulani ya kiserikali.

Hiyo ndiyo maana ya mandatory vaccination na hii inafanyika katika hali ya dharura ambayo ni moral justifiable kama nilivyosema. Isitoshe, kabla zoezi la chanjo kufikia nchi nzima (population-wide), lazima lianzie kwa makundi fulani yaliyo hatarini zaidi kama alivyosema Mbowe.

Naweza nisikubaliane naye katika masuala kadhaa ila kuhusu hilo suala la chanjo za lazima ni suala halisi na linafanyika kwa utaratibu maalumu unaokubalika kimataifa.

Nimalizie kwa kusema kuwa, ninakushukuru tena kwa hiyo video uliyoileta. Nafikiri imesaidia pakubwa sana kutujibia maswali kadhaa kuhusiana na mjadala huu ambao tumeujadili hapa kwa muda sasa.
Umeitaja Marekani.

Marekani imelazimisha wananchi wote wachanjwe?
 
Hivi mfano chanjo ikawa inaleta complications za kiafya kwa raia , ni nani atawajibika na maisha yao na afya (assume hizo complications ni irreversible)?!

Huwezi lazimisha mtu kuweka makitu kwenye mwili wake na hajui yataleta shida gani.

Mkiendelea kulazimisha hivi siku mtalazimisha watu kushare personal info zao au kuwalazimisha wale vyakula wasivyotumia.....
Maadili ya kitabibu yenyewe yanakataza kulazimisha chanjo.

Ndiyo maana chanjo ina consent.

Hivyo, mtu anayetaka kulazimisha chanjo anajionesha hajui hata maadili ya kitabibu.
 
Umeitaja Marekani.

Marekani imelazimisha wananchi wote wachanjwe?
Mkuu, umesoma lakini kile nilichoandika?

Nimeeleza kuhusu hiyo sera anayoisema Mbowe ya mandatory vaccination pamoja na vaccine mandates. Sera hiyo pia inatumika nchini Marekani.
 
Mbowe karopoka kwamba Watanzania walazimishwe chanjo.

Hajatoa nuanced position.
Kuropoka ama kutokuropoka si hoja hapa.

Yeye amesema kuwa, uwekwe utaratibu wa chanjo kuwa lazima kwa watu wote.

Lakini, hajaishia hapo tu, pia amesema kuwa utaratibu wa chanjo hizo kama ulivyo kwa nchi zingine, unaanzia kwa makundi yaliyo katika hatari zaidi katika nchi, na ameyataja.

Nuanced position gani hajatoa?
 
Kuropoka ama kutokuropoka si hoja hapa.

Yeye amesema kuwa, uwekwe utaratibu wa chanjo kuwa lazima kwa watu wote.

Lakini, hajaishia hapo tu, pia amesema kuwa utaratibu wa chanjo hizo kama ulivyo kwa nchi zingine, unaanzia kwa makundi yaliyo katika hatari zaidi katika nchi, na ameyataja.

Nuanced position gani hajatoa?
Marekani uliyoitaja haina utaratibu wa chanjo kuwa ya lazima kwa watu wote.

Mimi naishi Marekani. Mtaani kwangu kuna nurse. Kazini kwake wanamlazimisha kuchanja. Yeye hataki.

Anafikiria kuacha kazi na kutafuta kazi sehemu nyingine ambayo halazimishwi kuchanja.

Hakuna mpango wowote state yoyote ya Marekani kulazimisha watu kuchanja.

Watu wanaelimishwa umuhimu wa kuchanja na wanahimizwa kuchanja.

Mbowe na wewe ama mna uelewa mdogo wa habari nzima ya "mandatory vaccination", ama mnataka udikteta.

Mnalinganisha limited mandates kama kwa wafanyakazi wa sekta ya afya na mandate ya chanjo kwa watu wote.

Kuna watu hawakubali chanjo kwa sababu za kidini. Kuna watu hawakubali hata kuwekewa damu kwa sababu za kidini.

Hizi ni haki zao za kidini. Mimi sina dini, lakini natetea haki zao za kidini.

Hawa nao mtawalazimisha wachanje?

Ikitokea variant ya Covid ambayo tiba/ chanjo yake pekee ni nyama ya nguruwe, mtawalazimisha Waislamu wasiotaka kula nguruwe wale nguruwe kwa sababu inatibu Covid?
 
Back
Top Bottom