Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 12,699
- 22,598
- Thread starter
-
- #41
I say watu mna mawazo mafupi sana. Hebu niambie, Raisi akisema kuna ugonjwa wa kipindupindu umezuka marufuku mtu yeyote kutengeneza pombe za kienyezi na kuziuza vilabuni, kwako wewe huo ni udikteta?Kumbe udikteta tunaupenda!
Nitawasikilizaje wakati watu wote waliochanja wameshakufa? Si ndio umeambiwa hivyo?Huyu jamaa aliyeanzisha huu uzi kama siyo mchawi basi ni freemason. Utalazimishaje mtu kufanya unachoamini wewe?. Wasilikizie waliochanja!
kwa hiyo kufanya invasive procedures kwenye mwili wa binadamu unafananisha na quarantine? Hivi itoke decree leo kua mashoga wote wafanyiwe chemical castration ,utaunga mkono?I say watu mna mawazo mafupi sana. Hebu niambie, Raisi akisema kuna ugonjwa wa kipindupindu umezuka marufuku mtu yeyote kutengeneza pombe za kienyezi na kuziuza vilabuni, kwako wewe huo ni udikteta?
Kwa hiyo unalinganisha kuchanjwa Corona na chemical castration?kwa hiyo kufanya invasive procedures kwenye mwili wa binadamu unafananisha na quarantine? Hivi itoke decree leo kua mashoga wote wafanyiwe chemical castration ,utaunga mkono?
Siku njemaKwa hiyo unalinganisha kuchanjwa Corona na chemical castration?
Kama chanjo ya Corona ni chemical castration, nikisha chanja nipe my wife wako anikalie sawa, maana hutakuwa na la kuogopa
Sawa, acha mungu wenu awavushe salama kama alivyomvusha raisi wetu Magufuli. Anza kuimba kabisa mtakutana na Magufuli mtoni.Ndio tulichanjwa. Lakini chanjo unayopigia debe ni tofauti sana. Hivi hujiulizi juu hii chanjo ambayo hata waliowahi pokea Nobel Prize za sayansi wanatuhadharisha sisi hinadamu dhidi yake?.
Ugonjwa wa kuambukiza dunia yote kwa mpigo haijawahi tokea. Sisi na Mungu Mungu wetu atatuvusha salama. Endelea na kampeni zako una faida unaipata.
Hahahaha! Mkuu umetisha. Waswahili bwana wako tayari kumwamini mganga wa kienyeji kunyweshwa mavi ya kuku yamechanganywa na mkojo wa mbuzi ili wapate utajiri kuliko kupewa chanjo ya Corona ili wasije wakafa!Wakuuwe kwa nini? Hivi kwa nini watu mafukara huwa wanaishi kwa wasiwasi kuwa watu wengine wanawaonea wivu? Hata ukienda kwa waganga wa kienyeji wengi wa wateja ni mafukara wanaodhani wamelogwa ili wasipate maendeleo.
Watu wa aina hii unapoteza muda tu kulumbana nao. Ni uwezo wao wa kupambanua mambo ndiyo tatizo. Haya mambo hayahitaji akili kubwa sana lakini inasikitisha kuna watu hawaelewi. Mtu vitu anavyotumia katika maisha yake karibu asilimia 80 vimetengenezwa na wazungu halafu anachagua kimoja anasema wanataka kutuua na hiki. Hivi wanajua kuwa kama wazungu wakiamua kutuua tufe kama inzi watapoteza nguvu ku-create njia complicated namna hiyo? Hizi simu tunazotumia wakiweka mawimbi yenye madhara kuna ''kima'' atagundua?Sawa, ndio maana wakaleta Corona inayowaua na wao wenyewe ili kutukomoa Waafrika na watuuzie chanjo za Corona.
Hivi huko vichwani wengine mmejaza nini hasa?
Sawa. Lakini, yule aliyepata chanjo kwa nini asijitenge na ambao hawajachanjwa. Ukiona konda hajachanjwa usipande gari lake. Konda akikosa abiria ataitafuta chanjo mwenyewe.Chanjo ya Korona inaweza kuwa hiari, lakini usiseme hutaki chanjo halafu uendelee kuwa konda wa basi au nesi hospitali, tafuta kazi nyingine.
Wanatoboa mtumbwi...!!!Mkuu me nahisi kuna watu wanalipwa kwa kazi ya kuhamasisha huu upuuzi walio uita chanjo.
Haiwezekani me na familia yangu tukatae kudungwa chanjo, alafu anatokea kenge analazimisha tuchanjwe kisa yeye na familia yake wamechanjwa.
Mkuu, katika vitu kama hivi, ambavyo vinaingia kwenye mambo tunayoita public administration, kuna kitu kinaitwa cost of enforcement of directives.Sawa. Lakini, yule aliyepata chanjo kwa nini asijitenge na ambao hawajachanjwa. Ukiona konda hajachanjwa usipande gari lake. Konda akikosa abiria ataitafuta chanjo mwenyewe.
Na yule mgonjwa ambaye anaona daktari hajachajwa, basi mgonjwa huyo atafute chanjo mwenyewe ili awe huru kwenda kwa daktari ambaye hajachanjwa ama amtafute daktari aliyechanjwa. Pia katika hili Daktari mwenyewe akiona wagonjwa wanapungua kwake, na ile fomu ya kupima utendaji wake (OPRAS) ikionekana hayuko "effective" atapangiwa kazi nyingine. Rahisi tu.
Shida iko wapi katika hili, kwani ? Kwa nini mnataka makonda walazimishwe kuchanjwa? Kwa nini mnalazimisha matabibu kuchanjwa? Wakati huo huo hamtaki kushikwa makosa endapo chanjo hizo zitawaletea madhara hao makonda na matabibu? Mjifunge kisheria kuwa endapo konda ama daktari atapata madhara kutokana na madhara ya chanjo kiasi cha kutoweza kuendelea na kazi yake basi, mtakuwa tayari (ninyi ambao mnataka chanjo iwe lazima kwao) kuitunza familia nzima ya konda ama tabibu kwa zaidi ya miaka hamsini. Ni wajibu mdogo sana huu kuutekeleza ninyi mulio mstari wa mbele kuhusu ulazima wa chanjo. Rahisi tu namna hiyo, Mkuu.
Haya sasa shusha nondo zako, tukuelewe Mkuu.
Karibu.
Hao watu ni mazimwi? Kiasi wana weza kukabili mziki wa covid SA, covidUK, covidIndia, covidDelta, sijui kovid alfa...bila kutingishika!? Vipi kuhusu malarai, si kuna tiba, mbona bado hali tete...! Vipi kuhusu mafua, na ule ugonjwa wa upungufu wa kinga za mwili, si bado hali ni tete...ni 'cha umaalumu' kuhusu kovid hapa nchini ambao hatukuweka lock down na walioweka lockdown na kuchanjwa? umaalumu upo ukivua miwani ya upendeleo kutokana mambo yasiyowekwa wazi.....watu ambao wanavi-host. Sasa kadiri ambavyo watu hao wanaendelea kuwapo, na virusi vinaendelea kuwatumia kujibadilisha, hata nyie mliochanja itafikia mahali vile virusi wanavyosambaza vimebadilika na chanjo mliyofanya haiwazuii tena.
Kila mtu afanye maamuzi kwa faida zake mwenyewe. Kama Ni huduma za kijamii kila mtanzania anawajibika kuzitoa directly au indirectly.Chanjo ya Korona inaweza kuwa hiari, lakini usiseme hutaki chanjo halafu uendelee kuwa konda wa basi au nesi hospitali, tafuta kazi nyingine.
Katika hali ya haki za binadamu, kila mtu ana uhuru wa kufanya analotaka ili mradi asivunje sheria au kuingilia au kuathiri haki za watu wengine katika kuwa kwao huru na kutofanyiwa bugudha za kimaisha.
Sasa wapo wanaotaka kwamba suala la chanjo za Korona liwe la utashi wa mtu, watu kama kina Aunt Fatuma Karume. Na wapo wanaotaka chanjo za Korona liwe lazima, watu kama kina Mbowe. Wote hawa wapo sawa, lakini kuwa kwao sawa kuna mipaka.
Nikianza na kina Fatma Karume, ni sawa watu kuwa huru kuamua kuchanja au kutochanja dhidi ya Korona. Lakini sasa, wewe unapoamua hutaki kuchanja basi msimamo wako usiathiri au kuhatarisha maisha ya wengine.
Kama utakataa kuchanja na ukaamua kujifungia nyumbani kwako hilo ni hiari yako. Lakini usikatae kuchanja halafu uje unipumulie virusi vya korona sugu mimi ambaye nimekubali kuchanja, au hata watoto ambao wako chini ya umri wa kuchanja, au watu ambao wameambiwa wasichanje kwa sasa kwa sababu mbalimbali kama ujauzito.
Na kwa kina Mbowe, kinyume cha hili la kina Fatma kinatumika kwako. Ikiwa sitaki kuchanja na hata niko tayari kuacha kazi yangu ambayo inaweza kuhatarisha maisha ya wengine kwa sababu sijachanja, basi usiniingilie, niache nijifungie nyumbani kwangu, kwa kuwa sina haja ya kujichanganya na watu wengine.
Tukielewana katika haya basi tutakuwa sawa.
Soma hapo juu utapata jibu la issue yako unayoeleza hapa. Labda kwa kukusaidia;Kila mtu afanye maamuzi kwa faida zake mwenyewe. Kama Ni huduma za kijamii kila mtanzania anawajibika kuzitoa directly au indirectly.
Watu mnachanja halafu bado mnaogopa kuambukizwa, Basi hiyo si chanjo.
Eti mi nisiwe nimechanjwa halafu mtu akanipumulia virusi, Kwani Kama umechanjwa na chanjo inafanyakazi kweli virusi vitakufanya Nini.
Kila mtu alindwe au aangamie kwa kill anachokiamini. Kama unaamini chanjo itakulinda Basi uwe tayari kwa matokeo yake, na Kama huamini kulindwa na chanjo Basi ulindwe na kile unachokiamini.
Hatuna imani na wanasayansi katika corona, wao wenyewe wamechemsha, Kama sivyo ama corona ingekuwa imepotezwa, au ingebaki tu kwa nchi zenye uwezo na weledi mdogo wa kisayansi na kitechnolojia.Si katika kila jambo tunapaswa kuishi kwa imani. Mengine yanahitaji ukweli wa kisayansi.
Narudia Tena, 'hatuna imani na wanasayansi katika maswala ya corona' . Umeelewa mkuu?KY unayojivunia katika kulainisha njia yako inatengenezwa na hao hao watengeneza chanjo
Sasa mambo ya imani katika mambo ya kisayansi bwana, subiri kina Charles Darwin wakifufuka ukaongee nao. Maana mie siamini huko nyuma tulikuiwa sokwe, na kama unaamini tulikuwa sokwe nikisema sokwe wewe au ukoo wenu mnafanana na sokwe usikasirike.Hatuna imani na wanasayansi katika corona, wao wenyewe wamechemsha, Kama sivyo ama corona ingekuwa imepotezwa, au ingebaki tu kwa nchi zenye uwezo na weledi mdogo wa kisayansi na kitechnolojia.