Chato yazidi kuneemeka; Serikali kujenga Hospitali ya Rufaa ya kanda ya Ziwa

Chato yazidi kuneemeka; Serikali kujenga Hospitali ya Rufaa ya kanda ya Ziwa

Naona umechachamaa hatari kujibu ..
Hakuna alopinga huduma za jamii kuwepo kila nyanda.. Hoja hapa ni Hivi kweli ni Chato tuu? Hapa hakuhitaji hata akili ya darasani kuelewa kuna upendeleo kwa chato(tusitaje yalowekwa chato ) ambako sehem nyingine penye uhitaji zaidi hapakupewa kipaumbelele

Huduma ya jamii inatakiwa iwe sehem yenye kuhitajika sana na kufikaka kwa urahisi yaan umbali na miundo mbinu bora jee kwa kanda ya Ziwa nzima hapo chato ndo katikati et? Au tutete tuu ilimradi ugali uwepo mezani siku ziende...
Kwanza ni kutoe hofu, mimi sifungamani na vyama vya kisiasa wala kidini.

Pili, Wakati vitu vinarundikwa Daslam hamkujua kuna wahitaji? Je ulikuwa ni upendeleo?

Chato ipo katikati ya Wilaya takribani sita. Ndio maana nimesema Musoma na viunga vyake, Kahama, Shinyanga na Simuyu wafike Mwanza.

Ujiji, Kigoma, Bukoba, Biharamulo, Geita wafike Chato. Maana walifika Daslam kwa takribani miaka 60.
 
Kama mzaha kwenye Soap Opera walianza na Traffic Light pasipo na gari, mara paa mwanafunzi wa kwanza kitaifa hii ndani ya episode ya pili..
 
Ile ya Bugando imeshindwa kuwahudumia au? Au hayo yanafanyika hili hiyo huduma iwe karibu na nyumbani. Kama ni kufa mtu atakufa tu hata kama anahishi hospitalini.
 
Tumwulize Umi Tanga hamna watu wa kustahili hospitali ya rufaa ya kanda. Umbali wa Chato hadi Bugando na umbali wa Tanga hadi KCMC ama Mhimbili upi mkubwa? Kanda ya kusini je wana hospitali ya rufaa?
 
... kwa hiyo kuyarundika Chato ndio itakuwa tiba? Kama unadhani kurundika Dar sio tiba kwanini udhani kufanya hivyo Chato ndio itakuwa tiba?
Kuna vitu ni vyepesi sana kuvichanganua na moja ni Chato kuzungukwa kila pande yaani lazima tu watu wa maeneo hayo wakanyage pale. Ilhali mtu Kigoma anavuka takribani mikoa mitano hadi Daslam, Haiwezekani!
 
Watu walipoanza kujenga Ma Hotel Makubwa makubwa Chatto tukawaona hamnazo kumbe wameshajipanga vya kutosha

Kila la Kheir wana Chato

Ila maendeleo yanatabia moja mbaya sana

Wageni na Wazawa hufukuzwa na maendeleo hayo hayo

Wazaramo wamebaki wa kutafuta K.koo

Mtwara mjini Wamakonde wameanza kuwa wapangaji kwenye nyumba za Wahaya na Wapemba

Dodoma mjini ukimuona Mgogo basi kuwa kaja kama sio kuuza ubuyu basi zabibu
Dodoma hii hii nayoijua ama kuna nyingine boss?
 
Hakuna cha ubaba! Taifa umaskini chanzo ni yeye. Magufuli ndiyo ananyoosha hii sasa.
Wewe huijui Tanzania na wala haumjui Nyerere hata chembe, anayofanya Mh. Magufuli sasa hajafikia na hatafikia robo ya mambo ya maendeleo aliyofanya Nyerere.

Ushabiki usivuke mipaka ukawafanya watu wavimbe vichwa.
Sasa toka humu JF nenda kaanze kuhesabu barabara, madaraja, reli, ndege, shule, vyuo, hospital, viwanda, mabwawa ya kuzalisha umeme, na huduma zilizokuwa zinatolewa na serikali wakati wa Nyerere kwenye hivyo vitu nilivyo kutajia.

Huyu muheshimiwa Magufuli alikuwa anakunywa chai ya maziwa na mkate shuleni na vyuoni, hakukuwa na mkopo elimu ya juu, wote ilikuwa bure. Huenda hata enzi zake alipata madaftari shuleni huko primary school.

Watu walilipiwa na serikali usafiri wa kutoka kijijini huko inakojengwa hospital kwenda chuo, wanachuo walipanda hadi ndege kwenda UDSM.

Wewe nahisi ni kijana wa majuzi, mwache Nyerere aitwe baba wa Taifa. Kuna watu kibao kawapeleka nje kusoma elimu ya juu fani mbali mbali.
Huyu wa sasa unataka kumkuza kuliko Nyerere tuambie wangapi amepeleka nje tofauti na wale, nasema wale nikiamini unawajua.

Ukweli Mh. Magufuli ni rahisi ninae mkubali na kumtetea sana popote pale, ni wa mfano baada ya Nyerere anafuata yeye kwa mtazamo wangu hadi sasa.
Sijui hapo baadae ataendeleza ubora au ataharibu! Hilo swali muda utatupatia majibu sahihi. Hatuwezi kuagua na kupiga ramli kama waganga.
 
Kuna vitu ni vyepesi sana kuvichanganua na moja ni Chato kuzungukwa kila pande yaani lazima tu watu wa maeneo hayo wakanyage pale. Ilhali mtu Kigoma anavuka takribani mikoa mitano hadi Daslam, Haiwezekani!
... tuanzie na mkoa wenyewe wa Geita; hivi kwa akili ya kawaida sana katikati ni wapi? Naona Chato iko CENTRAL kwelikweli!
Chato.png
 
Wewe huijui Tanzania na wala haumjui Nyerere hata chembe, anayofanya Mh. Magufuli sasa hajafikia na hatafikia robo ya mambo ya maendeleo aliyofanya Nyerere.

Ushabiki usivuke mipaka ukawafanya watu wavimbe vichwa.
Sasa toka humu JF nenda kaanze kuhesabu barabara, madaraja, reli, ndege, shule, vyuo, hospital, viwanda, mabwawa ya kuzalisha umeme, na huduma zilizokuwa zinatolewa na serikali wakati wa Nyerere kwenye hivyo vitu nilivyo kutajia.

Huyu muheshimiwa Magufuli alikuwa anakunywa chai ya maziwa na mkate shuleni na vyuoni, hakukuwa na mkopo elimu ya juu, wote ilikuwa bure. Huenda hata enzi zake alipata madaftari shuleni huko primary school.

Watu walilipiwa na serikali usafiri wa kutoka kijijini huko inakojengwa hospital kwenda chuo, wanachuo walipanda hadi ndege kwenda UDSM.

Wewe nahisi ni kijana wa majuzi, mwache Nyerere aitwe baba wa Taifa. Kuna watu kibao kawapeleka nje kusoma elimu ya juu fani mbali mbali.
Huyu wa sasa unataka kumkuza kuliko Nyerere tuambie wangapi amepeleka nje tofauti na wale, nasema wale nikiamini unawajua.

Ukweli Mh. Magufuli ni rahisi ninae mkubali na kumtetea sana popote pale, ni wa mfano baada ya Nyerere anafuata yeye kwa mtazamo wangu hadi sasa.
Sijui hapo baadae ataendeleza ubora au ataharibu! Hilo swali muda utatupatia majibu sahihi. Hatuwezi kuagua na kupiga ramli kama waganga.
Hayo yote unayotanabaisha hapa mbona ameyapokea baada ya kuwafukuza British? tokea hapo mbona hamna yaliyoongezeka?!.

Hivi vitu vya ubaba na umama ni siasa tu! Nina documents za Germany East Africa (Deutschland) na British Territory ambazo hata Jamhuri haina na haitokuwa nazo.

Narudia nina documents za Germany na British zenye ukweli wa yote ambazo hata Jamhuri haina.

Ukitaka kupiga maendeleo Tanzania hii kwanza ukatae ubaba na hivyo ndivyo Magufuli alipofanikisha na watu wanastaajabu.

"Kama walikuwa wanafanya, mbona hayaonekani?!." - John Pombe Magufuli
 
Serikali imesema ina dhamiria kujenga hospital ya kanda ya Ziwa huko Chato mkoani Geita

Waziri wa Afya jinsia na watoto amebainisha hilo leo

My take: kwa nini ijengwe Chato na si Mwanza kitovu cha kanda ya Ziwa au Geita makao makuu ya mkoa?

Source Mwananchi

Sent using Jamii Forums mobile app
Dada shikamoo siyo kwa point hii!
happy-tears-salute-emojipedia-mockup-top-requests-2019-picsay.jpeg
 
Back
Top Bottom