Chatu mkubwa katika pori jirani na 'Chuo Nyeti' Mbweni Malindi adhibitiwe upesi kabla hajaleta madhara

Ndiyo yuko nao Jirani.
 
Ila wavulana wa Dar mnachekesha. Unaogopa chatu kweli? Asante mama kwa bandari, vijana wako hawana ujasiri wa kukabiliana na chatu, hawataweza mikiki mikiki ya bandari hawa.
😂😂😂😂😂😂 muulize yeye alienda kufanya nini malindi kama sio umbea tu ameshindwa kutulia zake 365
 
Ndomana wakati mwingine tunaambiwa usiwaamshe wale waliyolala,unawaacha na ubish wao

Ova
 
halafu wanadamu huwa wanamchukulia chatu poa sana. vile vile unavyomwona, anachohitaji yeye ni kukurukia akukamate tu, akishafanikiwa, kujiviringisha mwilini mwako ni dakika sifuri, na ukishaona amejiviringisha, hata uige greda lije livute ajiviringue haliwezi, ana nguvu za ajabu kuvunja mbavu na kuhakikisha haupumui na muda mchache tu unapoteza maisha. wapo watu walioshuhudia wenzao wakifa mbele yao na hawana uwezo kumwokoa mtu ambaye tayari ashakamatwa na chatu, sio rahisi. zamani kijijini kwetu tulikuwa tunaambiwa ukimchoma na sindano au kitu chenye ncha kali anaweza kuachia, ila sasa ngozi yake ni nguvu ajabu, unaweza kukata na panga likadunda. nakumbuka hiyo ndio ngozi kijijini kwetu tulikuwa tunatengenezea ngoma, zinalia vizuri kweli. nashauri maliasili waende wakamwue haraka huyo au la wanakijiji wajitolee wakammalize tu.
 
Kijijini walikuwepo wenye uwezo wa kumeza mpaka ndama na tuliwaua sana, huyo GENTAMYCINE aka Popoma ilibidi apambane naye amuue sio kutupigia kelele hapa.
Chatu anatakiwa kuhamishwa, siyo kuuawa. Ukizingatia pale alipo inawezekane kwa ni ni ndiyo natural habitat yake, hajavamia isiookuwa watu ndiyo wamevamia natural habitat yake.
Hivyo alichokifanya GENTAMYCINE ni sahihi kutoa wito kwa mamlaka husika kuchukua hatua.
Uanaume ni kujua mahitaji ya kimsingi na kiasili ya viumbe wengine.
 
Kwakua ni eneo la mafunzo ni sahihi awepo hapo kwani ni sehemu ya watakavyo kumbana navyo maporini.
 
Unachoma kitu chenye ncha Kali chili tumboni ambako ni laini,siyo juu,juu hata shoka linadunda
 
Kwa hio kila siku mida hio chatu ndio anatoka mishe zake anarudi chimbo [emoji23][emoji23]
 
Chatu akiwa na njaa hupita mpaka dirishani. Chuo hicho wajiangalie. Kama huo msitu Una wanyama wengi wadogo basi Hakuna shida.

Muhimu maliasili wamhamishe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…