Aisee umenikumbusha zamani sana, tulivokuwa high school shule flani kongwe sana iliyopo karibu na msituni Minaki tulikuwaga na chatu wengi sana na nyoka wengi sana, aisee namshukuru mungu nilimaliza salama na sikuwahi kuumwa na nyoka, kipindi cha mvua walikuwa wanatoka msituni wanapanda huku juu madarasani kutafuta joto, kuna siku wakati rafiki yangu anatoa vitabu kwa ajili ya kuvipanga, vitabu alivokuwa amevieka chini kweny kona ya ukutani, bhana si kulikuwa kuna nyoka kajificha kweny gape kali ya vile vitabu na ukuta, aliruka ghafla baada ya kusikia vitabu vinahamishwa, mm nilikuwa nipo busy nasoma zangu, jamaa yangu akapiga kelele "Wazee nyoka" aisee mm ni jasiri wa vitu vingi lakini nyoka hapana, baada ya kusikia hio sauti ya mshkaji nilijikuta nipo nje ya darasa sijui nilifikaje, haraka nilianza kuokota mawe na kumrushia, wengine wakawa wanahangaika kule ndani hawaamini kilichotokea, kwa bahati nzuri kuna washkaji walikuwa nje ya darasa wakajumuika na mm kumrushia mawe yule nyoka, bahati nzuri akafa hakumdhuru mtu yeyote, alikuwa ni nyoka wa kijani, unene na urefu wa yule nyoka ulikuwa very significant kabisa.
kuna mambo nikifikiria nabaki tuu namshukuru mungu, siku zingine unapishana na nyoka, one day nilimkanyaga nyoka mweusi bahati nzuri kwa hofu yangu ya nyoka likizo nilivorudi home mzee wangu alininunulia mabuti kwaio hakuweza kunidhuru lakini huo mshtuko na hizo mbio zilizofuata baada ya hapo aisee adrenaline ni kitu chengine. Ilikuwa ni kawaida sana kipindi cha mvua kwa wiki wanafunzi wawili au watatu kupelekwa hospitali ya kisarawe cause of snake bites.
Siku nyingine tuliua chatu mkubwa, yule alikuwa anauwezo wa kumeza mtu mzima bila shida, hio siku siwez sahau, wanaume tulipambana hadi akafa mm kawaida yangu nikiwa mbali nikirusha mawe yangu fresh kabisa.
Nakumbuka mwalimu mkuu alitupa kila mmoja aliyehusika kumuua kreti la soda, nilikuwa nasubiria siku za wali ndo nashushia wali na soda na washkaji zangu(sio mpenzi wa soda tokea kitambo, nilikunywa moja tuu zingine niliwaachia).
Baada ya kumuua yule chatu nakumbuka kuna mlinzi akatuambia hamwez kuwamaliza chatu wanaishi kweny huu msitu, nilichoka aisee.
Hadi namaliza minaki tulifanikiwa kuua chatu wawili.
Ushauri wangu, kama unaona hatari ipo karibu bora uifanyie timing, don't procrastinate kwa sababu ukifanyiwa timing ww ni kifo, kama sisi tulikuwa ni wanafunzi na tulitumia jembe, sululu na mawe kumuua na nyie tafuteni namna afe hata kama ni Mali ya mtu au ni mtu kajibadilisha kuwa chatu, naamini mna resources kuliko hata tulizokuwa nazo sisi.