Chatu mkubwa katika pori jirani na 'Chuo Nyeti' Mbweni Malindi adhibitiwe upesi kabla hajaleta madhara

Chatu mkubwa katika pori jirani na 'Chuo Nyeti' Mbweni Malindi adhibitiwe upesi kabla hajaleta madhara

Watu wa Dar ni kutumia akili na siyo nguvu. Wamikoani kila siku ndoto zao ni kuja Dar wakati wa Dar ndoto zao ni kwenda mbele. Nyie wa mikoani njooni mumue huyo Chatu sisi tutakuwa tunawaongoza kwenye jambo lenye kuhitaji akili
Ishu za kwenda huko unapoita mbele ndio zilinifanya nikapajua dar kinyume na apo nisingetaka ata kufika dar.
 
Wengi wanaojitia ujasiri hapa ni waoga wa kutupwa kwenye uhalisia, kwa aliyewahi kukutana na hayo madubwana anga zao sidhani kama ataweza kukejeli hatari yake.

Kuna sehemu ilikuwa ni lazima tufike ila tukaambiwa kuwa kuna joka linaonekanaga maeneo hayo hivyo tuwe makini, tulibeba kidumu cha mafuta ya taa kama silaha. Tulikuwa watatu tukawa tunasonga sasa tukafika mahali tukasikia kama majani yanacheza ebwana wee yule mwenzetu aliebeba kidumu alikitupa sasa wote tulijikuta tunakimbia spidi za ajabu kama wajinga.
 
Mpumbavu kama huyo na Wenzake baadhi unaowaona hapa ( Waliochangia ) waelewe nini Mkuu?

Wewe ndiyo uliyeuelewa vyema huu Uzi na Kuchangia Kiumakini na kwa tahadhari Kubwa ya huyo Chatu ambayo GENTAMYCINE nimeitoa / nimeileta hapa JamiiForums kwa nia njema tu ili nisaidie na niokoe Wengine wasije Kudhurika nae.
Nasikia wewe unapenda kukatikia chatu za wanaume wenzio, elewa maana ya neno chatu GENTAMYCIME
 
Takataka tu. Mkilewa kila mtu kitengo au anakijua kitengo kuliko wao.
 
Mida yake ya kuvuka barabara hiyo ya lami ni kati ya saa 2 hadi Saa 3 usiku na ni mkubwa sana.

Nina uhakika wale wote wanaopita hiyo njia wakiwa ama katika Bajaji au Pikipiki za Bodaboda au DalaDala za Mbweni - Makumbusho au hata gari binafsi ama mmeshawahi kukutana nae au nanyi hivi karibuni tu mtakutana nae.

Ushauri wangu kama GENTAMYCINE kwa taasisi zote kuu mbili nyeti nchini Tanzania ni kwamba kwakuwa mji unakuwa na watu wanahamia maemeo yaliyokuwa ni maalum kwa mafunzo yao (Maporini/Misituni) basi ikiwapendeza wawe wanahamishia hayo mapori mafunzo yao maeneo ya mbali zaidi ili viumbe hatari kama huyu chatu (joka kubwa) wasiwe hatarishi kwa wananchi / wakazi.
Nyoka wa plastiki huyo asikutishe
 
Chatu akamatwe apelekwe zoo. Lakini sijui Mbweni gani unayoizungumzia. Kwa sababu mini napenda sana kutembea maeneo ya Tegeta na Bunju.
Na mini nina experience ya chatu kijijini. Chatu alinisogelea up to a distance of one metre( or less) kabla sijakimbia.
 
Zamani niliamin JF Kuna watu wenye upeo mkubwa sana kumbe tofauti.Mtu anatoa tahadhari watu tunaleta mizaha ya kiwaki kabisa.Anyway Kwa akili hizi hata mkiachiwa bandari mtaifanyia Nini?
 
Kuna kipindi enzi za magazeti ya alasiri na dar leo chatu alitoka bonde la msimbazi na kuingia hosp ya muhimbili akakutwa na langoni wodi ya sewahaji.Mwaka huu huku mtoni kijichi aliuwawa chatu akiwa ndani ya fensi.Cha kutafakari ni kama ameuawa mmoja basi hawezi kuwa peke ake.
 
Chatu akamatwe apelekwe zoo. Lakini sijui Mbweni gani unayoizungumzia. Kwa sababu mini napenda sana kutembea maeneo ya Tegeta na Bunju.
Na mini nina experience ya chatu kijijini. Chatu alinisogelea up to a distance of one metre( or less) kabla sijakimbia.
Nimeshasema ( Kuandika ) katika Maelezo hapo juu kuwa ni Mbweni ya Malindi kilipo Chuo Kikubwa cha Mafunzo ya Wana Usalama wa Taifa ( TISS ) ukiachilia vile vya Dodoma na Zanzibar je, hukuona au unataka tu Kunikera kwani ni kama vile Unanisanifu.
 
Duniani kuna watu ni exceptional ndiyo maana kuna watu wanaokaa Dar lakini wanatamani kwenda kukaa bush
 
Nimeshasema ( Kuandika ) katika Maelezo hapo juu kuwa ni Mbweni ya Malindi kilipo Chuo Kikubwa cha Mafunzo ya Wana Usalama wa Taifa ( TISS ) ukiachilia vile vya Dodoma na Zanzibar je, hukuona au unataka tu Kunikera kwani ni kama vile Unanisanifu.
Jana usiku nimemuota Netanyahu. Tulikuwa ndani ya ndege. He was in the seat next to me.
 
....Haumi. Anakubana Mbavu Mpaka huwezi kupumua. Unakufa na anakumeza Mzima Mzima bila Kukutafuna ! [emoji26]
Hivi(nilimuota tu sijawahi kumuona).
-Anapendelea kukaa mazingira gani?
-Je,ana ukubwa gani(na urefu)
-Anatoa wapi nguvu ya kubana mtu mpaka ashindwe kupumua? Mbali na wanyama wadogo wadogo au hata watoto,anaweza akamuua mtu mzima hivi hivi?
 
Back
Top Bottom